Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.
1. Kwanza kabisa wakati tunapokuwa tunapangusa mtoto tunapaswa kuangalia upumuaji wake kwa kuangalia Dalili zote za upumuaji.
2.Vile vile Tunapaswa kusikiliza sauti inayotoka wakati wa kupumua na kuangalia jinsi kifua kinavyocheza cheza kwa kutumia sauti tunaweza kugundua kuwa mtoto yuko hai na anaweza.
3.Vili vile tunapaswa kuangalia kama mtoto anapumua haraka haraka na kwa urahisi au kuangalia kama mtoto analia kwa sababu kulia ni Dalili mojawapo ya kupumua kwa mtoto.
4. Na pia mtoto anapaswa kuonekana anapitisha hewa kwenye pua kwa urahisi sio kwa shida, ukiona anapitisha hewa kwa shida hiyo ni Dalili kwamba kuna Tatizo ambalo halijaenda sawa na pia ni lazima kumshughulikia mtoto.
5. Kwa kawaida mtoto anayepumua vizuri ni yule ambaye analia tu baada ya kuzaliwa, anapumua vizuri na kwa haraka haraka na upumuaji wake ni wa kawaida hakoromi au hakuna kitu chochote kinacholeta shida wakati wa upumuaji.
6. Na mtoto ambaye hapumui vizuri ni yule ambaye anahangaika wakati wa kupumua na anapumua kwa kutumia hewa nzito na pumzi haieleweki au kwa wakati mwingine hakuna kupumua kabisa, hali ya namna hii ikitokea huduma inapaswa kutolewa haraka.
7. Kwa wakati mwingine kuna watoto ambao wanazaliwa na hewa yao inakuwa ya shida na kwa wakati mwingine wanazaliwa wakiwa hawapumui kabisa kwa hiyo tunapaswa kuwasaidia kwa kufungua sahemu muhimu kama vile kwenye mdomo, kwenye pua au kifuani labda kuna baadhi ya vitu ambavyo vimefunga hewa isiweze kupita.
8. Pamoja na upumuaji wa shida kwa watoto kuna baadhi ya watoto wanaozaliwa wakiwa na uzito mkubwa na wanahitaji uangalizi wa karibu ili waweze kupata huduma kwa sababu walicheleweshwa wanaweza kupata matatizo mbalimbali.
9. Kwa hiyo baada ya kugundua kubwa mtoto anapumua vizuri na hana tatizo lolote ni lazima kumpeleka kifuani mwa Mama ili aendelee kuishi hapo kwa ajili ya kupata joto la Mama na kwa wale ambao hawapumui ni vizuri kabisa kuwahi kuwapeleka kwenye vituo vya afya kwa ajili ya uangalizi zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi na uvimbe katika mirija ya uzazi. Mara nyingi hutumiwa sawa na ugonjwa wa uvimbe kwenye fupa nyonga (PID), ingawa PID haina ufafanuzi sahihi na inaweza kurejelea magonjwa kadhaa ya njia ya juu ya uzazi
Soma Zaidi...Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi njia za kutibu kuharisha kwa watoto wakiwa nyumbani, kwa sababu mara nyingine mtoto anaweza kuharisha si kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ila ni uchafu tu kwa hiyo njia muhimu zinazofaa kutibu mtoto ni pamoja na yafuatayo.
Soma Zaidi...posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot
Soma Zaidi...ukiwa na ujauzito unaweza kuona mabadiliko mengi katika mwili wako yakiwemo kutokwa na majimaji. je majimaji haya yana dalili gani kwenye ujauzito?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun
Soma Zaidi...Hii ni hali inayowapata sana wanaume huwa wanamaliza hamu ya tendo la ndoa mapema kabla ya mwenza kuridhika.
Soma Zaidi...Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana
Soma Zaidi...Posti hii inahusu namna unavyoweza kumtambua mtoto mwenye Ugonjwa wa Nimonia na tiba anayopaswa kupata mtoto mwenye Nimonia
Soma Zaidi...