picha

Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.

Huduma muhimu kwa mtoto pindi anapozaliwa.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mtoto aliyekamilika na kufikia wakati wa kuzaliwa ni kuanzia miezi thelathini na saba mpaka arobaini na mbili chini yake mtoto akizaliwa anakuwa hajafikisha umri kwa hiyo mtoto akitoa kichwa tu, muuguzi anasafisha Uso wa mtoto, midomo na pua kwa hiyo hatua hii ufanyika kwa kutumia kitambaa safi au vifaa vilivyoandaliwa kwa ajili ya kazi hiyo ambavyo kwa kitaalamu huitwa gauze, ila kama Mama amejifungulia kwenye sehemu isiyo ya hospitalini anapaswa kufanya hivyo kwa kitambaa kisafi.

 

2. Pia mtoto akitolewa akitoka mzima anapaswa kuwekwa kwenye tumbo la mama yake moja kwa moja ili aweze kupata ujoto wa Mama, pia kwa wakati huo muuguzi au mtoa huduma kwa Mama anapaswa kumpangia mtoto kwa kutumia kitambaa safi, na anapompangusa awe kama anamtekenya tekenya ili kuweza kusaidia upumuaji na pia mapigo ya moyo, kwa hiyo Mtoto akiwa anapanguswa inabidi iwe kwa haraka ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi.

 

3. Kwa wakati huo mtoto anapaswa kufunikwa kwa nguo safi akiwa kwenye tumbo la Mama yake ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi na pia Mama anaweza kumnyonyesha mtoto hapo hapo, pia tunapaswa kujua kuwa mtoto anapaswa kunyonyeshwa ndani ya saa moja kabla ya kuzaliwa na hasizidi mda huo 

 

4.Baada ya kumaliza hayo, muuguzi au msaidizi wa Mama anapaswa kunawa vizuri na kuweka gloves ambazo ni maalum kwa kitaalamu huitwa stelire gloves kwa aji ya kukata kitovu, kwa hiyo kitovu kinapaswa kukatwa kwa uangalifu zaidi ili kuweza kuzuia maambukizi,na pia  hatua zinapaswa kufuatwa ili kukata kitovu kadri inavyopaswa .

 

5.Baada ya kukata kitovu, muuguzi anaweza kuendelea na kazi nyingine za kuhakikisha kubwa Mama yuko vizuri na kumfanyia Mama usafi na kutoa kondo la nyuma na kuhakikisha kuwa hakuna madhara yoyote kati ya Mama na mtoto na baadae Mama anaweza kuwekwa kwenye sehemu ya uangalizi ndani ya masaa ishirini na manne kwa ajili ya uangalizi zaidi na kwa kipindi hicho Mtoto na Mama wanakuwa kwenye uangalizi wa muuguzi

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/04/07/Thursday - 10:22:32 am Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3733

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 ai web app   

Post zinazofanana:

maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimba

Je kupata maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimb hizo syo dalili moja wapi?

Soma Zaidi...
Vyakula vinavyosaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone

Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo usaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone.

Soma Zaidi...
KUWAHI KUMALIZA TENDO LA NDOA MAPEMA: kumwaga mbegu mapema

Hii ni hali inayowapata sana wanaume huwa wanamaliza hamu ya tendo la ndoa mapema kabla ya mwenza kuridhika.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba yenye uvimbe

Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa

Soma Zaidi...
Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.

Soma Zaidi...
Njia za uzazi wa mpango

Posti hii inahusu zaidi kuhusu njia za uzazi wa mpango, uzazi wa mpango ni njia za kupanga uzazi Ili kupata idadi ya watoto unaohitaji

Soma Zaidi...
Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo yanayowapata watoto waliozaliwa kabla ya wakati au mapema (premature)

Kuzaa kabla ya wakati ni kuzaliwa ambayo hufanyika zaidi ya wiki tatu kabla ya kuzaliwa kwa mtoto au kuzaliwa mapema ni moja ambayo hutokea kabla ya mwanzo wa wiki ya 37 ya ujauzito. Kawaida, ujauzito hudumu kama wiki 40.

Soma Zaidi...
faida za tendo ka ndoa wakati wa ujauzito

Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba

Soma Zaidi...