USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Basi kama tulivyoona kwenye sehemu iliyopita kwamba Rhoda baada ya kuambiwa kwamba hakuna mwanamke mzuri duniani kama wewe alilia mno bila kunyamaza kama masaa matatu hivi na wakamwacha akalia hiyo ilikuwa ni dalili ya kuondoa maumivu yaliyompata, aliyemwambia maneno hayo alikuwa ameandaliwa kusudi amwambie ili kuona matokea au jinsi atakavyopokea neno hilo, wakaamua kuendesha gari huku Rhoda akilia mpaka nyumbani, baada ya kumaliza kulia alitumia siku nane bila kuongea na mtu yeyote  ila kwa siku hizo alikuwa na uwezo wa kuoga ,kufua ,kusafisha chumba chake na kufanya shughuli mbalimbali hapo nyumbani bila kuongea na mtu yeyote, na akaanza kuwasogelea hata watoto wa kiume kwa sababu hapo awali alikuwa hapendi kuona jinsia ya kiume na alianza kushiriki chakula na familia ila akiwa kimya.

 

Baada ya wataalamu wa saikolojia walikuja kuangalia maendeleo ya mgonjwa wao walikuta yuko kwenye hali ya usafi na alikuwa haongei,yule dada akavaa nguo alizokuwa anampenda kuvaa Rhoda akiwa bado yupo na akili nzuri,Rhoda alifurahi sana na yeye akavalishwa nguo ila akazivua akaenda nazo chumbani mwake akaoga akanawa akavaa na kupendeza basi wale wanasaikolojia wakamwambia apande kwenye gari akajipandisha mwenyewe wakaenda Rock City, walipofika pale akakutana na watu anaowafahamu akawasalimia wakaenda hotelini akaagiza chakula ambacho ni chips na kuku akakaa kwa heshima wakala akaanza kupiga story kama kawaida na walipomaliza kula wakaenda kwenye swimming pool akaogelea vizuri na ilipofika saa kumi na mbili akawaambia waondoke usiku umeingia.

 

Kabla hawajaingia kwenye gari aliwasihii wamnunulie nguo, alisema mda wote niliokaa nyumbani sikuwa na nguo kwa kuwa sasa nitaanza kutembea kwa watu naomba na mimi mnisaidie ni pate nguo nzuri, wakampigia baba simu wakamtaarifu kuhusu kinachoendelea baba alifurahi sana akatuma Hela ya kutosha wakampatia mwenyewe akaanza kununua alipomaliza akafunga vizuri akaweka kwenye gari wakaondoka akaomba mziki wakamwekea akaenda anaimba mpaka nyumbani, alipofika nyumbani akawasalimia, akamshukuru sana baba yake akachukua nguo akaenda kufua,akaoga na akaja kuongea na wanasaikolojia na walipotaka kuondoka akawasindikiza nje wakaenda na yeye akarudi ndani.

 

Kadri siku zilivyokuwa zinaenda akili yake ilirudi kabisa n mpaka sasa huyo dada yupo anaendelea na Kazi yake kwenye bank ila shida hapendi kutolewa , kwa hiyo wasomaji wote wa story hii ni ya ukweli kabisa na kama kuna mtu ambaye ameumizwa na tatizo lolote anione Ili kuweza kupata matibabu kutokana na wataalamu wa kisaikolojia, ila pia kutokana na story hii nawasihi sana watoto wa kike  kama mvulana au boyfriend wako ana mpango wa kukuoa na unaona Kuna nia kweli jaribu kujiwekea misimamo ya maisha kwa sababu Moses alimpenda Rhoda ila kwa sababu ya hali Ile ya kutoa mimba mara kwa mara ilimfanya  amwache kwa kuhofia kukosa watoto.

 

Vile vile na watoto wa kiume jaribu kuwa na huruma jamani hata kama msichana unaona hutaweza kumuoa usimwaribie maisha ,kama Moses angekuwa na moyo wa upendo na huruma kwa Rhoda pale walipobebeshana mimba wakiwa chuoni wangekubali kutunza hiyo mimba na kuendelea na masomo hatimaye baadae wangeoana, kwa sababu kitendo ambacho Moses alimfanyia Rhoda sio kizuri kwa sababu kimegharimu maisha yake na kufanya hata familia kutengwa na jamii,kwa hiyo inawezekana kitendo cha kumwacha Rhoda na kukimbilia mwanamke mwingine kwa wazo la kupata watoto inawezekana na kwa mwanamke aliyemuoa wasipate watoto kwa sababu damu ya zile mimba Bado unalia na pia Moses anapaswa kukumbuka machozi na mateso sliyoyapitia Rhoda ,kwa hiyo achana na tabia ya kuchezea maisha ya wenzenu miliojidai kwamba mnapendana.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 1214

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

NIMLAUMU NANI part 1

Post hii inahusu hadithi Moja ya kijana maaalufu aliyeitwa Frank, ni kijana aliyekuwa mwaminifu ila amekumbana na wasichana wengi wanamasaliti ukizingatia Frank alikuwa kijana mstaalabu na mwaminifu sana ila anafikia kufanya maamuzi magumu kufuatana na ku

Soma Zaidi...
NIMLAUM NANI? (Sehemu ya pili)

Post hii ni mwendelezo wa hadithi iliyopita ambapo Frank aliwakuta Amina ambaye ni mpenzi wake ameumbatiana na James ambaye ni rafiki yake ,kwa hiyo tuendelee kusikia yaliyotokea baada ya Amina na James kukutwa na Franki.

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)

Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa.

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 3)

Posti hii inahusu zaidi hasara za kuwa na wivu na kutokuwa wazi, sehemu hii inahusu zaidi maendeleo ya Lisa shuleni yanakuwa mabaya zaidi na lina anaendelea kumtunzia siri lengo lake lina ni kuendelea kuwa wa kwanza darasani.

Soma Zaidi...
Chemsha bongo na bongoclass

Jipime uwezo wako wa kufikiri pamoja nasi.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)

Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto.

Soma Zaidi...
Hadithi za alif lela u lela

Haya ni masimulizi ya Hadithi za alif lela u lela

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mtihani unafika ila Jackie hakujiandaa alishutuliwa na marafiki zake baada ya kuona mwenendo wake haueleweki.

Soma Zaidi...
Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.

Soma Zaidi...