Nguzo za Udhu



Allah (s.w) anatufunza kutia udhu katika aya ifuatayo:


Enyi mlioamini! Mnaposimama ili mkaswali, basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na (osheni) miguu yenu mpaka vifundoni...” (5:6)



Kutokana na aya hii na kutokana na mafundisho ya Mtume (s.a.w) nguzo au faradhi za udhu ni hizi zifuatazo
1. Kutia nia moyoni kuwa unatawadha.
2. Kuosha uso kwa ukamilifu kwa kufikisha maji mpaka kwenye mipaka yote ya uso.
3. Kuosha mikono miwili mpaka vifundoni.
4. Kupaka maji kichwani.
5. Kuosha miguu, mpaka vifundoni.
6. Kufuata utaratibu huu kwa kuanza (1) hadi (5) katika mfuatano huu.