Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
1. Mayai kushindwa kupevuka.
Hili ni tatizo ambalo uwakumba wanawake kwa kiwango cha asilimia arobaini kwa hiyo
mayai yakishindwa kupevuka usababisha kuwepo kwa ugumba.
2. Maambukizi sugu ya PID.
Kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi ya PID usababisha sehemu mbalimbali za via vya uzazi kuziba na kushindwa kuruhusu mayai kupita kwa ajili ya urutubishaji.
3. Mvurugiko wa homoni.
Na lenyewe hili ni tatizo kubwa ambapo homoni uweza kuongezeka au kupungua kwa hiyo kama ni homoni za uzazi zikapungua ni shida na ikiwa zikaongezeka na nalo ni tatizo jingine kwa hiyo homoni zinapaswa kulinga kabisa na kuwa sawia.
4. Kuwepo kwa uvimbe au maji maji kujaa kwenye sehemu ya kupitisha mayai.
Kuna wakati mwingine mirija ya kupitisha mayai inaweza kujaa maji maji au kwa wakati mwingine kuziba kabisa kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha maambukizi , kwa hiyo mayai hayawezi kupita kutoka kwenye ovaries na kuingia kwenye mirija kwa ajili ya urutubishaji.
5. Au wakati mwingine Kuna wakati panakuwepo na uvimbe , na pia uvimbe huo hauwezi kuruhusu mayai kupita kutoka kwenye ovaries mpaka kwenye mirija ya urutubishaji mpaka uvimbe huo kuondolewa ndipo mayai yanaweza kupita kwa ajili ya urutubishaji.
6. Mayai kuharibika kabla ya umri.
Kuna wakati mwingine mayai yanaweza kuwepo kabisa na ya kutosha na kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi mayai hayo uharibika kabla ya umri wake hali ambayo usababisha kuwepo kwa kiwango kikubwa cha ugumba kwa akina Mama kwa hiyo matibabu ni lazima Ili kuweza kuzuia maambukizi ya nayosababisha kutokomaa kwa mayai.
7. Kuwepo kwa matatizo au asidi nyingi kwenye mlango wa kizazi na uke .
Kwa sababu asidi ya kwenye uke uwa ni ya kawaida kwa ajili ya kuruhusu mbegu kupita na kurutubisha mayai Kuna wakati asidi inakuwa nyingi na kusababisha kuuua megu za kiume kabla hazijaendea kurutubisha mayai.
8. Kuwepo kwa makovu kwenye mji wa mimba.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na makovu kwenye mji wa mimba hali ambayo usababisha mimba kutoweza kutungwa kwa sababu ya kutokuwepo sehemu ya kutungwa.
9. Kulegea au kuziba kwa shingo ya kizazi.
Kuna wakati kunakuwepo kwa tatizo la kulegea na kuziba kwa shingo ya kizazi hali ambayo usababisha mimba bkushindwa kutungwa.
10. Uzito wa kupita kiasi.
Kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta mwilini usababisha kitendo cha urutubishaji kuleta shida na kusababisha ugumba, kwa hiyo akina Mama wenye uzito wa kupita kiasi ni vizuri kabisa kupunguza Uzito na kupata uja uzito.
11. Unywaji wa pombe kupita kiasi na uvutaji wa sigara kupita kiasi.
Kuna akina Mama wenye tatizo la kuvuta sigara kupita kiasi na kupiga pombe ya uhakika hali ambayo usababisha baadhi ya homoni kushindwa kufanya kazi vizuri na hatimaye kuwepo kwa ugumba.
12. Magonjwa sugu katika mfumo wa upumuaji.
Kwa kawaida Kuna tatizo la magonjwa sugu katika mfumo wa upumuaji nayo uharibu ubora wa mayai na mzunguko wa damu kwa hiyo ni vizuri kabisa kutibu magonjwa haya kabla hayajaleta matatizo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti.
Soma Zaidi...Post yetu imebeba mada inayohusiana na wanaume wanaowashwa Uume embu tuone dalili zinazopelekea kuwashwa kwa penis. Uume(penis) ni party ya mwanaume ya sehemu za siri.pia wanaume ambao hawajatahiriwa(unsircumside) kwasababu Ile ngozi ya juu husababishwa k
Soma Zaidi...Miongoni mwa changamoto za ujauzito ni maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanawezakuwaya kawaida ama makali zaidi. Vyema kufika Kituo cha Afya endapoyatakuwa makali.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia au namna ya kufunga kitovu cha mtoto mara tu anapozaliwa, kwa kawaida tunafahamu kwamba ili mtoto aweze kuishi akiwa tumboni anategemea sana kula na kufanya shughuli zake kwa kupitia kwenye plasenta kwa hiyo mtoto akizaliwa tu
Soma Zaidi...Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mbegu ambazo ni nzima na ambazo zina sifa ya kutungisha mimba kwa hiyo mbegu hizi utazigundua kwa kuwa na sifa zifuatazo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito faida na hasara zake
Soma Zaidi...posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot
Soma Zaidi...Post huu inahusu zaidi mambo yanayopelekea ugumba kwa wanaume, ni mambo ambayo uchangia au upelekea mwanaume kukosa uzazi.
Soma Zaidi...