picha

Namna ya kutunza joto la mtoto mara tu baada ya kuzaliwa.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha i

Njia za kutunza joto la mwili kwa mtoto aliyezaliwa.

1. Kwanza kabisa kwenye hospitali ni lazima chumba cha kujifungulia kiwe na joto la kutosha madirisha yawe yamefungwa pamoja na milango kwa ujumla ili kuweza kutunza joto la kutosha kwa mtoto, pia na feni hazipaswi kuwepo kwenye chumba cha kujifungulia, pia hata kama Mama amejifungulia nyumbani sehemu ile inapaswa kuwa na joto la kutosha kwa Mama na mtoto pia.

 

2. Pindi mtoto anapozaliwa tu anapaswa kupangunswa kwa kutumia kitambaa safi na kisicho na unyevunyevu wowote,kwa kutumia kitambaa hicho kikavu, macho yanapaswa kupangunswa, uso,kichwa, nyumba na mbele , miguu na mikono na pia kitendo cha kupangusa mtoto kinapaswa kutumia mda mfupi ili kuepuka kumletea mtoto baridi na kuleta matatizo kwa mtoto yatokanayo na baridi na baada ya kupangusa mtoto nguo nzuri zenye joto zinapaswa kuwepo.

 

3.Na kitu cha kuzingatia ni kuwa mtoto anapaswa kukaa amefunikwa kichwa kwa kofia bila kuvumiliwa mpaka masaa ishirini na manne,na pia sio vizuri kumwosha mtoto mdogo aliyezaliwa ndani ya masaa ishirini na manne mpaka ruhusa kutoka kwa muuguzi kwa sababu kwa kipindi hiki mtoto anakuwa bado yuko kwenye uangalizi mkubwa , kwa hiyo wazazi na walezi wote wanapaswa kujua kuwa mtoto ni lazima awe na joto la kutosha katika masaa ya mwanzo ya kuzaliwa.

 

4.Ni vizuri sana kama mtoto amezaliwa kwenye hospitali ambayo ina vifaa vyote hasa vya kutunza joto, mtoto akiwa anapanguswa anapaswa kupangunsiwa na katika sehemu ile ya joto ili kuendelea kuwa na joto la kutosha, kwa hiyo ni vema kumfanya mtoto awe na joto la kutosha kwa sababu mtoto akipata baridi kwenye siku za Mwanzo anaweza kupata matatizo mbalimbali kama vile vichomi, Nimonia na Magonjwa mengine yanayoweza kuletwa na baridi.

 

5.Kwa hiyo akina Mama na walezi wa watoto wanapaswa kuwa makini na kuzingatia joto la mtoto akiwa hospitalini au akiwa nyumbani ili tuweze kuepuka kuendelea kuwepo kwa magonjwa ya Nimonia na vichomi kwa watoto.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/04/07/Thursday - 06:37:49 pm Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2192

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰3 web hosting    πŸ‘‰4 ai web app    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu.

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUKOSA NGUVU ZA KIUME AMA KUWA NA UWEZO MDOGO WA KUHIMILI TENDO LA NDOA

Hii ni hali inayowapata wanaume kushindwa kuhimili tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea

Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeΒ  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.

Soma Zaidi...
Huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja.

Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja, aina hiyo ya mimba kwa kitaalamu huitwa complete abortion.

Soma Zaidi...
Huduma kwa mama mwenye mimba Inayotishia kutoka.

Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.

Soma Zaidi...
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Sababu za mwanamke kukosa hamu ya tendo la ndoa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mwanamke kukosa tendo la ndoa, ni sababu ambazo uwakuta wanawake wengi unakuta mama yuko kwenye ndoa ila hana hata hamu ya lile tendo la ndoa hali ambayo umfanya mwanamke kuona kitendo cha tendo la ndoa ni unyanyasaji au

Soma Zaidi...
Mke Wang Ana tatizo la tumbo kuuma chini upande wa kushoto akishika ni pagumu ,anapatwa na kichefuchef tumbo kujaa ges na kujiisi kusiba he mtanisaidije ili kuondoa tatizo Hilo Ila anaujauzito wa wiki mbili

Miongoni mwa changamoto za ujauzito ni maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanawezakuwaya kawaida ama makali zaidi. Vyema kufika Kituo cha Afya endapoyatakuwa makali.

Soma Zaidi...
Njia za kufanya ili kuepukana na tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo mtu anapaswa kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili kisiweze kutokea na pia kama jamii ikishirikiana kwa pamoja tunaweza kuepusha kwa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...