lengo la kuswali za faradhi na suna

lengo la kuswali za faradhi na suna

Lengo la Kusimamisha Swala



Bila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake. Lengo la swala limebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo


“Soma uliyoletewa wahyi katika kitabu (Qur-an) na usimamishe swala. Bila shaka swala (ikiswaliwa vilivyo) humzuilia (mwenye kuswali na) mambo machafu na maovu, na kw a yakini kumbuko la Mw enyezi Mungu (lililomo ndani ya swala ni jambo) kubwa kabisa (la kumzuilia mtu na mabaya). Na Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyatenda.” (29:45).



Kutokana na aya hii tunajifunza kuwa lengo la kusimamisha swala ni kumtakasa mja na mambo machafu na maovu. Kwa maana nyingine, tunajifunza kuwa swala ikisimamishwa vilivyo, humfanya msimamishaji awe mtu mwema mwenye kutakasika na mambo machafu na maovu na mwenye kuendea kila kipengele chake cha maisha kwa kumtii Allah (s.w). Labda tujiulize swali: “Ni nguvu gani au ni msukumo gani uliomo katika swala unaomfanya mwenye kuswali atakasike na maovu na awe na tabia njema anayoridhia Allah (s.w)” Linaloleta mabadiliko haya makubwa katika tabia na utendaji wa Muumini, ni lile kumbuko la Allah (s.w) lililomo ndani ya swala. Kwa hiyo lengo hili la swala litapatikana tu pale mwenye kuswali atakapokuwa na mazingatio na kumkumbuka Allah (s.w) katika kila hatua ya swala.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 967

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango

Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.

Soma Zaidi...
Sura zinazosomwa katika Swala ya Dhuha

Swala ya Dhuha ni swala ya sunna inayosaliwa wakati wa asubuhi baada ya jua kuchomoza na kupanda angalau kiasi cha mkuki (takribani dakika 15 baada ya jua kuchomoza) mpaka kabla ya adhuhuri. Ingawa hakuna sura maalum zilizowekwa kisheria, Mtume ﷺ alisoma baadhi ya sura zenye maana ya kuhimiza kheri na shukrani.

Soma Zaidi...
taratibu na namna ya kutaliki, na mambo ya kuzingatia

Taratibu za Kutaliki KiislamuKama palivyo na taratibu za kuoa Kiislamu ndivyo hivyo pia ilivyo katika kuvunja ndoa.

Soma Zaidi...
kuletewa ujumbe

(c)Kuletewa Ujumbe na Malaika kutoka kwa Allah (s.

Soma Zaidi...
Mambo yanayotenguwa udhu

Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.

Soma Zaidi...
Wanaowajibika kuhijji

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?

Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu?

Soma Zaidi...
Nguzo za swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...