picha

Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua

Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.

Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua.

1. Kwanza kabisa wakati tunapokuwa  tunapangusa mtoto tunapaswa kuangalia upumuaji wake kwa kuangalia Dalili zote za upumuaji.

 

2.Vile vile Tunapaswa kusikiliza sauti inayotoka wakati wa kupumua na kuangalia jinsi kifua kinavyocheza cheza kwa kutumia sauti tunaweza kugundua kuwa mtoto yuko hai na anaweza.

 

3.Vili vile tunapaswa kuangalia kama mtoto anapumua haraka haraka na kwa urahisi au kuangalia kama mtoto analia kwa sababu kulia ni Dalili mojawapo ya kupumua kwa mtoto.

 

4. Na pia mtoto anapaswa kuonekana anapitisha hewa kwenye pua kwa urahisi sio kwa shida, ukiona anapitisha hewa kwa shida hiyo ni Dalili kwamba kuna Tatizo ambalo halijaenda sawa na pia ni lazima kumshughulikia mtoto.

 

5. Kwa kawaida mtoto anayepumua vizuri ni yule ambaye analia tu baada ya kuzaliwa, anapumua vizuri na kwa haraka haraka na upumuaji wake ni wa kawaida hakoromi au hakuna kitu chochote kinacholeta shida wakati wa upumuaji.

 

6. Na mtoto ambaye hapumui vizuri ni yule ambaye  anahangaika wakati wa kupumua na anapumua kwa kutumia hewa nzito na pumzi haieleweki au kwa wakati mwingine hakuna kupumua kabisa, hali ya namna hii ikitokea huduma inapaswa kutolewa haraka.

 

7. Kwa wakati mwingine kuna watoto ambao wanazaliwa na hewa yao inakuwa ya shida na kwa wakati mwingine wanazaliwa wakiwa hawapumui kabisa kwa hiyo tunapaswa kuwasaidia kwa kufungua sahemu muhimu kama vile kwenye mdomo, kwenye pua au kifuani labda kuna baadhi ya vitu ambavyo vimefunga hewa isiweze kupita.

 

8. Pamoja na upumuaji wa shida kwa watoto kuna baadhi ya watoto wanaozaliwa wakiwa na uzito mkubwa na wanahitaji uangalizi wa karibu ili waweze kupata huduma kwa sababu walicheleweshwa wanaweza kupata matatizo mbalimbali.

 

9. Kwa hiyo baada ya kugundua kubwa mtoto anapumua vizuri na hana tatizo lolote ni lazima kumpeleka kifuani mwa Mama ili aendelee kuishi hapo kwa ajili ya kupata joto la Mama na kwa wale ambao hawapumui ni vizuri kabisa kuwahi kuwapeleka kwenye vituo vya afya kwa ajili ya uangalizi zaidi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 1580

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Mwenye ujauzito wa wiki moja na ana u.t.i anaweza kutumia dawa za aina gani ambozo zitakua salama kwa kiumbe kilichoanza kukua?

Ujauzito unaweza kutoka kwa sababu nyingi kama maradhi, madawa, vyakula na ajali. Unawezakutoa mimba bila kujuwa amakwakujuwa. Damu kutoka ni moja ya dalili za kutoka kwa mimba hata hivyo maumivu ya tumbo huweza kuandamana na damu hii.

Soma Zaidi...
Mimba iliyotungia nje, sababu zake na dalili zake. Nini kifanyike kuizuia?

Mimba hatari iliyotungia nje ya mji wa mimba, ni zipi dalili zake na ni kivipo mimba inatungia nje?

Soma Zaidi...
Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.

Soma Zaidi...
Vipimo muhimu wakati wa ujauzito

Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...