image

Sheria Katika Uislamu

4.

Sheria Katika Uislamu

4.2 Sheria Katika Uislamu

? Maana ya Sheria

Kilugha: njia ya Kufuata

Kimatumizi: ni taratibu, sharti, kanuni na amri zilizowekwa kuongoza jamii.



Kazi ya Sheria katika Jamii

i. Kulinda binaadamu binafsi dhidi ya madhara mbali mbali ya mwenendo wake mbaya.
ii. Kulinda na kuhifadhi maisha ya watu na mali au rasilimali zao kutokana na kuuliwa, kujeruhiwa, kuharibiwa, kuibiwa, n.k bila sababu ya msingi.
iii. Kuhifadhi na kulinda amani na usalama katika jamii kutokana na migongano, vurugu, n.k.
iv. Kuhifadhi na kulinda maadili ya jamii kama njia ya msingi ya kumbakisha mwanaadamu katika mwenendo mema.
v. Kuweka na kupanga utaratibu wa namna ya kuendesha shughuli na maisha ya kila siku kibinafsi na kijamii.
vi. Sheria ya Kiislamu ina kazi ya kulinda na kuhifadhi misingi mitano ya mwanaadamu ambao ni; imani, uhai, akili, heshima na hadhi na mali.




Chimbuko la Sheria za Kitwaghuti

- Zimetungwa na binaadamu kwa kutumia vipawa vya akili, elimu, mila, desturi, uzoefu, mazingira na matashi ya nafsi zao.

- Katiba ndio msingi (chombo) mkuu wa sheria za Kitwaghuti ambayo hugawanya utekelezaji wake katika vyombo vikuu vitatu;
1. Bunge (Legislature) – chombo kikuu cha kutunga sheria

2 Serikali (Executive) – chombo kikuu cha utendaji

3 Mahakama (Judiciary) – chombo kikuu cha kutafsiri sheria na kutoa haki.



Udhaifu wa Sheria za Kitwaghuti

- Pamoja na mwanaadamu kupewa na vipawa vya akili, ujuzi, elimu, n.k bado ana madhaifu mengi kama ifuatayo;
i. Mwanaadamu ana ujuzi wa mambo machache sana juu ya ulimwengu na yale yanayomzunguka.
Rejea Qur’an (17:85)

ii. Mwanaadamu anaathiriwa sana na matashi ya ubinafsi, uchoyo, upendeleo, chuki, n.k.
iii. Binaadamu wametofautiana mno katika fikra, uoni, vipawa, uzoefu

(mazoea).

iv. Mwanaadamu pia anaathiriwa sana na mabadiliko ya kimazingira na zama

(nyakati).



- Kutokana na mapungufu haya, usimamizi na utekelezaji wa sheria za kitwaghuti hufanywa na watu wachache (watawala) kwa ajili ya manufaa yao tu.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1098


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika
Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu. Soma Zaidi...

Maana ya shahada
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya zakat
Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nini maana ya twahara katika uislamu, na ni zipi njia za kujitwharisha
1. Soma Zaidi...

Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Haki na wajibu kwa jirani
Soma Zaidi...

Njia za kudhibiti riba
Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana. Soma Zaidi...

Wanaostahiki kupewa zakat
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Aina 12 za swala za sunnah na idadi ya rakaa zake wakati wa usiku na mchana
Aina za Swala za Sunnah. Soma Zaidi...

Waislamu wanaolazimika kufunga
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Swala ya jamaa.
Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa. Soma Zaidi...

Dua ya kuzuru makaburi, na utaratibu wa kuzuru makaburi
Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi. Soma Zaidi...