Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali.
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme ( sehemu ya tano).
1. Baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kugundua kwamba anapenda sana mali. Kwa hiyo bibi akagundua namna ya kumtega ili aweze kuona mke wa pili ili aje apate ufalme na bibi apate sehemu ya kuishi na kutunzwa.
2. Palikuwepo na mzee mmoja alikuwa na kiwanja kikubwa cha madini mbalimbali kwa hiyo bibi alisafiri akaenda huku na kuongea na mzee kwamba kuna mtoto wa kiume wa mfalme angependa kuchimba madini pamoja nawe, basi yule Mzee aliogopa sana na kusema yeye ni nani mpaka afanye kazi na mtoto wa pekee wa kiume wa mfalme? Bibi akasema usihofu yeye ameomba,
3. Basi yule mzee alikuwa na mabinti wanne wazuri sana . Bibi akamwambia sheria ni kwamba ukimpatia mtoto wa kiume wa mfalme sehemu ya kuchimba ni lazima umpatie na binti mmoja wa kumliwadha na mzee akafurahi sana kuona binti yake anaolewa na mtoto wa mfalme, kwa hiyo binti akaandaliwa vizuri na kupambwa kwa ajili ya mtoto wa kiume wa mfalme.
4. Basi bibi alienda kwa mtoto wa kiume wa mfalme na kumwambia yote kuhusu mali na madini kutoka kwa yule mzee, mtoto wa kiume wa mfalme alifurahi sana kusikia kitu kinachoitwa madini na kusikia mali kwa hiyo siku hiyo mtoto wa kiume wa mfalme akaandamana na umati mkubwa wa watu na farasi watu wa kijiji cha yule mzee waliogopa sana ila bibi aliwahakikishia usalama na amani pia.
5. Basi mtoto wa mfalme akaonyeshwa sehemu kubwa ya kuchimba akaanza kuchimba, na akapiga hema uko, ila siku ya kwanza alichoka mno alipoingia chumbani kwake alikuta binti mzuri alifurahi sana kuona jinsi alivyoandaliwa na yule mzee binti mzuri mno akalala naye na ilikuwa siku ya kubeba mimba akabeba mimba ya mapacha wa kiume na baada ya siku chache aliambiwa habari ya ujauzito wa mke wake alifurahi sana kwa sababu yule mke wa kwanza hakuwahi kuwa na mimba.
6. Basi bibi baada ya kuchimba kila kitu akamwacha mtoto wa kiume wa mfalme na mke mpa akaenda kwa mke mdogo wa mfalme akamwambia kila kitu na yule mama alifurahi mno.
Itaendelea baadae
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 ai web app 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)
Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambao walipoteana katika hali za kukimbizwa na wazazi Ili waweze kutimiza ndoto zao na siku wakakutana wakiwa watu wazima.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, kuhusu hadithi hii ni pale Jackie anaandikiwa barua na Julius ili apotezwe akili na wavulana wengine kwa sababu Jackie aliwapita darasani.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.
Soma Zaidi...WAKATI WA KUFUMBUKA
Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha.
Soma Zaidi...USALITI (sehemu ya tatu)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.
Soma Zaidi...