image

Faida za kuwa na Huruma Kwenye Uislamu

23.

Faida za kuwa na Huruma Kwenye Uislamu

23. Kuwa mwenye Huruma



Muumini hana budi kujipamba na tabia ya kuwahurumia viumbe wenzake. Amuoonee huruma kila mwenye shida na ajitahidi kumsaidia iwezekanavyo. Katika kuonesha umuhimu wa kipengele hiki cha tabia njema Mtume (s.a.w) amesema:



“Ambaye hahurumii watu, pia Allah (s.w) hatamuhurumia ”. (Bukhari).
Huruma hudhihiri katika kuwasaidia wenye shida na matatizo kwa mali na kauli njema kama tunavyojifunza katika Qur-an:



“Hamtaweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vitu mnavyovipenda, na chochote mnachokitoa, basi hakika Allah anakijua ”. (3:92).


“Sio wema (tu) kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa Mashariki na Magharibi. Bali wema (hasa) ni (wale) wanaomwamini Allah na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, w anawapa mali, juu ya kuwa wanayapenda, jamaa na mayatima na maskini na wasafiri (w alioharibikiwa) na waombao na katika kuwakomboa watumwa...” (2:177


“… Na wafanyie wema wazazi na jamaa na yatima na maskini na semeni na watu kwa wema…” (2:83).
Pamoja na kuonyesha huruma kwa wanaadam wenzetu, Uislamu pia umetutaka tuwe na huruma kwa wanyama. Tunafahishwa katika hadith kuwa mtu mmoja alimuambia Mtume:



Ee Mtume w a Allah! Ninapochinja mbuzi ninajaribu kumuonea huruma. Mtume (saw) akasema: “Kama utamuonea huruma , Huruma ya Allah itakuwa juu yako”. (Hakim)
Pia katika hadith nyingine Mtume (saw) amesema:



“Mwanamke mkosefu alimuona mbwa akiwa anachungulia kisima, siku ya joto kali na ulimi wake ukiwa umening’inia kuonyesha kiu kali aliyokuwa nayo. Alimuonea huruma na akamtekea maji na chombo chake. Kutokana na kitendo chake hiki (cha kumuhurumia mbwa), alipata uokovu”. (Muslim)
Pia Hadith ifuatayo inatuonyesha kuwa waislam wanatakiwa


wanyooshe mkono wa huruma kwa viumbe vyote vilivyo hai. Mtume (saw) amesema:
“Wahurumie waliomo ardhini, na yule aliyopo mbinguni atawamiminia huruma yake”



Kinyume chake kuwa katili kwa wanyama ni kitendo cha dhambi kinachoweza kumuingiza mtu motoni. Mtume (saw) amesema:
Mwanamke alitiwa motoni kwa sababu alimfunga paka bila ya kumlisha au kumwachia huru, ambapo angaliweza kwenda huku na huku na kujilisha kutokana na wadudu , n.k. (Bukhari)
Kutokana na Hadith hizi tujue kuwa Allah (sw) hata turehemu iwapo tutakuwa wakatili kwa wanaadamu wenzetu na viumbe wengine.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 462


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

ndoto za kweli
Soma Zaidi...

tawhid
Soma Zaidi...

jamii somo la 35
Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s. Soma Zaidi...

Husimamisha swala
Husimamisha swala katika maisha yao yote. Soma Zaidi...

Faida za kuwa na Huruma Kwenye Uislamu
23. Soma Zaidi...

Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili
عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ... Soma Zaidi...

Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe
Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi. Soma Zaidi...

quran na sayansi
QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh. Soma Zaidi...

Nini maana ya Kibri, madhara yake na kujiepusha na kibri
18. Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

Madhara ya matusi katika jamii, na Kujiepusha na Matusi
15. Soma Zaidi...

DARSA ZA DINI YA KIISLAMU KAMA QURAN, FIQH, SIRA, AFYA, TAJWID NA TAFSIR ZA QURAN
Soma Zaidi...