Iddil -Fitri
Iddil-Fitri ni siku kuu ya Kiislamu ya kusherehekea kumalizika kwa Mfungo wa Ramadhani. Mwezi wa Ramadhani ambao ndani yake imefaradhishwa funga ambayo imeambatanishwa na matendo mbali mbali ya sunnah, umekusudiwa uwe mwezi wa mafunzo na mazoezi ya kumfanya mja awe mchaji Mungu katika kiwango kinachostahiki kwa kipindi chote cha mwaka mzima.
Iddil-Fitri ndicho kilele cha mafunzo haya ambapo Waislamu wanafurahia na kumshukuru Allah (s.w) kwa kumaliza salama mafunzo haya muhimu na wakati huo huo humuomba Allah (s.w) ayafanye mafunzo hayo yawe yenye kuwafikisha kwenye lengo lililokusudiwa. Hivyo, moja kwa moja inadhihiri kuwa Iddil-Fitri haisherehekewi kwa mavazi mazuri na kwa vyakula na vinywaji vizuri tu, bali kilele cha sherehe hii kinafikiwa kwa kuswali swala ya Iddil-Fitri na kumtukuza na kumuhimidi Allah (s.w) sana kwa Takbira.
Swala ya Iddil-Fitri
Swala ya Idd mbili - Iddil-Fitri na Iddil-Hajj (kilele cha ibada ya Hija) ni sunnah zilizokokotezwa. Swala ya Idd inaswaliwa kwa rakaa mbili na kufuatiwa na Khutuba mbili kama zile zinazosomwa kabla ya swala ya Ijumaa. Swala ya idd ina Takbira 12,takbira 7 hutolewa katika rakaa ya kwanza kabla ya kusoma suratul-Faatiha na takbira 5 huletwa katika rakaa ya pili. vile vile kabla ya kusoma suratul-Faatiha.Mahali pa kuswalia Idd ni bora pawe uwanjani ili Waislamu wakusanyike pamoja kutoka sehemu mbali mbali za mji. Mtume (s.a.w) alikuwa akifanya hivyo. Ni sunnah kula chochote kabla ya kuswali Iddil-Fitri kama tunavyofahamishwa katika Hadith zifu atazo:
Anas (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah hakw enda kusw ali Iddil- Fitri mpaka alipokula Tende katika idadi ya witri. (Bukhari).
Buraydah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alikuwa hatoki kwa swala ya Iddil-Fitri mpaka awe amekula (Kitu) na hakuwa anakula katika s iku ya kuchinja (Iddil-Haj) mpaka asw ali (Dirim i).
Ni sunnah kuleta takbira mara kwa mara kuanzia pale mwezi wa Shawwal unapoandama mpaka baada ya swala ya Iddil-fitri. Takbira
Tafsiri ya Takbira:
Allah Mkubwa, Allah Mkubwa, Allah Mkubwa hapana mola ila Allah Allah Mkubwa, Allah Mkubwa na shukurani zote ni za Allah. Allah Mkubwa aliyetukuka, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi, na namtakasa asubuhi na jioni. Hapana Mola ila Allah. Wala hatumuabudu yeyote ila Yeye peke yake, tunamtakasa yeye na dini yake hata kama w atachukia makafiri.Hapana mola ila Allah peke yake. Ameisadikisha (ameitimiza) ahadi yake na akamnusuru mja (Mtume s.a.w) wake, na akalitukuza jeshi lake, akalipa ushindi kundi lake. Hapana mola ila Allah. Allah Mkubwa. Ewe Allah, teremsha rehma zako juu ya Muhammad, na Maswahaba wake Muhammad, na waliomnusuru Muhammad, na Wakeze Muhammad, na kizazi chake Muhammad, na uwape salama na amani kwa wingi.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2142
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2 Simulizi za Hadithi Audio
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 Kitau cha Fiqh
👉5 kitabu cha Simulizi
👉6 Madrasa kiganjani
Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu
HAKI NA UADILIFU KATIKA UISLAMU. Soma Zaidi...
Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu
Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu. Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi
Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu. Soma Zaidi...
Muundo wa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...
Masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat
Nguzo za uislamu, masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat
(EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu
Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu. Soma Zaidi...
Hijjah
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako. Soma Zaidi...
Mali zinazojuzu kutolewa zaka, nisaab yake na viwango vyake
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Watu wanaowajibikiwa kuhiji
Soma Zaidi...
Mifumo ya benki ya kiislamu.
Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha Soma Zaidi...