Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.
Huduma muhimu kwa mtoto pindi anapozaliwa.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mtoto aliyekamilika na kufikia wakati wa kuzaliwa ni kuanzia miezi thelathini na saba mpaka arobaini na mbili chini yake mtoto akizaliwa anakuwa hajafikisha umri kwa hiyo mtoto akitoa kichwa tu, muuguzi anasafisha Uso wa mtoto, midomo na pua kwa hiyo hatua hii ufanyika kwa kutumia kitambaa safi au vifaa vilivyoandaliwa kwa ajili ya kazi hiyo ambavyo kwa kitaalamu huitwa gauze, ila kama Mama amejifungulia kwenye sehemu isiyo ya hospitalini anapaswa kufanya hivyo kwa kitambaa kisafi.
2. Pia mtoto akitolewa akitoka mzima anapaswa kuwekwa kwenye tumbo la mama yake moja kwa moja ili aweze kupata ujoto wa Mama, pia kwa wakati huo muuguzi au mtoa huduma kwa Mama anapaswa kumpangia mtoto kwa kutumia kitambaa safi, na anapompangusa awe kama anamtekenya tekenya ili kuweza kusaidia upumuaji na pia mapigo ya moyo, kwa hiyo Mtoto akiwa anapanguswa inabidi iwe kwa haraka ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi.
3. Kwa wakati huo mtoto anapaswa kufunikwa kwa nguo safi akiwa kwenye tumbo la Mama yake ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi na pia Mama anaweza kumnyonyesha mtoto hapo hapo, pia tunapaswa kujua kuwa mtoto anapaswa kunyonyeshwa ndani ya saa moja kabla ya kuzaliwa na hasizidi mda huo
4.Baada ya kumaliza hayo, muuguzi au msaidizi wa Mama anapaswa kunawa vizuri na kuweka gloves ambazo ni maalum kwa kitaalamu huitwa stelire gloves kwa aji ya kukata kitovu, kwa hiyo kitovu kinapaswa kukatwa kwa uangalifu zaidi ili kuweza kuzuia maambukizi,na pia hatua zinapaswa kufuatwa ili kukata kitovu kadri inavyopaswa .
5.Baada ya kukata kitovu, muuguzi anaweza kuendelea na kazi nyingine za kuhakikisha kubwa Mama yuko vizuri na kumfanyia Mama usafi na kutoa kondo la nyuma na kuhakikisha kuwa hakuna madhara yoyote kati ya Mama na mtoto na baadae Mama anaweza kuwekwa kwenye sehemu ya uangalizi ndani ya masaa ishirini na manne kwa ajili ya uangalizi zaidi na kwa kipindi hicho Mtoto na Mama wanakuwa kwenye uangalizi wa muuguzi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Njia za uzazi wa mpango zinazomhusisha mwanaume
Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango unavyofanya na mwanaume kushiriki, ni njia ambayo umfanye mwanaume awe mhusika hasa wakati wa kujamiiana.
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.
Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.
Soma Zaidi...Dalili za kuziba kwa mirija ya uzazi
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi.
Soma Zaidi...Madhara ya kutoka kwa mimba
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutoka kwa mimba, kwa kawaida tunafahamu kwamba mimba ikitungwa na mwili mzima huwa na wajibu wa kutunza kilichotungwa kwa hiyo ikitokea mimba ikatoka usababisha madhara yafuatayo.
Soma Zaidi...Dalili ninazoziona kwangu chuchu zinauma na sjapata period mwezi huu na nlishiriki tarehe 19 mwezi wa tisa
Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu.
Soma Zaidi...Njia za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha.
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha kwa sababu kuna familia nyingi zinakosa watoto sio kwa sababu ni tasa ila kuna njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...