Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri.

Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Nini Zaka?

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri. Husemwa imekua konde yake, na husemwa imeongezeka mali yake, na husemwa umezidi uchamngu na kutenda kheri kwake, na husemwa kwa ku'tahirika (takasika): "Hakika amefanikiwa alieitakasa". (Ash-shamsu : 9).

Na hutumika kwa kusifu: "............ Basi msijisifu usafi. ............". (Annajm : 32).

Na Zaka, kisharia ni jina lililowekwa kwa kukusudiwa kiwango makhsusi cha mali chenye kutolewa kwa kadiri makhsusi na kupewa watu wa aina makhsusi kwa shuruti makhsusi. Zaka imepewa jina hili - kwa vile mali inayotolewa Zaka hukua na kubariki kwa du'a za wale wenye kupewa hio Zaka. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

……Lakini mnacho kitoa kwa Zaka kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi hao ndio watao zidishiwa". (Ar-rum : 39).

Hukumu ya Zaka

Kuwajibika Zaka kumekuja kwa Qauli ya Mwenyezi Munguna Hadithi za Mtume s.a.w. na itifaqi ya wanazuoni.

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: . "……na toeni Zaka; ………". (Al Baqara : 110).

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Chukua sadaka katika mali zao, ...........". (Tawba : 103).

Na amesema Mtume s.a.w.: . Maana ya Hadithi hii ni kama hivi:

"Umejengwa Uislam juu ya (Nguzo) tano". Miongoni mwa nguzo tano hizo za Uislam ni Zaka. Basi mwenye kukanya kulazimika kutoa Zaka huwa amekufuru, ila akiwa ni aliesilim karibuni hajapata kuufaham vyema Uislam, au amekulia mbali na elimu ya Kiislam. Mwenye kukataa kutoa Zaka, huchukuliwa (na Dola) Zaka yake kwa nguvu; hivi ndivyo alivyofanya Sayyidna Abu Bakar r.a. kwa wale waliokataa kutoa Zaka na akasema r.a.:

Maana ya maneno haya ya Sayyidna Abu Bakar r.a. ni kama hivi: "Wallahi, lau kama wangalinizuilia (wangalikataa kutowa) pingu za ngamia walikuwa wakizitekeleza (wakizitowa) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungus.a.w.; basi ningaliwapiga vita kwa ajili ya hizo".


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1361

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia na kupunguza zinaa katika jamii

(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.

Soma Zaidi...
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha

Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba

Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutwaharisha Aina mbalimbali za Najisi katika uislamu

Katika somo hili utakwedna kujifunza jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi kwa mujibu wa mafundiso ya Mtume Muhammad (s.a.w)

Soma Zaidi...
Faida za funga

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya twahara na kujitwaharisha?

Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
benki za kiislamu na njia zake za kuingiza kipato

Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya haja

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya haja na jisi ya kuiswali.

Soma Zaidi...