Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha i
1. Kwanza kabisa kwenye hospitali ni lazima chumba cha kujifungulia kiwe na joto la kutosha madirisha yawe yamefungwa pamoja na milango kwa ujumla ili kuweza kutunza joto la kutosha kwa mtoto, pia na feni hazipaswi kuwepo kwenye chumba cha kujifungulia, pia hata kama Mama amejifungulia nyumbani sehemu ile inapaswa kuwa na joto la kutosha kwa Mama na mtoto pia.
2. Pindi mtoto anapozaliwa tu anapaswa kupangunswa kwa kutumia kitambaa safi na kisicho na unyevunyevu wowote,kwa kutumia kitambaa hicho kikavu, macho yanapaswa kupangunswa, uso,kichwa, nyumba na mbele , miguu na mikono na pia kitendo cha kupangusa mtoto kinapaswa kutumia mda mfupi ili kuepuka kumletea mtoto baridi na kuleta matatizo kwa mtoto yatokanayo na baridi na baada ya kupangusa mtoto nguo nzuri zenye joto zinapaswa kuwepo.
3.Na kitu cha kuzingatia ni kuwa mtoto anapaswa kukaa amefunikwa kichwa kwa kofia bila kuvumiliwa mpaka masaa ishirini na manne,na pia sio vizuri kumwosha mtoto mdogo aliyezaliwa ndani ya masaa ishirini na manne mpaka ruhusa kutoka kwa muuguzi kwa sababu kwa kipindi hiki mtoto anakuwa bado yuko kwenye uangalizi mkubwa , kwa hiyo wazazi na walezi wote wanapaswa kujua kuwa mtoto ni lazima awe na joto la kutosha katika masaa ya mwanzo ya kuzaliwa.
4.Ni vizuri sana kama mtoto amezaliwa kwenye hospitali ambayo ina vifaa vyote hasa vya kutunza joto, mtoto akiwa anapanguswa anapaswa kupangunsiwa na katika sehemu ile ya joto ili kuendelea kuwa na joto la kutosha, kwa hiyo ni vema kumfanya mtoto awe na joto la kutosha kwa sababu mtoto akipata baridi kwenye siku za Mwanzo anaweza kupata matatizo mbalimbali kama vile vichomi, Nimonia na Magonjwa mengine yanayoweza kuletwa na baridi.
5.Kwa hiyo akina Mama na walezi wa watoto wanapaswa kuwa makini na kuzingatia joto la mtoto akiwa hospitalini au akiwa nyumbani ili tuweze kuepuka kuendelea kuwepo kwa magonjwa ya Nimonia na vichomi kwa watoto.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa, ni njia zitoleeazo na wakunga Ili kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo usaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya HCG katika kupima mimba, HCG maana yake ni human chorionic gonadotropin ni homoni ambayo uonekanekana kwenye mkojo na damu kama mtu ana mimba.
Soma Zaidi...KubaleheΓΒ ni wakati mwili wa mtoto unapoanza kubadilika na kuwa wa mtu mzima (balehe) hivi karibuni. Kubalehe ambao huanza kabla ya umri wa miaka 8 kwa wasichana na kabla ya umri wa miaka 9 kwa wavulana.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili pamoja na mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua kwa Wanaume
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja, mara nyingi kuna Watu ambao huwa wanalalamika kwa sababu ya kupata hedhi za mara kwa mara kwa mwezi mmoja.
Soma Zaidi...