Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.
Basi kama tulivyoona kwenye sehemu iliyopita kwamba Rhoda baada ya kuambiwa kwamba hakuna mwanamke mzuri duniani kama wewe alilia mno bila kunyamaza kama masaa matatu hivi na wakamwacha akalia hiyo ilikuwa ni dalili ya kuondoa maumivu yaliyompata, aliyemwambia maneno hayo alikuwa ameandaliwa kusudi amwambie ili kuona matokea au jinsi atakavyopokea neno hilo, wakaamua kuendesha gari huku Rhoda akilia mpaka nyumbani, baada ya kumaliza kulia alitumia siku nane bila kuongea na mtu yeyote ila kwa siku hizo alikuwa na uwezo wa kuoga ,kufua ,kusafisha chumba chake na kufanya shughuli mbalimbali hapo nyumbani bila kuongea na mtu yeyote, na akaanza kuwasogelea hata watoto wa kiume kwa sababu hapo awali alikuwa hapendi kuona jinsia ya kiume na alianza kushiriki chakula na familia ila akiwa kimya.
Baada ya wataalamu wa saikolojia walikuja kuangalia maendeleo ya mgonjwa wao walikuta yuko kwenye hali ya usafi na alikuwa haongei,yule dada akavaa nguo alizokuwa anampenda kuvaa Rhoda akiwa bado yupo na akili nzuri,Rhoda alifurahi sana na yeye akavalishwa nguo ila akazivua akaenda nazo chumbani mwake akaoga akanawa akavaa na kupendeza basi wale wanasaikolojia wakamwambia apande kwenye gari akajipandisha mwenyewe wakaenda Rock City, walipofika pale akakutana na watu anaowafahamu akawasalimia wakaenda hotelini akaagiza chakula ambacho ni chips na kuku akakaa kwa heshima wakala akaanza kupiga story kama kawaida na walipomaliza kula wakaenda kwenye swimming pool akaogelea vizuri na ilipofika saa kumi na mbili akawaambia waondoke usiku umeingia.
Kabla hawajaingia kwenye gari aliwasihii wamnunulie nguo, alisema mda wote niliokaa nyumbani sikuwa na nguo kwa kuwa sasa nitaanza kutembea kwa watu naomba na mimi mnisaidie ni pate nguo nzuri, wakampigia baba simu wakamtaarifu kuhusu kinachoendelea baba alifurahi sana akatuma Hela ya kutosha wakampatia mwenyewe akaanza kununua alipomaliza akafunga vizuri akaweka kwenye gari wakaondoka akaomba mziki wakamwekea akaenda anaimba mpaka nyumbani, alipofika nyumbani akawasalimia, akamshukuru sana baba yake akachukua nguo akaenda kufua,akaoga na akaja kuongea na wanasaikolojia na walipotaka kuondoka akawasindikiza nje wakaenda na yeye akarudi ndani.
Kadri siku zilivyokuwa zinaenda akili yake ilirudi kabisa n mpaka sasa huyo dada yupo anaendelea na Kazi yake kwenye bank ila shida hapendi kutolewa , kwa hiyo wasomaji wote wa story hii ni ya ukweli kabisa na kama kuna mtu ambaye ameumizwa na tatizo lolote anione Ili kuweza kupata matibabu kutokana na wataalamu wa kisaikolojia, ila pia kutokana na story hii nawasihi sana watoto wa kike kama mvulana au boyfriend wako ana mpango wa kukuoa na unaona Kuna nia kweli jaribu kujiwekea misimamo ya maisha kwa sababu Moses alimpenda Rhoda ila kwa sababu ya hali Ile ya kutoa mimba mara kwa mara ilimfanya amwache kwa kuhofia kukosa watoto.
Vile vile na watoto wa kiume jaribu kuwa na huruma jamani hata kama msichana unaona hutaweza kumuoa usimwaribie maisha ,kama Moses angekuwa na moyo wa upendo na huruma kwa Rhoda pale walipobebeshana mimba wakiwa chuoni wangekubali kutunza hiyo mimba na kuendelea na masomo hatimaye baadae wangeoana, kwa sababu kitendo ambacho Moses alimfanyia Rhoda sio kizuri kwa sababu kimegharimu maisha yake na kufanya hata familia kutengwa na jamii,kwa hiyo inawezekana kitendo cha kumwacha Rhoda na kukimbilia mwanamke mwingine kwa wazo la kupata watoto inawezekana na kwa mwanamke aliyemuoa wasipate watoto kwa sababu damu ya zile mimba Bado unalia na pia Moses anapaswa kukumbuka machozi na mateso sliyoyapitia Rhoda ,kwa hiyo achana na tabia ya kuchezea maisha ya wenzenu miliojidai kwamba mnapendana.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mtihani unafika ila Jackie hakujiandaa alishutuliwa na marafiki zake baada ya kuona mwenendo wake haueleweki.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hadithi ya Binti mfalme ni hadithi ya kusisimua, kuhusu hadithi hii ni kwamba mfalme alihitaji mtoto wa kiume ila wanawake wote hawakumpata ila alitokea mke mdogo mmoja wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha mmoja wa kiume na
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il
Soma Zaidi...Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .
Soma Zaidi...Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambao walipoteana katika hali za kukimbizwa na wazazi Ili waweze kutimiza ndoto zao na siku wakakutana wakiwa watu wazima.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.
Soma Zaidi...Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina.
Soma Zaidi...