Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri.
Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri. Husemwa imekua konde yake, na husemwa imeongezeka mali yake, na husemwa umezidi uchamngu na kutenda kheri kwake, na husemwa kwa ku'tahirika (takasika): "Hakika amefanikiwa alieitakasa". (Ash-shamsu : 9).
Na hutumika kwa kusifu: "............ Basi msijisifu usafi. ............". (Annajm : 32).
Na Zaka, kisharia ni jina lililowekwa kwa kukusudiwa kiwango makhsusi cha mali chenye kutolewa kwa kadiri makhsusi na kupewa watu wa aina makhsusi kwa shuruti makhsusi. Zaka imepewa jina hili - kwa vile mali inayotolewa Zaka hukua na kubariki kwa du'a za wale wenye kupewa hio Zaka. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
……Lakini mnacho kitoa kwa Zaka kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi hao ndio watao zidishiwa". (Ar-rum : 39).
Hukumu ya Zaka
Kuwajibika Zaka kumekuja kwa Qauli ya Mwenyezi Munguna Hadithi za Mtume s.a.w. na itifaqi ya wanazuoni.
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: . "……na toeni Zaka; ………". (Al Baqara : 110).
Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Chukua sadaka katika mali zao, ...........". (Tawba : 103).
Na amesema Mtume s.a.w.: . Maana ya Hadithi hii ni kama hivi:
"Umejengwa Uislam juu ya (Nguzo) tano". Miongoni mwa nguzo tano hizo za Uislam ni Zaka. Basi mwenye kukanya kulazimika kutoa Zaka huwa amekufuru, ila akiwa ni aliesilim karibuni hajapata kuufaham vyema Uislam, au amekulia mbali na elimu ya Kiislam. Mwenye kukataa kutoa Zaka, huchukuliwa (na Dola) Zaka yake kwa nguvu; hivi ndivyo alivyofanya Sayyidna Abu Bakar r.a. kwa wale waliokataa kutoa Zaka na akasema r.a.:
Maana ya maneno haya ya Sayyidna Abu Bakar r.a. ni kama hivi: "Wallahi, lau kama wangalinizuilia (wangalikataa kutowa) pingu za ngamia walikuwa wakizitekeleza (wakizitowa) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungus.a.w.; basi ningaliwapiga vita kwa ajili ya hizo".
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za uislamu, kusimamisha swala za Sunnah (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.
Soma Zaidi...Katika Uislamu kuwa na hisa kwenye mali inaruhusiwa. Hapa utajifunza taratibu za kumiliki hisa.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha aina za najis. Pia utajifunza aina za twahara katika uislamu
Soma Zaidi...Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.
Soma Zaidi...