Swala za sunnah na faida zake

Swala za sunnah na faida zake

Kusimamisha Swala za Sunnah



Baada ya Swala tano za faradhi, kuna swala nyingine za nyongeza alizozisimamisha Mtume (s.a.w) na akatuagiza nasi tumuigize. Swala hizi za ziada tunaziita Swala za Sunnah (Nawafil).



Lengo la Swala za sunnah ni lile lile la swala za faradhi la kututakasa na mambo maovu na machafu. Ni muhimu kwa kila Muislamu kudumisha hizi swala za Sunnah kwa sababu zifuatazo:



1.Kusimamisha Swala za Sunnah ni katika kumtii na kumuigiza Mtume (s.a.w), jambo ambalo ametuamrisha Allah (s.w) katika Qur-an:
2.Kusimamisha swala za sunnah kutatupelekea kufikia ucha Mungu kwa wepesi.


3.Swala za Sunnah pia zina kazi ya kujaziliza swala za faradhi ambazo kwa sababu ya udhaifu wa kibinaadamu hazikuswaliwa kwa ukamilifu unaostahiki.Kama tunavyojifunza katika Hadithi zifu atazo.



Imesimuliwa na Abu Hurairah (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema: Amali ya kwanza atakayoulizwa mtu siku ya Kiyama (siku ya Hukumu) ni Swala. Swala zake zikiwa zimekamilika atafuzu. Swala zake zikiwa pungufu atafeli na kuhasirika. Kama swala zake za faradhi zitakuwa zimepungua, Allah (s.w) atasema angalia kwa mja wangu kama anaswala za ziada (Sw ala za Sunnah) ili zichukuliwe kujazia sehemu iliyopungua katika sw ala za faradhi. Kisha ndio vitendo vyake vingine vitaangaliw a kwa namna hiyo hiyoโ€. (Tirmidh, Abu Daud, An-Nasai, Ibn Majah na Ahm ad).



Swala za Sunnah ni nyingi. Muislamu anatakiwa, kila atakapohisi kuhitajia msaada wa Allah (s.w) atatawadha na kuswali kwani Allah (s.w) anatuagiza:


โ€œJisaidieni (katika mambo yenu) kwa kusubiri na kuswali, na kwa hakika jambo hilo ni gumu isipokuwa kwa wanyenyekevu. Ambao wana yakini ya kwamba watakutana na Mola wao na watarejea kwakeโ€. (2:45-46)



Hata hivyo katika kitabu hiki tutajihusisha na Swala maalum za Sunnah zifuatazo:




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1902

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 web hosting    ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Soma Zaidi...
haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.

Soma Zaidi...
udhaifu wa hoja za kuunga mkono kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Udhaifu wa Hoja za Kudhibiti Uzazi:Hoja nyingi zinazotolewa kuunga mkono udhibiti wa uzazi zimejengwa juu ya hali na mazingira ya maisha yaliyoletwa na utamaduni na maendeleo ya nchi za Ulaya na Marekani.

Soma Zaidi...
NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...
Matendo ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...