Kuwa na mwenye haya, na faida zake

Kuwa na mwenye haya, na faida zake

24.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kuwa na mwenye haya, na faida zake

24. Kuwa na Haya



Kuwa na haya ni miongoni mwa tabia njema. Mtu mwenye haya ni yule anayejichunga na maovu na mambo ya aibu. Kuhusu umuhimu wa kuwa na haya, tunajifunza katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Haya ni sehemu ya imani na imani mahali pake ni Peponi; na uchafu (uovu) ni sehemu ya ugumu wa moyo na ugumu wa moyo mahali pake ni Motoni. (Ahmad, Tirmidh).



Ibn Mas ’ud amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Miongoni mwa ujumbe watu waliopokea kutokana na mafundisho ya mwanzo ya Utume ni: Wakati unapokuwa huna haya, fanya ulitakalo. (Bukhari).



Hapa ina maana kuwa mtu asiye na haya hachagui la kufanya au la kusema. Pia Mtume (s.a.w) amesema katika Hadithi iliyosimuliwa na Imran bin Husain kuwa:
Haya haileti kitu kingine ila uzuri na katika maelelezo mengine; Haya ni nzuri katika kila hali. (Bukhari na Muslim).
Mtume (s.a.w) ambaye ndiye kiigizo chetu alikuwa ni mwenye haya sana kama Hadithi ifuatayo inavyobainisha:


Abu Said al-Khudri (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa na haya zaidi kuliko wasichana vigori ndani ya mitandio yao. Alipoona kitu kisichopendeza kwake tulikuwa tunakigundua kutokana na uso wake. (Bukhari na Muslim).



Muislamu anatakiwa awe na haya katika maongezi, katika kuangalia na katika kujisitiri uchi na katika kufanya kila jambo. Haya ni ngao ya kumuepusha mja na mambo maovu na machafu. Wa kwanza anayestahiki kuonewa haya ni Allah (s.w) kwani mwanaadamu hana kificho chochote cha kumsitiri asionekane kwake. Hivyo mja anayemuamini Allah (s.w) atamuonea haya na kujiepusha na maovu na machafu katika maisha yake yote popote atakapokuwa.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 1175

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kitabu Cha  Darsa za dua
Kitabu Cha Darsa za dua

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Majina ya vijana wa pangoni
Majina ya vijana wa pangoni

Makala hii inakwenda kukutajia majina ya vijana saba wa pangoni

Soma Zaidi...
Fadhila za kujenga msikiti
Fadhila za kujenga msikiti

Kuna malipo makubwa kwa ambaye amejenga msikiti kwa ajili ya kuoatavradhi za Allah.

Soma Zaidi...
Aina za hadithi
Aina za hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...