Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 3)

Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 3)

Posti hii inahusu zaidi hasara za kuwa na wivu na kutokuwa wazi, sehemu hii inahusu zaidi maendeleo ya Lisa shuleni yanakuwa mabaya zaidi na lina anaendelea kumtunzia siri lengo lake lina ni kuendelea kuwa wa kwanza darasani.

Download Post hii hapa

Hasara za wivu na kutokuwa wazi.

1. Basi Lisa akawa jambazi kabisa na siku nyingine akawa anatoka nyumbani usiku na kwenda kwa mpenzi wake na akigunduliwa na mama yake anamdanganya kwamba kuna mtu alinipeleka usiku,kweli mama Lisa akaumia kweli  na akaamua kwenda kwa mganga na waganga walivyo waongo, yule mganga akamwambia kwamba ni rafiki yako yaani mama lina ndiye anayemchezaea  mtoto wako, kwa hiyo mama Lisa akakumbuka na neno alilolisema lina siku Lisa anakuja aliumia mno kwa hiyo mama Lisa akaamua kwenda kwa mama lina akiwa na hasira kubwa na kulalamika kuhusu yote anayotendewa mwanae.

 

 

 

 

 

2. Basi mama lina akaumia sana na akaamua kumuuliza mwanae lina kwa nini Lisa anafeli darasani na lina alikosa jibu la kumpa mamae ila mama yake alipombana zaidi ndipo akaamua kumwambia kila kitu kwamba lisa aendagi darasani na anashinda na mvulana, kwa hiyo mama lina aliumia sana akataka kumwambia mama Lisa ila alikosa jinsi na baadae aliamua kumwambia ila mama Lisa alikataa kabisa, basi hali ya Lisa ikawa mbaya zaidi, na walipofanya mtihani wa kuingia darasa la saba alikuwa mtoto wa tisini na tano kati ya mia moja ila Lina alikuwa wa kwanza, mama Lisa akaongeza chuki zaidi juu ya lina na mamaye.

 

 

 

 

 

3. Basi mama Lisa akaenda kwa watu mbalimbali akitangaza kuwa mama lina ni mchawi na amemfundisha mwanae lina naye ni mchawi kwa hiyo watu wakachukia wakataka kumfukuza mama lina kwenye nzengo yao ila wakampa mwaka mmoja kusudi mtoto amalize shule na akimaliza hawataki kumwona pale, kwa sababu baba yake  lini alifariki lina akiwa mdogo kwa hiyo ilikuwa ni shida kubwa kwa mama lina kuhama pale kwa hiyo alitafuta sehemu kila kona na hakufanikiwa kwa sababu alikua hana kipato kikubwa cha kununua kiwanja kwa hiyo aliamua kumpigia mama wa kambo wa Lisa ili kumwambia kila kitu jinsi mke mwenza alivyofanyia .

 

 

 

 

4. Basi kwa sababu mama wa kambo wa Lisa lengo lake ni kuharibu maisha ya Lisa alipata nafasi nzuri ya kuharibu, kwa hiyo yule mama wa kambo wa Lisa alikuwa na pesa na alichokifanya ni kuhakikisha kujua ukweli kupitia kwa mama lina na kuhakikisha kwamba Lisa anaharbiwa kila kitu, kwa hiyo mama lina alipatiwa kiwanja na mama wa kambo wa Lisa na pia akamjengea nyumba nzuri na akasubiri mtoto wake amalize la saba wahamie huko, basi kwa sababu mama wa kambo wa Lisa alijua ukweli wote na tatizo la Lisa ,akaamua kumwambia mkewe kwamba wamlete tena mtoto nyumbani wamtafutie mwalimu awe anamfundishia nyumbani na baba Lisa akakubali.

 

 

 

 

5. Kwa hiyo mama wa kambo wa Lisa akamwambia nitamtafuta mwalimu na baba lisa akakubali, kwa hiyo mama wa kambo wa Lisa akamwendea  mama lina wakamtafuta yule mwalimu anayempenda Lisa wakaongea naye na kuhaidi kumlipa hela kubwa na kumpatia sehemu ya kuishi, na yule mwalimu akakubali kazi ile na Ela ilikuwa kubwa na kufika kuanza kazi akakuta mwanafunzi ni Lisa akafurahi sana kwa sababu alikuwa anatafuta alipo hakufanikiwa kumpata kwa sababu Lisa hakuwa na simu, basi yule mama wa kambo akamwambia baba Lisa kwamba Lisa anapaswa kuwa na chumba chake karibu na mwalimu ili akipata shida kimasomo mwalimu anafundisha, na baba Lisa akakubali lile ombi.

