picha

NIMLAUMU NANI part 1

Post hii inahusu hadithi Moja ya kijana maaalufu aliyeitwa Frank, ni kijana aliyekuwa mwaminifu ila amekumbana na wasichana wengi wanamasaliti ukizingatia Frank alikuwa kijana mstaalabu na mwaminifu sana ila anafikia kufanya maamuzi magumu kufuatana na ku

"NIMLAUMU NANI"

1. Ni asubuhi Moja nzuri iliyokuwa na upepo kidogo na jua kuanza kujitokeza huku ndege wakiimba nyimbo nzuri na watu wakijiandaa kwenda makazini, ila kwa sababu Frank siku hiyo hakuwa na picha atatokea wapi kwa sababu yeye kupata kazi kwa siku ilikuwa ni majaliwa ya mwenyezi Mungu kwa sababu alitegemea vibarua Ili mkono uweze kuingia kinywani kwa hiyo siku hiyo alikuwa Hana picha na hata hajapata mtu wa kumwita kumpatia kibarua. Frank aliendelea kuvuta shuka ghafla akasikia simu ikiitia kupokea anasikia maneno makali kutoka kwa mpenzi wake Amina, ni maneno ya kusikitisha yakisema.

 

 

 

 

2. "Wewe ni mpenzi gani maskini naona huwezi kunitunza kwa hiyo chukua zako hamsini na mimi nichukue zangu hamsini kwa sababu siwezi kuishi na mvulana maskini Kama wewe" maneno haya yalimchoma sana Frank na yalimfanya ahamke kutoka usingizi na kukimbia kwenda dukani kutafuta vocha kwa ajili ya kuongea na mpenzi wake Amina, lakini Amina alimjibu hivi, " yaani wewe maskini hujanielewa sikutaki na usinifatilie na koma kwa sababu mimi sio wa kiwango chako, baada ya Frank kusikia maneno kama hayo aliumia sana na kuwa na uchungu sana kwa sababu alitegemea sana Amina kama faraja kwake, alifikilia sana akajipigapiga kichwa ,akajishauri na akaamua kwenda kwa rafiki yake James kuomba ushauri Ili kumbembeleza Amina kuendelea kuwa karibu na frank.

 

 

 

 

 

3 Basi frank aliamua kujiandaa vizuri kwenda kwa rafiki yake James kumwambia yaliyo moyoni, ingawa  Frank alikuwa na uchungu aliamua kuwa mkakamavu Ili asiweze kuonyesha uchungu kwa watu aliokutana nao kwa sababu ilimpasa kupanda daladala kwa sababu Kuna mwendo kama saa moja  hivi, Frank alikuwa kwenye kituo cha daladala anmesubiri daladala ghafla akaja gari linaendeshwa na msichana mlembo sana yule msichana akamwambia frank aingie kwenye gari ampe lift akihaidi kumfikisha pale anapoenda basi frank akakubali akapanda lile gari na alifurahi kwa sababu na nauli kwake  ilikuwa ni shida.

 

 

 

 

4. Basi frank alipokuwa kwenye gari alikuwa na uzuni, ila yule msichana aliamua kusimamisha gari Ili kujua yaliyompata Frank, basi frank akapaswa kumwambia msichana yaliyompata yule msichana akaumia sana akaamua kumpa Frank moyo na kumpatia frank number za simu Ili waje kuongea baadae basi frank akafikishwa kwa rafiki yake wakaagana na yule msichana wakapeana number za simu  basi frank alipofika kwake na James akabisha hodi hakufunguliwa akazunguka nyuma ya nyumba hakuona mtu baadae aliamua kuingia ndani mpaka chumbani kwa James ndipo aliposhutuka kuwakuta James na Amina wako kitandani wamekumbatiana.

 

Itaendelea.

 

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF Views 2095

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰3 ai web app     πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Hadithi katika kijiji cha burugo

Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .

Soma Zaidi...
WAKATI WA KUFUMBUKA

Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya nne)

Post hii inahusu zaidi watoto Hawa wawili wakiwa kwenye kituo cha mapumziko ambapo mtoto wa tajiri anabugia soda aliyopewa na yule mwalimu pia tumbo linaanza tena na anaanza kuendesha

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.

Soma Zaidi...
Ni nani kama mama

Nani kama mama? Hadithi hii itakufunza umuhimu wa kuwa muwazi kuhusu familia yako.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA

Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama.

Soma Zaidi...