Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
1. Mayai kushindwa kupevuka.
Hili ni tatizo ambalo uwakumba wanawake kwa kiwango cha asilimia arobaini kwa hiyo
mayai yakishindwa kupevuka usababisha kuwepo kwa ugumba.
2. Maambukizi sugu ya PID.
Kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi ya PID usababisha sehemu mbalimbali za via vya uzazi kuziba na kushindwa kuruhusu mayai kupita kwa ajili ya urutubishaji.
3. Mvurugiko wa homoni.
Na lenyewe hili ni tatizo kubwa ambapo homoni uweza kuongezeka au kupungua kwa hiyo kama ni homoni za uzazi zikapungua ni shida na ikiwa zikaongezeka na nalo ni tatizo jingine kwa hiyo homoni zinapaswa kulinga kabisa na kuwa sawia.
4. Kuwepo kwa uvimbe au maji maji kujaa kwenye sehemu ya kupitisha mayai.
Kuna wakati mwingine mirija ya kupitisha mayai inaweza kujaa maji maji au kwa wakati mwingine kuziba kabisa kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha maambukizi , kwa hiyo mayai hayawezi kupita kutoka kwenye ovaries na kuingia kwenye mirija kwa ajili ya urutubishaji.
5. Au wakati mwingine Kuna wakati panakuwepo na uvimbe , na pia uvimbe huo hauwezi kuruhusu mayai kupita kutoka kwenye ovaries mpaka kwenye mirija ya urutubishaji mpaka uvimbe huo kuondolewa ndipo mayai yanaweza kupita kwa ajili ya urutubishaji.
6. Mayai kuharibika kabla ya umri.
Kuna wakati mwingine mayai yanaweza kuwepo kabisa na ya kutosha na kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi mayai hayo uharibika kabla ya umri wake hali ambayo usababisha kuwepo kwa kiwango kikubwa cha ugumba kwa akina Mama kwa hiyo matibabu ni lazima Ili kuweza kuzuia maambukizi ya nayosababisha kutokomaa kwa mayai.
7. Kuwepo kwa matatizo au asidi nyingi kwenye mlango wa kizazi na uke .
Kwa sababu asidi ya kwenye uke uwa ni ya kawaida kwa ajili ya kuruhusu mbegu kupita na kurutubisha mayai Kuna wakati asidi inakuwa nyingi na kusababisha kuuua megu za kiume kabla hazijaendea kurutubisha mayai.
8. Kuwepo kwa makovu kwenye mji wa mimba.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na makovu kwenye mji wa mimba hali ambayo usababisha mimba kutoweza kutungwa kwa sababu ya kutokuwepo sehemu ya kutungwa.
9. Kulegea au kuziba kwa shingo ya kizazi.
Kuna wakati kunakuwepo kwa tatizo la kulegea na kuziba kwa shingo ya kizazi hali ambayo usababisha mimba bkushindwa kutungwa.
10. Uzito wa kupita kiasi.
Kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta mwilini usababisha kitendo cha urutubishaji kuleta shida na kusababisha ugumba, kwa hiyo akina Mama wenye uzito wa kupita kiasi ni vizuri kabisa kupunguza Uzito na kupata uja uzito.
11. Unywaji wa pombe kupita kiasi na uvutaji wa sigara kupita kiasi.
Kuna akina Mama wenye tatizo la kuvuta sigara kupita kiasi na kupiga pombe ya uhakika hali ambayo usababisha baadhi ya homoni kushindwa kufanya kazi vizuri na hatimaye kuwepo kwa ugumba.
12. Magonjwa sugu katika mfumo wa upumuaji.
Kwa kawaida Kuna tatizo la magonjwa sugu katika mfumo wa upumuaji nayo uharibu ubora wa mayai na mzunguko wa damu kwa hiyo ni vizuri kabisa kutibu magonjwa haya kabla hayajaleta matatizo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Ni Swali kila mjamzito anataka kujiuliza hasa akiwa katika mimba ya kwanza. Wengine wanataka kujuwa ni muda gani anujuwe mavazi makubwa. Kama na wewe unataka kujuwa muda ambao tumbo huwa kubwa, endelea kusoma.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufunza mambo mengi kuhusu tezi dume kama chanzo, dalili, matibabu, njia za kujikinga na mambo hatari yanayoweza kukusababishia kupata tezi dume.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukutania madhara ya kuoiga punyeto kwa afya yako.
Soma Zaidi...Swali langi ni hiliMama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?
Soma Zaidi...Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia Faida, hasara, na madhara ya Kufunga kizazi kwa Wanaume.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maji ya Amniotic ni maji ambayo uzunguka mtoto na kufanya kazi mbalimbali kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...