picha

Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili

عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ...

Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili

HADITHI YA 04

عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم -وَهُوَ الصَّادِقُ الْمَصْدُوقُ-: "إنَّ أَحَدَكُمْ يُجْمَعُ خَلْقُهُ فِي بَطْنِ أُمِّهِ أَرْبَعِينَ يَوْمًا نُطْفَةً، ثُمَّ يَكُونُ عَلَقَةً مِثْلَ ذَلِكَ، ثُمَّ يَكُونُ مُضْغَةً مِثْلَ ذَلِكَ، ثُمَّ يُرْسَلُ إلَيْهِ الْمَلَكُ فَيَنْفُخُ فِيهِ الرُّوحَ، وَيُؤْمَرُ بِأَرْبَعِ كَلِمَاتٍ: بِكَتْبِ رِزْقِهِ، وَأَجَلِهِ، وَعَمَلِهِ، وَشَقِيٍّ أَمْ سَعِيدٍ؛ فَوَاَللَّهِ الَّذِي لَا إلَهَ غَيْرُهُ إنَّ أَحَدَكُمْ لَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ الْجَنَّةِ حَتَّى مَا يَكُونُ بَيْنَهُ وَبَيْنَهَا إلَّا ذِرَاعٌ فَيَسْبِقُ عَلَيْهِ الْكِتَابُ فَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ النَّارِ فَيَدْخُلُهَا. وَإِنَّ أَحَدَكُمْ لَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ النَّارِ حَتَّى مَا يَكُونُ بَيْنَهُ وَبَيْنَهَا إلَّا ذِرَاعٌ فَيَسْبِقُ عَلَيْهِ الْكِتَابُ فَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ الْجَنَّةِ فَيَدْخُلُهَا".
[رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ]

Kwa mapokezi ya Abdullah ibn Masood (ra), ambaye alisema:Mjumbe wa Allaah ((s.a.w)), na yeye ni mkweli, aliyeaminiwa, ametusimulia sisi kuwa, "Hakika uumbaji wa kila mmoja wenu unakusanywa katika tumbo la mama yake kwa siku arobaini katika umbo la nutfah (tone la manii).

kisha anakuwa alaqah (tone la damu) kwa kipindi kama hicho, kisha anakuwa mudgha (pande la nyama) kwa kipindi kama hicho, kisha hutumwa kwake malaika atakayempulizia roho yake ndani yake na ameamrishwa mambo manne : kuandika rizq yake (riziki), maisha ya muda wake, vitendo vyake, na ikiwa vya heri au vya shari (yaani, ikiwa ataingia Peponi).

Na ninaapa kwa yule, ambaye hakuna Muungu isipokuwa Yeye, kwa hakika mmoja wenu anatenda vitendo vya watu wa Peponi hadi kutakapokuwa na urefu wa dhiraa kati yake na hiyo pepo, na yale yaliyoandikwa yatamtangulia, na kwa hivyo atafanya. vitendo vya watu wa Motoni na kwa hivyo atauiingia; na kwa hakika mmoja wenu atatenda vitendo vya watu wa Motoni, mpaka itakuwa kati yake na pepo ni urefu wa dhiraa, na yale ambayo yameandikwa yatamtangulia na atafanya vitendo vya watu wa Peponi na atainaingia peponi"[Bukhari & Muslim]،


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 2081

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 web hosting     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 ai web app     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.

Soma Zaidi...
Mawaidha Kutokwa kwa Shekhe

Karibu kwenye Darsa za mawaidha na Mafundisho ya dini.

Soma Zaidi...
Je wajuwa kuwa jua hujizungurusha kwenye mhimili wake?

Tulipokuwa shule tulisoma kuwa jua halizunguruki, ila dunia ndio huzunguka jua.

Soma Zaidi...