Navigation Menu



UANDISHI WA HADITHI WAKATI WA MASWAHABA

Wakati wa Masahaba wa Mtume (s.

UANDISHI WA HADITHI WAKATI WA MASWAHABA

Wakati wa Masahaba wa Mtume (s.a.w)11-100. A.H
Kipindi hiki ambacho kimechukua kama karne moja hivi kuanzia pale alipotawafu Mtume (s.a.w) mpaka kutawafu kwa sahaba wa mwisho. Sahaba wa mwisho, Anas bin Malik alifariki 91 A.H. Hiki ni kipindi cha Makhalifa wanne waongofu na Masahaba mashuhuri wa Mtume (s.a.w).. Ni katika kipindi hiki ambapo Dola ya Kiislamu ilitanuka sana. Matatizo mengi ya wakati huu yalitatuliwa kwa kutegemea hukumu za Hadith zilizohifadhiwa vifuani mwa Masahaba. Kwa mfano, baada ya kutawafu Mtume (s.a.w),zilijitokeza kesi ambazo zilionesha umuhimu wa kuhifadhiwa Hadith kama vile: "Mtume azikwe wapi - Makka au Jerusalem?" Ikatolewa Hadith ya Mtume isemayo: "Mtume azikwe afiapo." Hadith ikamaliza tatizo.

Katika kipindi cha Makhalifa wanne waongofu kazi ya uandishi ilikuwepo, lakini haikuwa katika kiwango kikubwa. Kazi kubwa ya kwanza ya uandishi wa Hadith iliyoonekana katika kipimdi hiki ni ile ya kitabu cha Hadith - "Alqatadaya cha 'Ali (r.a) aliyefariki 40 A.H. Pia palikuwa na Juzuu (Pamphlet) ya Hadith ya Ibn 'Abbas (r.a) aliyoiandika muda mrefu baada tu ya kutawafu Mtume (s.a.w). Ibn 'Abbas (r.a) alifariki 61 A.H. Hazrat 'Ali na Ibn 'Abbas japo walikuwa wanazuoni wakubwa, kazi yao hii ndogo, haikuwa inatosheleza mahitaji ya wakati huo.

Katika kipindi hiki haja kubwa ya kuhifadhi Hadith katika maandishi ilijitokeza baada ya kutokea matatizo ya kisiasa, palipotokea makundi mawili: Kundi la 'Ali na kundi la Mu'awiayh. Hadith zilianza kutumiwa vibaya kwa maslahi ya kikundi. Kila kikundi kilikubaliana tu na Hadith zile zinazotetea upande wake. Vile vile kulizuka Hadith nyingi za uongo. 

Ikumbukwe pia katika wakati huu wa Historia, dola ya Kiislamu ilikuwa imepanuka sana na kwa hiyo ulikuwepo uwezekano mkubwa wa kuzusha Hadith za uongo. Hii ndio sababu iliyomsukuma kiongozi aliyekuja baadaye kabisa 'Umar bin 'Abdul-Azizi (101 A.H.) achukuwe dhima ya kuchuja na kuandika Hadith zilizo sahihi. Chini ya uongozi wake vitabu kadhaa viliandikwa na ziliwekwa sheria za kutambua asili ya Hadith na maisha ya wapokezi hasa kuhusu mwenendo na msimamo wao. Watu wawili walifanya kazi hii, Ibn Shihab Al-Zuberi na Abu Bakr al-Hazm.


                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 325


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo
Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo. Soma Zaidi...

namna ya kuswali swala ya dhuha
7. Soma Zaidi...

swala ya idi na nmna ya kuiswali swala ya idi
6. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA KUSOMA QURAN, HUKUMU ZA TAJWID, HUKUMU ZA NUN SAKINA, MIM SAKINA, QLQALA NA IQLAB, TANWIN NA MADA
Soma Zaidi...

fadhila za kusoma quran
Fadhila na umuhimu wa kusoma quran 1. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUOMBA DUA, SUNNAH ZA DUA NA FADHILA ZA DUA
Soma Zaidi...

Makundi ya dini zilizotajwa kwenye quran na athari zake katika jamii
2. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Mbegu za maboga
Soma Zaidi...

NDANI YA SHIMO LA KABURI
Download kitabu Hiki Bofya hapa NDANI YA PANGO LA MAKABURI Mmoja wapo akatowa kamba na kulifunga jeneza vizuri na kuanza kulishusha chini ya mapango kwa kamba ile. Soma Zaidi...

Kuamini qadar na qudra katika uislamu
Kuamini Qadar ya Allah (s. Soma Zaidi...