image

Sanda ya mwanaume na namna ya kumkafini

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

-    Sanda ya mwanamume ina vipande (majavi) vitatu.

 

  1. Weka kipande cha kwanza juu ya mkeka kisha cha pili na cha tatu na vyote kushikizwa kwa uzi katikati, na kila kipande kipakwe marashi na ubani. 

 

  1. Pasua kamba katika pembe mbili za jamvi la kwanza, moja kwa ajili ya kufungia kichwani na nyingine kwa ajili ya kufungia miguuni.

Kamba moja itachanwa kutoka jamvi la pili, ili kumfunika (kufungia) maiti katikati. Na kamba tatu zitachanwa jamvi la tatu na la pili kwa ajili ya kufungia juu ya mkeka.

 

  1. Maiti italazwa juu ya majavi yote matatu. Ichukuliwe pamba iwekwe manukato kisha iwekwe juu ya viungo vyote vya sijda; paji la uso, viganja vya mikono, magotini na vidole vya miguu. Pamba itumike pia kuziba tundu zote mwilini; mdomo, masikio, pua na makalio.

 

  1. Maiti itatizwe (ifunikwe) mwili wote, kwa kuanza kipande cha kwanza, kisha cha pili na cha tatu ukitanguliza kunjo la kushoto kisha la kulia linafuata. Zile kamba zilizochanwa zitatumika kufungia vitanzi maiti kichwani, tumboni na miguuni. Baada ya hapo maiti inaweza kuwekwa kwenye jeneza baada ya kuzungushiwa kwa mkeka tayari kwa kuswaliwa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1711


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

NGUZO ZA UISLAMU: SWALA NA SHAHADA NA FAIDA ZAKE
NGUZO ZA UISLAMU. Soma Zaidi...

Maana ya Hija na Umuhimu wa kuhiji
Soma Zaidi...

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya
Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Hili ndio lengo la kufunga.
Ni kwa nini Allah ametutaka tugunge. Je kuna lengo gani hasa katika kufunga. Soma Zaidi...

Sanda ya mwanamke na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

nini maana ya hadathi na ni zipi aina za hadathi na uchafu katika uislamu
Soma Zaidi...

Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo. Soma Zaidi...

Nini maana ya twahara katika uislamu, na ni zipi njia za kujitwharisha
1. Soma Zaidi...

Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nguzo za uislamu:Shahada
Nguzo za uislamu: Shahada (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kuswali swala ya maiti: nguzo zake, sunnah zake na maandalizi juu ya maiti
3. Soma Zaidi...

Zijuwe nguzo tano za uislamu na maana zake katika sheria ya uislamu
Hili ni somo letu la kwanza kwenye mtiririko huu wa darsa za fiqh. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya uislamu na nguzo zake. Soma Zaidi...