Ni nani kama mama

Ni nani kama mama

Nani kama mama? Hadithi hii itakufunza umuhimu wa kuwa muwazi kuhusu familia yako.

Binti mmoja alizaliwa na kulelewa na Mama ambaye ni kichaa wale wakuzunguka na kuokota vitu barabarani, pamoja na ukichaa wake lakini yule mama alimlea vizuri binti yake akimpa chakula mpaka alipofikia umri wa kwenda shule. Kwa bahati nzuri yule binti alipata msamaria mwema ambaye alimsomesha, ingawa yule msamaria mwema alijaribu kumchukua yule Mama na kukaa naye lakini haikusaidia.
 
 
Kila aliporudishwa nyumbani siku mbili alirudi mtaani kuokota makopo na kula matakataka. Pamoja na ukichaa wake lakini kila siku ilikuwa ni lazima kwenda kwenye ile nyumba alikokuwa akilelewa binti yake kumsalimia na kila siku alikuwa akibeba chakula kwaajili ya binti yake.
 
 
Ili binti yule ale kile chakula illibidi kila siku kumuwekea chakula kizuri kwenye mfuko na pale alipokuwa akiomba basi walimpa kile chakula na yeye kabla ya kula alimletea binti yake. Maisha yaliendelea hivyo mpaka binti alipoenda chuo ndipo Mama alibaki mpweke akizunguka zunguka tu mtaani. Kule chuoni binti alifanya vizuri na alipomaliza chuo alifanikiwa kupata mchumba.
Alirudi kumtambulisha kwa wale wazazi waliomlea, lakini chakushangaza tusiku aliyorudi kumtambulisha mchumba wake na Mama yake alikuepo. kwa uoga na aibu aligoma kabisa kumtambulisha, ingawa yule mama alimng'ang'ania lakini alidanganya kuwa ni kichaa tu ambaye alizoea kumpa zawadi. Siku iliisha na mipango ya harusi ikafanyika, baada ya miezi mitatu ikafanyika harudi kubwa na ya kifahari.
 
 
Wakiwa katikati ya sherehe binti alishangaa kumuona Mama yake anaingia akiwa maevaa nguo zake chafu vilevile, Mama alisogea mpaka mbele watu wakimshangaa akatoa mfuko wake wa chakula na kumkabidhi binti yake ili ale. Binti aliukataa na kuanza kupiga kelele lakini kabla hajafanya chochote Mume wake aliuchukua ule mfuko na kuufungua kisha kuanza kukila kile chakula.
 
 
Watu wote walishtuka na kuanza kushangaa, lakini yule bwana harusi alichukua Mic na kusema. Huyu ndiye Mama mkwe wangu, Mama mzaa chema. Najua mnamshangaa na hali yake lakini kwa hali hii hii ndiyo alimza na kumlea mke wangu na ndiye atakuwa Bibi wa watoto wangu" Kila mtu alibaki kushangaa hata yule binti alishangaa huku machozi ya kimtoka, yule kijana alimgeukia mkewe.
 
 
"Najua sababau za wewe kuficha lakini unapaswa kutambua kuwa nakupenda na nampenda Mama yako kama vile ninavyompenda Mama yangu. Ulimwengu mzima utamuona kichaa lakini yeye ndiye aliyekuzaa na kukufanya uwe hivi leo. Unavyoniona hivi Baba yangu alinizaa na kunitelekeza, pamoja na pesa zake akili zake lakini alinitelekeza, sasa hembu jiulize kichaa ni nani kati ya mwanaume aliyetelekeza mwanae au Mama kama huyu ambaye mpaka leo anajua bado ni mtoto na anakujali kwa chakula?"
 
 
Ukumbi mzima uliibuka kwa vifijo, watu wakishangilia biti akiwa anatokwa na machozi alimkumbatia Mama yake, alichukua kile chakula na wote wakaanza kukila. Yule kijana ndiyo alimualika kwani siku aliyoenda kutambulishwa na kumuona alihisi kitu hivyo akaamua kufuatilia mpaka alipoujua ukweli. Alijua sababu ya mchumba wake kuficha lakini alitaka ulimwengu mzima kujua kuwa hajali na anampenda bila kujali historia yake.
 
HAKUNA KAMA MAMA, UPENDO WAKE HAUNUNULIWI WALA HAUPUNGUI USICHOKE KUMUAMBIA NAMNA UNAVYOMPENDA.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Emmanueli image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 407

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, hapa tunaona Jackie anajibu barua ya Julius kwa kusema yafuatayo.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI part 1
NIMLAUMU NANI part 1

Post hii inahusu hadithi Moja ya kijana maaalufu aliyeitwa Frank, ni kijana aliyekuwa mwaminifu ila amekumbana na wasichana wengi wanamasaliti ukizingatia Frank alikuwa kijana mstaalabu na mwaminifu sana ila anafikia kufanya maamuzi magumu kufuatana na ku

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il

Soma Zaidi...
Mahusiano ya vijana wawili
Mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake.

Soma Zaidi...
Hadithi katika kijiji cha burugo
Hadithi katika kijiji cha burugo

Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)

Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu

Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mtihani unafika ila Jackie hakujiandaa alishutuliwa na marafiki zake baada ya kuona mwenendo wake haueleweki.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili
Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili baada ya kuhamia shule mpya.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambao walipoteana katika hali za kukimbizwa na wazazi Ili waweze kutimiza ndoto zao na siku wakakutana wakiwa watu wazima.

Soma Zaidi...