umuhimu wa swala katika uislamu

umuhimu wa swala katika uislamu

Umuhimu wa Kusimamisha Swala



Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.a) tuliyoirejea mwanzoni, kusimamisha swala ni nguzo ya pili ya nguzo za Uislamu. Katika kuonyesha umuhimu wa kusimamisha nguzo hii Mtume (s.a.w) a me sem a:



“Sw ala ndio nguzo kubw a ya Dini (Uislamu) mwenye kusimamisha swala amesimamisha dini (Uislamu) na mwenye kuiacha swala amevunja Dini .” (Uislamu)”
Katika Hadithi nyingine, amesimulia Jabir (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema:



“Tofauti yetu sisi (Waislamu) na ukafiri ni kuacha swala”. (Muslim) Pia Mtume (s.a.w) amesema:
“Tofauti iliyopo kati yetu (Waislamu) na wengine (wasiokuw a Waislamu) ni swala ”. (Ahmad, Abu Daud, An-Nasai, Tirmidh)
Kutokana na hadithi hizi, tunajifunza kuwa mtu ambaye hasimamishi swala, hatakama anajiita Muislamu si Muislamu bali ni kafiri kama makafiri wengine. Anakuwa kafiri kwa sababu amekanusha amri ya Allah iliyowazi kama inavyobainika katika aya zifuatazo:


“Waambie waja wangu walioamini, wasimamishe swala. ”(14:31)


“... Basi simamisheni swala, kwa hakika swala kwa waumini ni faradhi iliyow ekewa nyakati makhsusi.” (4:1 03)


“Na waamrishe watu wako kuswali (kusimamisha swala) na uendelee mwenyewe kwa hayo...” (20:132).


Tukumbuke kuwa hawi Muumini yule anayekuwa na hiari katika kutekeleza amri ya Allah na Mtume wake kama tunavyokumbushwa katika aya ifuatayo:


“Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi”. (33:36)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1705

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Lengo la kusimamisha swala kwa mwanadamu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala.

Soma Zaidi...
Wafundisheni kuswali watoto wenu

Mtume amemfundisha kuwa watoto wafundishwe kuswali wakiwa na miaka saba na waadhibiwe wakiacha wakiwa na miaka 10

Soma Zaidi...
Haki za viumbe na mazingira

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Umuhimu na nafasi za hijjah katika uislamu

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maswali juu ya Nguzo za uislamu

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali.

Soma Zaidi...
Vituo vya kunuia hijjah au umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...