Namna ya kufunga kitovu cha mtoto.
Posti hii inahusu zaidi njia au namna ya kufunga kitovu cha mtoto mara tu anapozaliwa, kwa kawaida tunafahamu kwamba ili mtoto aweze kuishi akiwa tumboni anategemea sana kula na kufanya shughuli zake kwa kupitia kwenye plasenta kwa hiyo mtoto akizaliwa tu
Namna ya kufunga kitovu cha mtoto.
1. Tufahamu kuwa kitovu cha mtoto kinakuwa kimeunganika na Mama pindi mtoto anapozaliwa kwa hiyo mtoto anapolia tu pale wakati wa kuzaliwa anaanza kutegemea hewa ya nje na kuacha kutegemea hewa ya kupitisha kwenye plasenta kwa hiyo kitovu hicho kinaweza kutenganishwa na pia mtoto akaanza kutumia maziwa ya Mama kama chakula chake.na kitovu hiki kinahitaji sana umakini wakati wa kutenganishwa ili kuweza kuepuka matatizo ya Maambukizi na kuoza kwenye sehemu ya kitovu.
2. Kwa hiyo hatua ya kwanza tunapaswa kutenganisha mtoto kutoka kwenye plasenta kwa hiyo tunapima sentimita kuanzia nane mpaka kumi na tunabana, hizo sentimita zinaanzia kwenye kitovu cha mtoto tunafanya hivyo ili kuepuka kuchanganya damu ya Mama na mtoto.
3. Wakati wa kufanya hivyo tunazingatia usafi wa hali ya juu na kutumia glovesi nzuri na za kitaaluma zinazoitwa stelire gloves, kwa kufanya hivyo tunaepuka Maambukizi yanayoweza kujitokeza kwa wakati wowote.
4. Pa damu ukiacha kuzunguka tunapima sentimita mbili kutoka kwa mtoto na kufunga vizuri na pia tunapima sentimita tatu kutoka kwenye sentimita mbili na tunafunga, kwa hiyo tunakata kati kati ya sentimita mbili na tatu na tunazingatia usafi kwa kuweka kitambaa ili damu iweze kudondoka humo.
5.Baada ya kumaliza kuweka vizuri kitovu chukua vifaa vyote kwenye sehemu muhimu na inayohitajika na kuosha mikono vizuri kwa maji na sabuni hatimaye unaweza kuendelea na vitu vingine.na pia walezi na wazazi wote wanapaswa kuachana na mila potofu za kuweka vitu visivyofaa kwenye kitovu kwa hiyo niache kitovu kitakauka chenyewe.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Faida za Uzazi wa mpango
Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA.
Soma Zaidi...Madhara ya fangasi ukeni.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi ukeni, madhara mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa fangasi mapema.
Soma Zaidi...Dalili za ujauzito: Nini kinatokea kwanza
Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.
Soma Zaidi...Uzazi wa mpango
Uzazi wa Mpango hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa. Uzazi wa mpango una faida kadhaa kwa mama wa mtoto, wanandoa na jamii Ujuzi wa mzunguko wa hedhi humwezesha mtoa huduma kumshaur
Soma Zaidi...Jinsi ya kuacha kupiga punyeto.
Post hii inakwenda kukupa njia za kukusaidia kuacha punyeto.
Soma Zaidi...Nini husababisha korodani moja kuwa kubwa kuliko nyingine
kama pumbu moja ni kubwa uliko jingine post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakwend akuangalia vinavyoweza kusababisha korodani moja kuw akubwa zaidi ya lingine
Soma Zaidi...