Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.
Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n
1. Kwanza kabisa uchungu usio wa kawaida ni uchungu ambao utokea zaidi ya massa kumi na mawili na uchungu unakuwa na nguvu kama kawaida na mtoto hatoki tumboni mwa Mama kwa hiyo Kuna sababu zinazosababisha uchungu kupita mda wake,
2. Uchungu kuwa kidogo.
Kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa na nguvu Ili kuweza kumfanya mtoto apite na kuzaliwa mapema lakini tatizo utokea pale uchungu unapokuwa kidogo na kusababisha mtoto asitoke mapema na pia mtoto anakuwa Hana uwezo wa kusukuma viungo vya Mama na kusababisha uchungu, hali inayofanya mtoto kutozaliwa mapema kwa mda
3. Kiuno cha Mama kushindwa kupitisha mtoto, Kuna wakati mwingine muundo wa kiuno cha Mama ushindwa kupitisha mtoto na hivyo kusababisha uchungu kuwapo kwa mda mrefu, hali hii kwa kitaalamu huitwa cephalopelvic disproportion, kwa hiyo wauguzi na wote wanaozalisha wanapaswa kumtambua tatizo hili na kuhakikisha kuwa mtoto anapata sehemu Sahihi ya kupita na ikiwezekana upasuaji unapaswa kutolewa Ili kuruhusu mtoto apitishwe.
4. Ikitokea mtoto akakosa msaada wa haraka na kukaa tumbo bila kutoka hali hii usababisha mtoto kuchoka sana na Mama akilazimisha kusukuma akiwa kwenye hali hii anaweza kusababisha kumuua mtoto kwa kumbana na kusababisha ulemavu kwa Mama kwa hiyo ni vizuri kabisa Mama kuangaliwa njia mapema Ili kuweza kumtambua kama mtoto ataweza kuzaliwa kwa njia ya kawaida au upasuaji ufanyike, kwa hiyo Ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto ni vizuri kuwepo wahudumu wenye sifa za kuzalisha.
5. Mtoto kutanguliza USO.
Kuna wakati mwingine mtoto utanguliza uso badala ya kichwa hali hii usababisha mtoto kushindwa kutoka na kutumia mda mrefu wa mtoto kuzaliwa, kwa hiyo Mama anaweza kupata uchungu kwa mda mrefu kwa sababu ya kitangulizi cha mtoto, ni vizuri kabisa kuangalia mtoto katanguliza nini Ili kuweza kuepuka mtoto kuzaliwa amechoka na kusababisha matatizo kwa Mama na mtoto pia
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 web hosting 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa Mama
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.
Soma Zaidi...Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...Madhara ya tumbaku na sigara
Post hii itakwenda kuangalia madhara ya tumbaku na sigara anayoweza kuyapata mvutaji
Soma Zaidi...Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Post hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, mara nyingi tatizo hili uwakumba akina mama mbalimbali ambapo mtoto uzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Soma Zaidi...Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto
Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Soma Zaidi...