picha

Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi

Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.

Hasara za wivu na kutokuwa wazi.

1. Palikuwepo na wasichana wawili marafiki sana na waliofahamika pia kwa wazazi wao kuwa ni marafiki majina ya wasichana hao ni lisa na Lina ,urafiki wao ulitokana na wazazi wao waliishi sehemu moja na watoto hao walikua wanapendana kwa sababu ya wazazi wao pia walikuwa marafiki.

 

 

 

2.Watoto lina na Lisa wakiwa na miaka mitano walipelekwa kuanza chekechea walipelekwa na mama Lisa kuandikishwa kwa sababu ya kuzoeaana lina hakuona shida kwamba amepelekwa na mama Lisa shule kwa sababu alimwona kama mama yake pia, kwa hiyo mama Lisa aliwaandikisha na akawaacha pale shule na wakati wa kuondoka waliweza kurudi nyumbani kwa sababu hapakuwa mbali.

 

 

 

 

3. Siku zilienda na watoto hao wakawa wanasoma shule na matokeo yao yalikuwa mazuri mno na walikuwa hawaachani kila sehemu ukimwona lina kuna Lisa,na waalimu waliwapenda sana kwa sababu ya urafiki wao, nidhamu na pia ufaulu wao na kwa sababu walikuwa wadogo hawakuona shida kuishi na kupendana na kusaidiana katika kila kitu hasa kusoma pamoja na kucheza pamoja.

 

 

 

 

 

4. Basi watoto hao walipofika darasa la sita wakaanza kukua kimwili na kuanza kuwa na hisia hali ambayo iliwafanya kuwa tofauti kidogo kwa sababu palikuwepo na wanachuo wa mazoezi yaani kwa kitaalamu huitwa wanachuo wa field, yaani wale waliokuja kufanya mazoezi shuleni, mmoja kati yao akaanza mahusiano na Lisa ila Lisa hakumwambia lina na lina aliona kila kitu kinachoendelea kwa hiyo Lisa akapunguza kutembea na lina kwa sababu akihofu anaweza kumwambia mama yake.

 

 

 

 

5. Siku zikaendelea na Lisa akafanya mtihani akawa mtoto wa thelathini kati ya mia moja na siku zote alikuwa mtoto wa kwanza au wa pili walikuwa wanapisha na lina ,ila lina siku hiyo akawa wa kwanza mama Lisa akashangaa sana na alikuwa ameshashutuka kwa sababu Lisa alikuwa hana mahusiano mazuri na lina na siku hizo walikuwa hawasomi wala kucheza wote kama mwanzo, basi mama Lisa akaamua kwenda shule kwa waalimu kuuliza waalimu wakamwambia aende kwa lina atapata jibu kamili na waalimu walijua kila kitu ndipo mama Lisa akaenda kwa mama lina kupata jibu kamili.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/08/23/Tuesday - 07:58:29 am Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 1846

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu

Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)

Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, kuhusu hadithi hii ni pale Jackie anaandikiwa barua na Julius ili apotezwe akili na wavulana wengine kwa sababu Jackie aliwapita darasani.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA ( SEHEMU YA PILI)

Post hii ni mwendelezo wa hadithi ya safari yenye muujiza ,ni pale mtoto ya Mungu mengi anafika kwenye kituo Cha ntonga na kuona yake mazingira na kufahamu njia ya kwenda kule.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.

Soma Zaidi...
Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya tatu)

Post hii inahusu zaidi mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini wakipanda gari kuelekea shule kuanza maisha mapya.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto.

Soma Zaidi...
Hadithi ya Mama mchoyo na mwehu

Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 3)

Posti hii inahusu zaidi hasara za kuwa na wivu na kutokuwa wazi, sehemu hii inahusu zaidi maendeleo ya Lisa shuleni yanakuwa mabaya zaidi na lina anaendelea kumtunzia siri lengo lake lina ni kuendelea kuwa wa kwanza darasani.

Soma Zaidi...