 

 

 

 

 

6. Basi maisha ya kusoma yakaanza siku zote Lisa alikuwa analala kwa yule mwalimu wake yaani walikuwa kama mke na mme na yule mama wa kambo wa Lisa alifahamu hilo akafurahi sana akatamani yule Lisa ababeshwe mimba na kuharibikiwa maisha ila kaka alikuwa makini, sasa ikafika siku ya kufanya mtihani wa robo muhula, kwa sababu yule kaka alikuwa anafundisha pale akaiba mitihani akasolve yote na Lisa na Lisa alipokuja kufanya mtihani akawa mtu wa tano ila lina alikuwa wa kwanza,baba yake akafurahi sana akampa yule kijana zawadi ila mama wa kambo wa Lisa hakufurahi kwa hiyo akaanza kumfanyia yule mwalimu visa na kuamua kumfukuza yule mwalimu na kumtafuta mwalimu mwingine kijana ambaye atamfundisha Lisa, ila Lisa kwa sababu alikuwa ni binti wa kuvutia alipendwa na yule kijana ila Lisa alikataa kwa sababu hisia zake zote zilikuwa kwa mwalimu wake.

 

 

 

 

 

7. Basi kwa sababu  ya hisia za Lisa  kwa mwalimu wake akamwambia yule mwalimu kijana kama utanisumbua nitamwambia baba, basi yule kijana akaanza kumfundisha kwa kumtugia mitihani migumu na Lisa anafeli na baba yake anamtukana kwamba hana akili ila yale maswali magumu yalimsaidia kuona maswali ya shule ni marahisi sana,kwa kipindi hicho maisha ya Lisa yakabadilika na akaanza kusoma na yule mama baada ya kuona juhudi za Lisa akaamua kumnunulia simu nzuri sana na kumwekea Salio la kutosha, hapo Lisa akafurahi sana na akaanza kuchati na yule mwalimu na akili zikaanza kupotea tena ila yule kijana siku moja akagundua hilo akapaswa kumsema kwa baba yake na baba alipoona hayo akagundua kwamba tatizo la mwanae ni lipi na akaamua kuonge na mama mzazi wa Lisa kuhusu tabia yake na ndipo mama Lisa aliona aibu na kujifanya kwamba hajui lolote.

 

 

 

 

 

8. Kwa sababu baba Lisa alimpenda sana binti yake aliamua kumwamisha bila kumwambia mama wa kambo wa Lisa na akampeleka shule za private akamrudisha darasa la tano, kwa sababu Lisa hakuwa na kitu kinachomsumbua akasoma kwa bidii kubwa na akafahamu kingereza na baada ya mwezi mmoja walimpeleka darasa la sita na akasoma vizuri bila shida na akawa anawazidi wanafunzi wengine na kufanya vizuri sana, kwa hiyo mama wake wa kambo hakujua mtoto yuko wapi na mama Lisa hakujua kwa sababu baba Lisa aliona wote hawana uwezo wa kumwambia mtoto wake ukweli ila watampoteza, ila kwa sababu yule binti alivutia yule kijana aliyemfundisha mara ya pili akawa anamfatilia kwa mbali na ndiye aliyemwambia baba yake ampeleke mbali na akina mama hao wawili.

 

 

 

 

 

9. Basi ikafika siku ya likizo yule kijana akamwambia baba Lisa kwamba yeye ana sehemu nzuri na akampeleka Lisa akawa anaishi naye akamshauri vizuri kuhusu kusoma na kutimiza ndoto na yule Lisa akamwelewa kabisa akawa anasoma na yule kijana alikuwa mkali sana kwa Lisa ila lengo lake ni kwamba baada ya Lisa kukaa vizuri na kumaliza aje awe mke wake, kwa hiyo Lisa alikaa huko na kusoma ila mama yake na mama wa kambo hawakujua Lisa yuko wapi,ila baba yake alisema mtoto yuko kwenye mikono salama,

 

 

 

 

 

10. Basi Lisa akafanya mtihani wa darasa la saba akafaulu vizuri na baba akampatia yule mwalimu zawadi nzuri kwa sababu ya kumtunza binti yake, sasa swali linabaki kichwani mwa baba je huyu binti pamoja na uzuri wake na akili yake ataenda kusoma wapi?.

 

 

 

itaendelea baadae

 

 

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 1010

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

SAFARI YA MUUJIZA
SAFARI YA MUUJIZA

Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI (sehemu ya nne)
NIMLAUMU NANI (sehemu ya nne)

Post hii inahusu zaidi kijana Frank anayelazimishwa kuolewa na Amisa yeye hayuko tayari ila kwa sababu ya maisha kuwa magumu anaamua kulala na Amina na kumbebesha Mimba ya watoto mapacha.

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)

Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa.

Soma Zaidi...
Hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Hadithi ya Mama mchoyo na mwehu

Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali

Soma Zaidi...
Hadithi ya Binti mfalme
Hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi hadithi ya Binti mfalme ni hadithi ya kusisimua, kuhusu hadithi hii ni kwamba mfalme alihitaji mtoto wa kiume ila wanawake wote hawakumpata ila alitokea mke mdogo mmoja wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha mmoja wa kiume na

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu

Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya tatu)
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya tatu)

Post hii inahusu zaidi mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini wakipanda gari kuelekea shule kuanza maisha mapya.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)

Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina.

Soma Zaidi...
Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)
Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto.

Soma Zaidi...