HADITHI HII INAHUSU HASARA ZA WIVU NA KUTOKUWA WAZI


image


Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.


Hasara za wivu na kutokuwa wazi.

1. Palikuwepo na wasichana wawili marafiki sana na waliofahamika pia kwa wazazi wao kuwa ni marafiki majina ya wasichana hao ni lisa na Lina ,urafiki wao ulitokana na wazazi wao waliishi sehemu moja na watoto hao walikua wanapendana kwa sababu ya wazazi wao pia walikuwa marafiki.

 

 

 

2.Watoto lina na Lisa wakiwa na miaka mitano walipelekwa kuanza chekechea walipelekwa na mama Lisa kuandikishwa kwa sababu ya kuzoeaana lina hakuona shida kwamba amepelekwa na mama Lisa shule kwa sababu alimwona kama mama yake pia, kwa hiyo mama Lisa aliwaandikisha na akawaacha pale shule na wakati wa kuondoka waliweza kurudi nyumbani kwa sababu hapakuwa mbali.

 

 

 

 

3. Siku zilienda na watoto hao wakawa wanasoma shule na matokeo yao yalikuwa mazuri mno na walikuwa hawaachani kila sehemu ukimwona lina kuna Lisa,na waalimu waliwapenda sana kwa sababu ya urafiki wao, nidhamu na pia ufaulu wao na kwa sababu walikuwa wadogo hawakuona shida kuishi na kupendana na kusaidiana katika kila kitu hasa kusoma pamoja na kucheza pamoja.

 

 

 

 

 

4. Basi watoto hao walipofika darasa la sita wakaanza kukua kimwili na kuanza kuwa na hisia hali ambayo iliwafanya kuwa tofauti kidogo kwa sababu palikuwepo na wanachuo wa mazoezi yaani kwa kitaalamu huitwa wanachuo wa field, yaani wale waliokuja kufanya mazoezi shuleni, mmoja kati yao akaanza mahusiano na Lisa ila Lisa hakumwambia lina na lina aliona kila kitu kinachoendelea kwa hiyo Lisa akapunguza kutembea na lina kwa sababu akihofu anaweza kumwambia mama yake.

 

 

 

 

5. Siku zikaendelea na Lisa akafanya mtihani akawa mtoto wa thelathini kati ya mia moja na siku zote alikuwa mtoto wa kwanza au wa pili walikuwa wanapisha na lina ,ila lina siku hiyo akawa wa kwanza mama Lisa akashangaa sana na alikuwa ameshashutuka kwa sababu Lisa alikuwa hana mahusiano mazuri na lina na siku hizo walikuwa hawasomi wala kucheza wote kama mwanzo, basi mama Lisa akaamua kwenda shule kwa waalimu kuuliza waalimu wakamwambia aende kwa lina atapata jibu kamili na waalimu walijua kila kitu ndipo mama Lisa akaenda kwa mama lina kupata jibu kamili.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    2 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    3 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    6 Jifunze fiqh    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, hapa tunaona Jackie anajibu barua ya Julius kwa kusema yafuatayo. Soma Zaidi...

image Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi. Soma Zaidi...

image Hadithi ya kinyozi msiri wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Mrembo mtoto wa tajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Hatma ya kinyozi maishani mwangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Hadithi iliyosimuliwa na mshona nguo
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image USALITI (sehemu ya tatu)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi. Soma Zaidi...

image Kuelekea bonde la uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Nani muuaji?
Posti hii inakwenda kukusimulia kuhusu muuaji wa mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

image Hadithi ya tunda la tufaha (epo)
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...