Ni nani kama mama

Ni nani kama mama

Nani kama mama? Hadithi hii itakufunza umuhimu wa kuwa muwazi kuhusu familia yako.

Binti mmoja alizaliwa na kulelewa na Mama ambaye ni kichaa wale wakuzunguka na kuokota vitu barabarani, pamoja na ukichaa wake lakini yule mama alimlea vizuri binti yake akimpa chakula mpaka alipofikia umri wa kwenda shule. Kwa bahati nzuri yule binti alipata msamaria mwema ambaye alimsomesha, ingawa yule msamaria mwema alijaribu kumchukua yule Mama na kukaa naye lakini haikusaidia.
 
 
Kila aliporudishwa nyumbani siku mbili alirudi mtaani kuokota makopo na kula matakataka. Pamoja na ukichaa wake lakini kila siku ilikuwa ni lazima kwenda kwenye ile nyumba alikokuwa akilelewa binti yake kumsalimia na kila siku alikuwa akibeba chakula kwaajili ya binti yake.
 
 
Ili binti yule ale kile chakula illibidi kila siku kumuwekea chakula kizuri kwenye mfuko na pale alipokuwa akiomba basi walimpa kile chakula na yeye kabla ya kula alimletea binti yake. Maisha yaliendelea hivyo mpaka binti alipoenda chuo ndipo Mama alibaki mpweke akizunguka zunguka tu mtaani. Kule chuoni binti alifanya vizuri na alipomaliza chuo alifanikiwa kupata mchumba.
Alirudi kumtambulisha kwa wale wazazi waliomlea, lakini chakushangaza tusiku aliyorudi kumtambulisha mchumba wake na Mama yake alikuepo. kwa uoga na aibu aligoma kabisa kumtambulisha, ingawa yule mama alimng'ang'ania lakini alidanganya kuwa ni kichaa tu ambaye alizoea kumpa zawadi. Siku iliisha na mipango ya harusi ikafanyika, baada ya miezi mitatu ikafanyika harudi kubwa na ya kifahari.
 
 
Wakiwa katikati ya sherehe binti alishangaa kumuona Mama yake anaingia akiwa maevaa nguo zake chafu vilevile, Mama alisogea mpaka mbele watu wakimshangaa akatoa mfuko wake wa chakula na kumkabidhi binti yake ili ale. Binti aliukataa na kuanza kupiga kelele lakini kabla hajafanya chochote Mume wake aliuchukua ule mfuko na kuufungua kisha kuanza kukila kile chakula.
 
 
Watu wote walishtuka na kuanza kushangaa, lakini yule bwana harusi alichukua Mic na kusema. Huyu ndiye Mama mkwe wangu, Mama mzaa chema. Najua mnamshangaa na hali yake lakini kwa hali hii hii ndiyo alimza na kumlea mke wangu na ndiye atakuwa Bibi wa watoto wangu" Kila mtu alibaki kushangaa hata yule binti alishangaa huku machozi ya kimtoka, yule kijana alimgeukia mkewe.
 
 
"Najua sababau za wewe kuficha lakini unapaswa kutambua kuwa nakupenda na nampenda Mama yako kama vile ninavyompenda Mama yangu. Ulimwengu mzima utamuona kichaa lakini yeye ndiye aliyekuzaa na kukufanya uwe hivi leo. Unavyoniona hivi Baba yangu alinizaa na kunitelekeza, pamoja na pesa zake akili zake lakini alinitelekeza, sasa hembu jiulize kichaa ni nani kati ya mwanaume aliyetelekeza mwanae au Mama kama huyu ambaye mpaka leo anajua bado ni mtoto na anakujali kwa chakula?"
 
 
Ukumbi mzima uliibuka kwa vifijo, watu wakishangilia biti akiwa anatokwa na machozi alimkumbatia Mama yake, alichukua kile chakula na wote wakaanza kukila. Yule kijana ndiyo alimualika kwani siku aliyoenda kutambulishwa na kumuona alihisi kitu hivyo akaamua kufuatilia mpaka alipoujua ukweli. Alijua sababu ya mchumba wake kuficha lakini alitaka ulimwengu mzima kujua kuwa hajali na anampenda bila kujali historia yake.
 
HAKUNA KAMA MAMA, UPENDO WAKE HAUNUNULIWI WALA HAUPUNGUI USICHOKE KUMUAMBIA NAMNA UNAVYOMPENDA.

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Emmanueli image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 468

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi ( sehemu ya 2)
Hasara za wivu na kutokuwa wazi ( sehemu ya 2)

Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu na kutokuwa wazi sehemu ya pili, sehemu hii inahusu mama Lisa anaenda kwa mama lina ili kuuliza kinachoendelea kwa mtoto wake , kwa hiyo tuona atapata jibu gani.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili
Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili baada ya kuhamia shule mpya.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara.

Soma Zaidi...
Mahusiano ya vijana wawili
Mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya kwanza)
USALITI (sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA
SAFARI YA MUUJIZA

Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu

Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.

Soma Zaidi...
Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.

Soma Zaidi...