image

USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Basi kama tulivyoona kwenye sehemu iliyopita kwamba Rhoda baada ya kuambiwa kwamba hakuna mwanamke mzuri duniani kama wewe alilia mno bila kunyamaza kama masaa matatu hivi na wakamwacha akalia hiyo ilikuwa ni dalili ya kuondoa maumivu yaliyompata, aliyemwambia maneno hayo alikuwa ameandaliwa kusudi amwambie ili kuona matokea au jinsi atakavyopokea neno hilo, wakaamua kuendesha gari huku Rhoda akilia mpaka nyumbani, baada ya kumaliza kulia alitumia siku nane bila kuongea na mtu yeyote  ila kwa siku hizo alikuwa na uwezo wa kuoga ,kufua ,kusafisha chumba chake na kufanya shughuli mbalimbali hapo nyumbani bila kuongea na mtu yeyote, na akaanza kuwasogelea hata watoto wa kiume kwa sababu hapo awali alikuwa hapendi kuona jinsia ya kiume na alianza kushiriki chakula na familia ila akiwa kimya.

 

Baada ya wataalamu wa saikolojia walikuja kuangalia maendeleo ya mgonjwa wao walikuta yuko kwenye hali ya usafi na alikuwa haongei,yule dada akavaa nguo alizokuwa anampenda kuvaa Rhoda akiwa bado yupo na akili nzuri,Rhoda alifurahi sana na yeye akavalishwa nguo ila akazivua akaenda nazo chumbani mwake akaoga akanawa akavaa na kupendeza basi wale wanasaikolojia wakamwambia apande kwenye gari akajipandisha mwenyewe wakaenda Rock City, walipofika pale akakutana na watu anaowafahamu akawasalimia wakaenda hotelini akaagiza chakula ambacho ni chips na kuku akakaa kwa heshima wakala akaanza kupiga story kama kawaida na walipomaliza kula wakaenda kwenye swimming pool akaogelea vizuri na ilipofika saa kumi na mbili akawaambia waondoke usiku umeingia.

 

Kabla hawajaingia kwenye gari aliwasihii wamnunulie nguo, alisema mda wote niliokaa nyumbani sikuwa na nguo kwa kuwa sasa nitaanza kutembea kwa watu naomba na mimi mnisaidie ni pate nguo nzuri, wakampigia baba simu wakamtaarifu kuhusu kinachoendelea baba alifurahi sana akatuma Hela ya kutosha wakampatia mwenyewe akaanza kununua alipomaliza akafunga vizuri akaweka kwenye gari wakaondoka akaomba mziki wakamwekea akaenda anaimba mpaka nyumbani, alipofika nyumbani akawasalimia, akamshukuru sana baba yake akachukua nguo akaenda kufua,akaoga na akaja kuongea na wanasaikolojia na walipotaka kuondoka akawasindikiza nje wakaenda na yeye akarudi ndani.

 

Kadri siku zilivyokuwa zinaenda akili yake ilirudi kabisa n mpaka sasa huyo dada yupo anaendelea na Kazi yake kwenye bank ila shida hapendi kutolewa , kwa hiyo wasomaji wote wa story hii ni ya ukweli kabisa na kama kuna mtu ambaye ameumizwa na tatizo lolote anione Ili kuweza kupata matibabu kutokana na wataalamu wa kisaikolojia, ila pia kutokana na story hii nawasihi sana watoto wa kike  kama mvulana au boyfriend wako ana mpango wa kukuoa na unaona Kuna nia kweli jaribu kujiwekea misimamo ya maisha kwa sababu Moses alimpenda Rhoda ila kwa sababu ya hali Ile ya kutoa mimba mara kwa mara ilimfanya  amwache kwa kuhofia kukosa watoto.

 

Vile vile na watoto wa kiume jaribu kuwa na huruma jamani hata kama msichana unaona hutaweza kumuoa usimwaribie maisha ,kama Moses angekuwa na moyo wa upendo na huruma kwa Rhoda pale walipobebeshana mimba wakiwa chuoni wangekubali kutunza hiyo mimba na kuendelea na masomo hatimaye baadae wangeoana, kwa sababu kitendo ambacho Moses alimfanyia Rhoda sio kizuri kwa sababu kimegharimu maisha yake na kufanya hata familia kutengwa na jamii,kwa hiyo inawezekana kitendo cha kumwacha Rhoda na kukimbilia mwanamke mwingine kwa wazo la kupata watoto inawezekana na kwa mwanamke aliyemuoa wasipate watoto kwa sababu damu ya zile mimba Bado unalia na pia Moses anapaswa kukumbuka machozi na mateso sliyoyapitia Rhoda ,kwa hiyo achana na tabia ya kuchezea maisha ya wenzenu miliojidai kwamba mnapendana.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1075


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

SAFARI YA MUUJIZA ( SEHEMU YA PILI)
Post hii ni mwendelezo wa hadithi ya safari yenye muujiza ,ni pale mtoto ya Mungu mengi anafika kwenye kituo Cha ntonga na kuona yake mazingira na kufahamu njia ya kwenda kule. Soma Zaidi...

NIMLAUM NANI? (Sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelezo wa hadithi iliyopita ambapo Frank aliwakuta Amina ambaye ni mpenzi wake ameumbatiana na James ambaye ni rafiki yake ,kwa hiyo tuendelee kusikia yaliyotokea baada ya Amina na James kukutwa na Franki. Soma Zaidi...

Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini. Soma Zaidi...

Hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya Binti mfalme ni hadithi ya kusisimua, kuhusu hadithi hii ni kwamba mfalme alihitaji mtoto wa kiume ila wanawake wote hawakumpata ila alitokea mke mdogo mmoja wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha mmoja wa kiume na Soma Zaidi...

USALITI (sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo Soma Zaidi...

SAFARI YA MUUJIZA
Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto. Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI part 1
Post hii inahusu hadithi Moja ya kijana maaalufu aliyeitwa Frank, ni kijana aliyekuwa mwaminifu ila amekumbana na wasichana wengi wanamasaliti ukizingatia Frank alikuwa kijana mstaalabu na mwaminifu sana ila anafikia kufanya maamuzi magumu kufuatana na ku Soma Zaidi...

WAKATI WA KUFUMBUKA
Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha. Soma Zaidi...

Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)
Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa. Soma Zaidi...

Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi. Soma Zaidi...