picha

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali.

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme ( sehemu ya tano).

1. Baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kugundua kwamba anapenda sana mali. Kwa hiyo bibi akagundua namna ya kumtega ili aweze kuona mke wa pili ili aje apate ufalme na bibi apate sehemu ya kuishi na kutunzwa.

 

2. Palikuwepo na mzee mmoja alikuwa na kiwanja kikubwa cha madini mbalimbali kwa hiyo bibi alisafiri akaenda huku na kuongea na mzee kwamba kuna mtoto wa kiume wa mfalme angependa kuchimba madini pamoja nawe, basi yule Mzee aliogopa sana na kusema yeye ni nani mpaka afanye kazi na mtoto wa pekee wa kiume wa mfalme? Bibi akasema usihofu yeye ameomba,

 

3. Basi yule mzee alikuwa na mabinti wanne wazuri sana . Bibi akamwambia sheria ni kwamba ukimpatia mtoto wa kiume wa mfalme sehemu ya kuchimba ni lazima umpatie na binti mmoja wa kumliwadha na mzee akafurahi sana kuona binti yake anaolewa na mtoto wa mfalme, kwa hiyo binti akaandaliwa vizuri na kupambwa kwa ajili ya mtoto wa kiume wa mfalme.

 

4. Basi bibi alienda kwa mtoto wa kiume wa mfalme na kumwambia yote kuhusu mali na madini kutoka kwa yule mzee, mtoto wa kiume wa mfalme alifurahi sana kusikia kitu kinachoitwa madini na kusikia mali kwa hiyo siku hiyo mtoto wa kiume wa mfalme akaandamana na umati mkubwa wa watu na farasi watu wa kijiji cha yule mzee waliogopa  sana ila bibi aliwahakikishia usalama na amani pia.

 

5. Basi mtoto wa mfalme akaonyeshwa sehemu kubwa ya kuchimba akaanza kuchimba, na akapiga hema uko, ila siku ya kwanza alichoka mno alipoingia chumbani kwake alikuta binti mzuri alifurahi sana kuona jinsi alivyoandaliwa na yule mzee binti mzuri mno akalala naye na ilikuwa siku ya kubeba mimba akabeba mimba ya mapacha wa kiume na baada ya siku chache aliambiwa habari ya ujauzito wa mke wake alifurahi sana kwa sababu yule mke wa kwanza hakuwahi kuwa na mimba.

 

6. Basi bibi baada ya kuchimba kila kitu akamwacha mtoto wa kiume wa mfalme na mke mpa akaenda kwa mke mdogo wa mfalme akamwambia kila kitu na yule mama alifurahi mno.

 

Itaendelea baadae

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF Views 2985

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili baada ya kuhamia shule mpya.

Soma Zaidi...
Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi

Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sita

Post hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sehemu ya sita.sehemu hii inaonyesha jinsi bibi alivyo ndumila kuwili na hapendi kuonekana mbaya.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo.

Soma Zaidi...
Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya pili)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara.

Soma Zaidi...