Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.
Huduma muhimu kwa mtoto pindi anapozaliwa.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mtoto aliyekamilika na kufikia wakati wa kuzaliwa ni kuanzia miezi thelathini na saba mpaka arobaini na mbili chini yake mtoto akizaliwa anakuwa hajafikisha umri kwa hiyo mtoto akitoa kichwa tu, muuguzi anasafisha Uso wa mtoto, midomo na pua kwa hiyo hatua hii ufanyika kwa kutumia kitambaa safi au vifaa vilivyoandaliwa kwa ajili ya kazi hiyo ambavyo kwa kitaalamu huitwa gauze, ila kama Mama amejifungulia kwenye sehemu isiyo ya hospitalini anapaswa kufanya hivyo kwa kitambaa kisafi.
2. Pia mtoto akitolewa akitoka mzima anapaswa kuwekwa kwenye tumbo la mama yake moja kwa moja ili aweze kupata ujoto wa Mama, pia kwa wakati huo muuguzi au mtoa huduma kwa Mama anapaswa kumpangia mtoto kwa kutumia kitambaa safi, na anapompangusa awe kama anamtekenya tekenya ili kuweza kusaidia upumuaji na pia mapigo ya moyo, kwa hiyo Mtoto akiwa anapanguswa inabidi iwe kwa haraka ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi.
3. Kwa wakati huo mtoto anapaswa kufunikwa kwa nguo safi akiwa kwenye tumbo la Mama yake ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi na pia Mama anaweza kumnyonyesha mtoto hapo hapo, pia tunapaswa kujua kuwa mtoto anapaswa kunyonyeshwa ndani ya saa moja kabla ya kuzaliwa na hasizidi mda huo
4.Baada ya kumaliza hayo, muuguzi au msaidizi wa Mama anapaswa kunawa vizuri na kuweka gloves ambazo ni maalum kwa kitaalamu huitwa stelire gloves kwa aji ya kukata kitovu, kwa hiyo kitovu kinapaswa kukatwa kwa uangalifu zaidi ili kuweza kuzuia maambukizi,na pia hatua zinapaswa kufuatwa ili kukata kitovu kadri inavyopaswa .
5.Baada ya kukata kitovu, muuguzi anaweza kuendelea na kazi nyingine za kuhakikisha kubwa Mama yuko vizuri na kumfanyia Mama usafi na kutoa kondo la nyuma na kuhakikisha kuwa hakuna madhara yoyote kati ya Mama na mtoto na baadae Mama anaweza kuwekwa kwenye sehemu ya uangalizi ndani ya masaa ishirini na manne kwa ajili ya uangalizi zaidi na kwa kipindi hicho Mtoto na Mama wanakuwa kwenye uangalizi wa muuguzi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?
Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi?
Soma Zaidi...Namna ya kutibu ugumba kwa Mwanaume.
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume.
Soma Zaidi...Je, mwanamke anapataje Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi PID?
Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi.
Soma Zaidi...Dalili za PID
Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia
Soma Zaidi...Sababu za kuharibika kwa ujauzito na dalili zake
Dalili za kuharibika kwa ujauzito na dalili za kuharibika kwa ujauzo
Soma Zaidi...