Faida za kuwa na Huruma Kwenye Uislamu

Faida za kuwa na Huruma Kwenye Uislamu

23.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Faida za kuwa na Huruma Kwenye Uislamu

23. Kuwa mwenye Huruma



Muumini hana budi kujipamba na tabia ya kuwahurumia viumbe wenzake. Amuoonee huruma kila mwenye shida na ajitahidi kumsaidia iwezekanavyo. Katika kuonesha umuhimu wa kipengele hiki cha tabia njema Mtume (s.a.w) amesema:



“Ambaye hahurumii watu, pia Allah (s.w) hatamuhurumia ”. (Bukhari).
Huruma hudhihiri katika kuwasaidia wenye shida na matatizo kwa mali na kauli njema kama tunavyojifunza katika Qur-an:



“Hamtaweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vitu mnavyovipenda, na chochote mnachokitoa, basi hakika Allah anakijua ”. (3:92).


“Sio wema (tu) kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa Mashariki na Magharibi. Bali wema (hasa) ni (wale) wanaomwamini Allah na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, w anawapa mali, juu ya kuwa wanayapenda, jamaa na mayatima na maskini na wasafiri (w alioharibikiwa) na waombao na katika kuwakomboa watumwa...” (2:177


“… Na wafanyie wema wazazi na jamaa na yatima na maskini na semeni na watu kwa wema…” (2:83).
Pamoja na kuonyesha huruma kwa wanaadam wenzetu, Uislamu pia umetutaka tuwe na huruma kwa wanyama. Tunafahishwa katika hadith kuwa mtu mmoja alimuambia Mtume:



Ee Mtume w a Allah! Ninapochinja mbuzi ninajaribu kumuonea huruma. Mtume (saw) akasema: “Kama utamuonea huruma , Huruma ya Allah itakuwa juu yako”. (Hakim)
Pia katika hadith nyingine Mtume (saw) amesema:



“Mwanamke mkosefu alimuona mbwa akiwa anachungulia kisima, siku ya joto kali na ulimi wake ukiwa umening’inia kuonyesha kiu kali aliyokuwa nayo. Alimuonea huruma na akamtekea maji na chombo chake. Kutokana na kitendo chake hiki (cha kumuhurumia mbwa), alipata uokovu”. (Muslim)
Pia Hadith ifuatayo inatuonyesha kuwa waislam wanatakiwa


wanyooshe mkono wa huruma kwa viumbe vyote vilivyo hai. Mtume (saw) amesema:
“Wahurumie waliomo ardhini, na yule aliyopo mbinguni atawamiminia huruma yake”



Kinyume chake kuwa katili kwa wanyama ni kitendo cha dhambi kinachoweza kumuingiza mtu motoni. Mtume (saw) amesema:
Mwanamke alitiwa motoni kwa sababu alimfunga paka bila ya kumlisha au kumwachia huru, ambapo angaliweza kwenda huku na huku na kujilisha kutokana na wadudu , n.k. (Bukhari)
Kutokana na Hadith hizi tujue kuwa Allah (sw) hata turehemu iwapo tutakuwa wakatili kwa wanaadamu wenzetu na viumbe wengine.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 1033

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii
Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kushika mwenendo wa kati "Na ushike mwenendo wa kati…." (31:19)
Kushika mwenendo wa kati "Na ushike mwenendo wa kati…." (31:19)

Mwenendo wa kati ni mwenendo ulioepukana na kibri na majivuno kwa upande mmoja na ulioepukkana na udhalili na unyonge kwa upande mwingine.

Soma Zaidi...
Neno la awali
Neno la awali

Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo.

Soma Zaidi...
Zoezi la 5
Zoezi la 5

Maswali mbalimbali kuhusu fiqih

Soma Zaidi...
(xiii)Huwa muaminifu
(xiii)Huwa muaminifu

Waumini wa kweli waliofuzu huchunga amana.

Soma Zaidi...