Namna ya kutunza joto la mtoto mara tu baada ya kuzaliwa.


image


Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha ili kuweza kuendelea kukua vizuri na kuepukana na magonjwa.


Njia za kutunza joto la mwili kwa mtoto aliyezaliwa.

1. Kwanza kabisa kwenye hospitali ni lazima chumba cha kujifungulia kiwe na joto la kutosha madirisha yawe yamefungwa pamoja na milango kwa ujumla ili kuweza kutunza joto la kutosha kwa mtoto, pia na feni hazipaswi kuwepo kwenye chumba cha kujifungulia, pia hata kama Mama amejifungulia nyumbani sehemu ile inapaswa kuwa na joto la kutosha kwa Mama na mtoto pia.

 

2. Pindi mtoto anapozaliwa tu anapaswa kupangunswa kwa kutumia kitambaa safi na kisicho na unyevunyevu wowote,kwa kutumia kitambaa hicho kikavu, macho yanapaswa kupangunswa, uso,kichwa, nyumba na mbele , miguu na mikono na pia kitendo cha kupangusa mtoto kinapaswa kutumia mda mfupi ili kuepuka kumletea mtoto baridi na kuleta matatizo kwa mtoto yatokanayo na baridi na baada ya kupangusa mtoto nguo nzuri zenye joto zinapaswa kuwepo.

 

3.Na kitu cha kuzingatia ni kuwa mtoto anapaswa kukaa amefunikwa kichwa kwa kofia bila kuvumiliwa mpaka masaa ishirini na manne,na pia sio vizuri kumwosha mtoto mdogo aliyezaliwa ndani ya masaa ishirini na manne mpaka ruhusa kutoka kwa muuguzi kwa sababu kwa kipindi hiki mtoto anakuwa bado yuko kwenye uangalizi mkubwa , kwa hiyo wazazi na walezi wote wanapaswa kujua kuwa mtoto ni lazima awe na joto la kutosha katika masaa ya mwanzo ya kuzaliwa.

 

4.Ni vizuri sana kama mtoto amezaliwa kwenye hospitali ambayo ina vifaa vyote hasa vya kutunza joto, mtoto akiwa anapanguswa anapaswa kupangunsiwa na katika sehemu ile ya joto ili kuendelea kuwa na joto la kutosha, kwa hiyo ni vema kumfanya mtoto awe na joto la kutosha kwa sababu mtoto akipata baridi kwenye siku za Mwanzo anaweza kupata matatizo mbalimbali kama vile vichomi, Nimonia na Magonjwa mengine yanayoweza kuletwa na baridi.

 

5.Kwa hiyo akina Mama na walezi wa watoto wanapaswa kuwa makini na kuzingatia joto la mtoto akiwa hospitalini au akiwa nyumbani ili tuweze kuepuka kuendelea kuwepo kwa magonjwa ya Nimonia na vichomi kwa watoto.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image tuseme nilifanya ngono jana na leo nipata period,je kuna uwezekano wa kupata mimba
Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi? Soma Zaidi...

image Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren. Soma Zaidi...

image Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa. Soma Zaidi...

image mim ninaujauzito wa mwezi mmoja lakini naona kama hali fulani ya damu inanitoka sehemu ya Siri inafanana na damu ya wakati wa period
Kutokuwa na damu wakati wa ujauzito ni hali uliyo ya kawida lakini inapaswa kujuwa sifa za damu hiyo nabje unatoka kwa namna gani. Kama unasumbuliwa na tatizo hili makala hii ni kwa ajili yako. Soma Zaidi...

image Vyanzo vya kuharibika kwa mimba ya miezi kuanzia 0-3
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki. Soma Zaidi...

image Sababu za uke kuwa na harufu mbaya.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa harufu mbaya kwenye uke ukizingatia usafi huwa unafanyika mara kwa mara ila harufu bado inaendelea kuwa mbaya kwa hiyo tutaona sababu hapo chini. Soma Zaidi...

image Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.
Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla. Soma Zaidi...

image Dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14 Soma Zaidi...

image Mtoto anaanz kucheza kwa mda gan
Kuna watoto wengine huanza kucheza mapema kuliko watoto wengine. Tunapozungumzia kucheza kwa mtoto aliye tumboni yaani mimba hapa inatubidi tuangalie kwa undani zaidi, je ni muda gani mtoto ataanza kucheza? Soma Zaidi...

image Namna ya kutibu ugumba kwa Mwanaume.
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume. Soma Zaidi...