Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.
Huduma muhimu kwa mtoto pindi anapozaliwa.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mtoto aliyekamilika na kufikia wakati wa kuzaliwa ni kuanzia miezi thelathini na saba mpaka arobaini na mbili chini yake mtoto akizaliwa anakuwa hajafikisha umri kwa hiyo mtoto akitoa kichwa tu, muuguzi anasafisha Uso wa mtoto, midomo na pua kwa hiyo hatua hii ufanyika kwa kutumia kitambaa safi au vifaa vilivyoandaliwa kwa ajili ya kazi hiyo ambavyo kwa kitaalamu huitwa gauze, ila kama Mama amejifungulia kwenye sehemu isiyo ya hospitalini anapaswa kufanya hivyo kwa kitambaa kisafi.
2. Pia mtoto akitolewa akitoka mzima anapaswa kuwekwa kwenye tumbo la mama yake moja kwa moja ili aweze kupata ujoto wa Mama, pia kwa wakati huo muuguzi au mtoa huduma kwa Mama anapaswa kumpangia mtoto kwa kutumia kitambaa safi, na anapompangusa awe kama anamtekenya tekenya ili kuweza kusaidia upumuaji na pia mapigo ya moyo, kwa hiyo Mtoto akiwa anapanguswa inabidi iwe kwa haraka ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi.
3. Kwa wakati huo mtoto anapaswa kufunikwa kwa nguo safi akiwa kwenye tumbo la Mama yake ili kuweza kuepuka kuwepo kwa baridi na pia Mama anaweza kumnyonyesha mtoto hapo hapo, pia tunapaswa kujua kuwa mtoto anapaswa kunyonyeshwa ndani ya saa moja kabla ya kuzaliwa na hasizidi mda huo
4.Baada ya kumaliza hayo, muuguzi au msaidizi wa Mama anapaswa kunawa vizuri na kuweka gloves ambazo ni maalum kwa kitaalamu huitwa stelire gloves kwa aji ya kukata kitovu, kwa hiyo kitovu kinapaswa kukatwa kwa uangalifu zaidi ili kuweza kuzuia maambukizi,na pia hatua zinapaswa kufuatwa ili kukata kitovu kadri inavyopaswa .
5.Baada ya kukata kitovu, muuguzi anaweza kuendelea na kazi nyingine za kuhakikisha kubwa Mama yuko vizuri na kumfanyia Mama usafi na kutoa kondo la nyuma na kuhakikisha kuwa hakuna madhara yoyote kati ya Mama na mtoto na baadae Mama anaweza kuwekwa kwenye sehemu ya uangalizi ndani ya masaa ishirini na manne kwa ajili ya uangalizi zaidi na kwa kipindi hicho Mtoto na Mama wanakuwa kwenye uangalizi wa muuguzi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
anawashwa Sana sehemu ya Siri mpaka anatoka vipele vingi kwenye mapaja korodani zake zimebadilika kuwa nyekundu
Abali mkuu Nina mdogo wangu anawashwa Sana sehemu ya Siri mpaka anatoka vipele vingi kwenye mapaja korodani zake zimebadilika kuwa nyekundu na zenye kutisha uume wake nao umekuwa unakama mabaka umebabuka aisee nime angaika Sana kumtibia mpaka nakata tamaa
Soma Zaidi...Madhara ya kupungua kwa homoni ya projestron
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa homoni ya projestron ikipungua mwilini na pia kuweza kutambua dalili za kupungua kwa homoni hii ya progesterone.
Soma Zaidi...Sababu za mwanamke kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa
Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazosababisha kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Mimba kutoka kabla ya umri wake
Posti hii inahusu zaidi kuhusu kwa mimba kutoka kabla ya mda wake,ni kitendo ambacho mimba utoka kabla ya wiki ishilini na na nane.
Soma Zaidi...Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri
Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.
Soma Zaidi...CHANGAMOTO ZA UJAUZITO, NA DALILI ZAKE NA NAMNA YA KUKABILIANA NAZO
Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.
Soma Zaidi...