Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri.

Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Nini Zaka?

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri. Husemwa imekua konde yake, na husemwa imeongezeka mali yake, na husemwa umezidi uchamngu na kutenda kheri kwake, na husemwa kwa ku'tahirika (takasika): "Hakika amefanikiwa alieitakasa". (Ash-shamsu : 9).

Na hutumika kwa kusifu: "............ Basi msijisifu usafi. ............". (Annajm : 32).

Na Zaka, kisharia ni jina lililowekwa kwa kukusudiwa kiwango makhsusi cha mali chenye kutolewa kwa kadiri makhsusi na kupewa watu wa aina makhsusi kwa shuruti makhsusi. Zaka imepewa jina hili - kwa vile mali inayotolewa Zaka hukua na kubariki kwa du'a za wale wenye kupewa hio Zaka. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

……Lakini mnacho kitoa kwa Zaka kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi hao ndio watao zidishiwa". (Ar-rum : 39).

Hukumu ya Zaka

Kuwajibika Zaka kumekuja kwa Qauli ya Mwenyezi Munguna Hadithi za Mtume s.a.w. na itifaqi ya wanazuoni.

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: . "……na toeni Zaka; ………". (Al Baqara : 110).

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Chukua sadaka katika mali zao, ...........". (Tawba : 103).

Na amesema Mtume s.a.w.: . Maana ya Hadithi hii ni kama hivi:

"Umejengwa Uislam juu ya (Nguzo) tano". Miongoni mwa nguzo tano hizo za Uislam ni Zaka. Basi mwenye kukanya kulazimika kutoa Zaka huwa amekufuru, ila akiwa ni aliesilim karibuni hajapata kuufaham vyema Uislam, au amekulia mbali na elimu ya Kiislam. Mwenye kukataa kutoa Zaka, huchukuliwa (na Dola) Zaka yake kwa nguvu; hivi ndivyo alivyofanya Sayyidna Abu Bakar r.a. kwa wale waliokataa kutoa Zaka na akasema r.a.:

Maana ya maneno haya ya Sayyidna Abu Bakar r.a. ni kama hivi: "Wallahi, lau kama wangalinizuilia (wangalikataa kutowa) pingu za ngamia walikuwa wakizitekeleza (wakizitowa) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungus.a.w.; basi ningaliwapiga vita kwa ajili ya hizo".


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1750

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir

Soma Zaidi...
Aina za Najisi na twahara katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha aina za najis. Pia utajifunza aina za twahara katika uislamu

Soma Zaidi...
Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.

Soma Zaidi...
Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu

Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu.

Soma Zaidi...
Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.

Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu

Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Maana ya shahada

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...