Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.
Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n
1. Kwanza kabisa uchungu usio wa kawaida ni uchungu ambao utokea zaidi ya massa kumi na mawili na uchungu unakuwa na nguvu kama kawaida na mtoto hatoki tumboni mwa Mama kwa hiyo Kuna sababu zinazosababisha uchungu kupita mda wake,
2. Uchungu kuwa kidogo.
Kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa na nguvu Ili kuweza kumfanya mtoto apite na kuzaliwa mapema lakini tatizo utokea pale uchungu unapokuwa kidogo na kusababisha mtoto asitoke mapema na pia mtoto anakuwa Hana uwezo wa kusukuma viungo vya Mama na kusababisha uchungu, hali inayofanya mtoto kutozaliwa mapema kwa mda
3. Kiuno cha Mama kushindwa kupitisha mtoto, Kuna wakati mwingine muundo wa kiuno cha Mama ushindwa kupitisha mtoto na hivyo kusababisha uchungu kuwapo kwa mda mrefu, hali hii kwa kitaalamu huitwa cephalopelvic disproportion, kwa hiyo wauguzi na wote wanaozalisha wanapaswa kumtambua tatizo hili na kuhakikisha kuwa mtoto anapata sehemu Sahihi ya kupita na ikiwezekana upasuaji unapaswa kutolewa Ili kuruhusu mtoto apitishwe.
4. Ikitokea mtoto akakosa msaada wa haraka na kukaa tumbo bila kutoka hali hii usababisha mtoto kuchoka sana na Mama akilazimisha kusukuma akiwa kwenye hali hii anaweza kusababisha kumuua mtoto kwa kumbana na kusababisha ulemavu kwa Mama kwa hiyo ni vizuri kabisa Mama kuangaliwa njia mapema Ili kuweza kumtambua kama mtoto ataweza kuzaliwa kwa njia ya kawaida au upasuaji ufanyike, kwa hiyo Ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto ni vizuri kuwepo wahudumu wenye sifa za kuzalisha.
5. Mtoto kutanguliza USO.
Kuna wakati mwingine mtoto utanguliza uso badala ya kichwa hali hii usababisha mtoto kushindwa kutoka na kutumia mda mrefu wa mtoto kuzaliwa, kwa hiyo Mama anaweza kupata uchungu kwa mda mrefu kwa sababu ya kitangulizi cha mtoto, ni vizuri kabisa kuangalia mtoto katanguliza nini Ili kuweza kuepuka mtoto kuzaliwa amechoka na kusababisha matatizo kwa Mama na mtoto pia
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Fahamu kuhusu mapacha wanaofanana
Post hii inahusu zaidi watoto mapacha wanaofanana,ni watoto wanaozaliwa wakiwa wanaofanana kwa sura na hata group la damu huwa ni Moja.
Soma Zaidi...Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Soma Zaidi...Sababu za za ugumba kwa Mwanaume
Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa Mwanaume, ni sababu ambazo umfanye mwanaume ashindwe kumpatia mwanamke mimba.
Soma Zaidi...Faida za kula yai lililopikwa kwa mama mjamzito
Yai lililopikwa ni chanzo kizuri cha protini, vitamini, na madini muhimu kwa mama mjamzito. Husaidia katika ukuaji wa mtoto tumboni, afya ya mama, na kuimarisha kinga ya mwili.
Soma Zaidi...Samahani nauliza mjamzito akiwa na presha140/90 Kuna madhara?
Presha ya kupanda hypertension huweza kuzumbuwa watu kwa jinsia zote, na umri wote. Wajawazito pia wamekuwa wakisumbuliwa na presha hii mara kwa mara.
Soma Zaidi...Mimba iliyotunga nje
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya
Soma Zaidi...