image

kuwa mwenye huruma na faida zake

25.

kuwa mwenye huruma na faida zake

25. Kuwa na Upendo



Upendo ni matunda ya vipengele vingi vya tabia njema vikiunganishwa pamoja. Kwa mfano kuongea na watu vizuri, kuwahurumia wakati wanamatatizo au kuwafanyia wema wa aina yoyote kama kuwasaidia kazi, kuwakirimu kitu n.k. ni miongoni mwa maadili mema yanayoleta upendo na mahusiano mema kati ya wanaadamu. Kinyume chake, kauli mbaya, ukatili, usengenyi, fitina, uchochezi, husuda, na matendo mengine mabaya kama haya yakitendwa kwa wan adam hujenga chuki na uadui.



Uislamu unatutaka tudumishe upendo kati yetu kwa kuwafanyia wenzetu mema tunayoyapenda na ambayo tungeliwataka wengine watufanyie. Pamoja na kusisitizwa na Uislamu kuwafanyia wengine mema na kujiepusha na kuwaudhi, tunashauriwa pia tuwe na tabia ya kupeana zawadi ili kukaza imara zaidi kifungo cha uhusianao mwema na upendo. Muislamu anashuriwa ajitahidi kutoa zawadi kuwapa wengine kila anapopata fursa ya kufanya hivyo na pia anashauriwa kupokea zawadi kwa moyo mkunjufu kila anapo pewa hata kama yeye ni tajiri na huyo anayempa ni maskini. Hebu turejee Hadith zifuatazo tuone jinsi Mtume (saw) anavyotuelekeza katika kupeana na kupokea zawadi:



Aysha(ra) amesimulai kuwa Mtume w a Allah amesema: Peaneni zawadi, kwani zawadi inaondoa chuki. (Tirmidh)
Aysha (ra) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa akipokea zawadi akirudisha kitu kin gine badala yake kama badilisho kumpa yule aliyetoa. (Bukh ari).


Jab ir ames imulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Yeyote yule aliyepewa zawadi na akawa na uwezo, na airudishie kwa zawadi nyingine , na yule ambaye hana kitu cha ku rejesha , na atoe shukurani na yule asiyetoa ahsante, ni mkosefu wa shukurani, na yule anayejifanya amepewa kitu na huku hakupewa, anakuwa kama yule aliyevaa magwanda(nguo) maw ili ya uw ongo ( ni mw ongo mkubw a-mnafiki). (Tirmidh, Abu-Daud).



Hadith hizi mbili zinatufahamisha kuwa zawadi isielekee upande mmoja tu bali kila anayepokea zawadi naye ajitahidi, kutoa zawadi ya namna nyingine kwa yule aliyempa kama ana uwezo na kama hana cha kutoa atoe ahsante na kumuombea dua aliye mzawadia.
Si tabia ya kiislamu kukataa zawadi- ya aina yoyote iliyohalali. Tunajifunza hili kutokana na hadith zifuatazo:



Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Ningalikaribishwa unyayo wa mguu wa mbuzi (uliopikwa) hakika ningalikaribia na ningalipewa zawadi ya mguu wa mbuzi, hakika ningali pokea. (Bukhari).
Anas amesimulia kuwa Mtume wa Allah alikuwa harudishi manukato yoyote (aliyopewa kama zawadi). (Bukhari)



Ibn Sayid amesimulia: โ€œOmar aliniteua kukusanya Zakat. Nilipo maliza na kuwasilisha zakat yote kwake, aliamuru nipwe ujira wangu. Nilisema: Nilifanya kwa ajili ya Allah na ujira wangu uko kwa Allah. Alisema: chukua kile ulichopewa kwa sababu niliteuliwa kufanya kazi kama hiyo wakati wa Mtume wa Allah. Aliniteua nikasema namna unavyosema. Mtume wa Allah akaniambia: unapopewa kitu ambacho hukukiomba, basi kula na toa sadaqa. (Abu Daud).



Hadith zote hizi zinatufundisha kuwa Muislamu akipewa kitu chochote cha halali asikatae hata kikiwa kidogo namna gani. Na kama hakihitajii sana, basi akipokee kisha atoe sadaqa. Pia tunapata fundisho kuwa Muislamu akikaribishwa na mwenziwe kula kitu chochote kilicho halali asikatae. Alimradi madhumuni ya kutoa na kupokea zawadi siku zote yawe ni kuzidisha upendo, udugu na mahusiano mema kati ya Waislamu na wanaadamu wote kwa ujumla.
Pia kutoleana salamu ni miongoni mwa nyenzo za kujenga upendo baina ya watu kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:


Abu Hurairah (ra) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema; โ€œHam taingia Pep oni mpaka mw amini na hamtaamini mpaka mpendane. Je, nisikufahamisheni juu ya jambo ambalo mkilifanya mtapendana? Toleaneni salamu baina yenuโ€ (Muslim)




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 425


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰2 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe
Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi. Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nini maana ya Kibri, madhara yake na kujiepusha na kibri
17. Soma Zaidi...

VITABU VYA DINI
Soma Zaidi...

Assalam Baada yakufariki wazazi wake mtume alilelewa nanani???
Mtume Muhammad s.a.w amezaliwa yatima asiyena baba. Lakini hii haikumfanya asipate maelezo bora yaliyo mazuri. Je unajuwa aliyemlea baada ya kufariki kwa mama yake?. Soma Zaidi...

Tanzu (makundi) za hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

MAADILI MEMA KATIKA UISLAMU
Yajuwe maadili mema yaliyotajwa katika quran Soma Zaidi...

Kitabu Cha Quran na sayansi
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

(xiii)Huwa muaminifu
Waumini wa kweli waliofuzu huchunga amana. Soma Zaidi...

Elimu
Uwanja wa elimu na maarifa Soma Zaidi...

Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili
ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ุฑูŽู‘ุญู’ู…ูŽู†ู ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุจู’ู†ู ู…ูŽุณู’ุนููˆุฏู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ู‚ูŽุงู„ูŽ: ุญูŽุฏูŽู‘ุซูŽู†ูŽุง ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ... Soma Zaidi...