picha

Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi

Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.

Hasara za wivu na kutokuwa wazi.

1. Palikuwepo na wasichana wawili marafiki sana na waliofahamika pia kwa wazazi wao kuwa ni marafiki majina ya wasichana hao ni lisa na Lina ,urafiki wao ulitokana na wazazi wao waliishi sehemu moja na watoto hao walikua wanapendana kwa sababu ya wazazi wao pia walikuwa marafiki.

 

 

 

2.Watoto lina na Lisa wakiwa na miaka mitano walipelekwa kuanza chekechea walipelekwa na mama Lisa kuandikishwa kwa sababu ya kuzoeaana lina hakuona shida kwamba amepelekwa na mama Lisa shule kwa sababu alimwona kama mama yake pia, kwa hiyo mama Lisa aliwaandikisha na akawaacha pale shule na wakati wa kuondoka waliweza kurudi nyumbani kwa sababu hapakuwa mbali.

 

 

 

 

3. Siku zilienda na watoto hao wakawa wanasoma shule na matokeo yao yalikuwa mazuri mno na walikuwa hawaachani kila sehemu ukimwona lina kuna Lisa,na waalimu waliwapenda sana kwa sababu ya urafiki wao, nidhamu na pia ufaulu wao na kwa sababu walikuwa wadogo hawakuona shida kuishi na kupendana na kusaidiana katika kila kitu hasa kusoma pamoja na kucheza pamoja.

 

 

 

 

 

4. Basi watoto hao walipofika darasa la sita wakaanza kukua kimwili na kuanza kuwa na hisia hali ambayo iliwafanya kuwa tofauti kidogo kwa sababu palikuwepo na wanachuo wa mazoezi yaani kwa kitaalamu huitwa wanachuo wa field, yaani wale waliokuja kufanya mazoezi shuleni, mmoja kati yao akaanza mahusiano na Lisa ila Lisa hakumwambia lina na lina aliona kila kitu kinachoendelea kwa hiyo Lisa akapunguza kutembea na lina kwa sababu akihofu anaweza kumwambia mama yake.

 

 

 

 

5. Siku zikaendelea na Lisa akafanya mtihani akawa mtoto wa thelathini kati ya mia moja na siku zote alikuwa mtoto wa kwanza au wa pili walikuwa wanapisha na lina ,ila lina siku hiyo akawa wa kwanza mama Lisa akashangaa sana na alikuwa ameshashutuka kwa sababu Lisa alikuwa hana mahusiano mazuri na lina na siku hizo walikuwa hawasomi wala kucheza wote kama mwanzo, basi mama Lisa akaamua kwenda shule kwa waalimu kuuliza waalimu wakamwambia aende kwa lina atapata jibu kamili na waalimu walijua kila kitu ndipo mama Lisa akaenda kwa mama lina kupata jibu kamili.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/08/23/Tuesday - 07:58:29 am Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 1717

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 web hosting    πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na maskini (sehemu ya pili)

Post hii inahusu zaidi watoto wa wawili ambapo mmoja ni mtoto wa tajiri na mwingine ni mtoto wa maskini.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya nne)

Post hii inahusu zaidi watoto Hawa wawili wakiwa kwenye kituo cha mapumziko ambapo mtoto wa tajiri anabugia soda aliyopewa na yule mwalimu pia tumbo linaanza tena na anaanza kuendesha

Soma Zaidi...
Hadithi katika kijiji cha burugo

Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya pili)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu

Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, hapa tunaona Jackie anajibu barua ya Julius kwa kusema yafuatayo.

Soma Zaidi...