Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.
1. Basi siku ya maongezi ikafika kati ya bibi na mke wa mdogo wa mfalme,bibi akamsalimia vizuri akampa sifa zote ila akamwambia kwamba wafanye utaratibu wa kumshauri kijana wa kiume wa mfalme awe na mke wa pili ili aweze kupata ufalme wa nane kwanza na mke huyu ambaye ni ndugu yake na kadri ya sheria hataweza kupata ufalme.
2. Basi bibi na yule mke mdogo wa mfalme wakamwita yule kijana na kumpasha habari ya kila kitu kinachoendelea ila kijana akasema siwezi kumwacha mke wangu ili niwe mfalme bora nikakosa ufalme ila nikaishi na mpenzi wangu, mama yake baada ya kusikia hivyo akahisi kuchanganyikiwa na siku zinaenda kijana hana mda mpaka mama yake akajuta na kusema bora ningewazaa watoto wangu wakiwa wawili.
3. Basi bibi akamwambia Mama usihofu kila kitu kitakuwa sawa nihaidi utanipa nini ,Mama akamwambia nitakutunza mpaka utakapofariki, akasema iwapo yeye atafariki ataacha ujumbe wa bibi kutunzwa maisha yake yote, bibi akasema tuandikiane wakaandikiana bibi akaanza mbinu za kuhakikisha kuwa ufalme unabaki mikononi mwa uzao wa mke mdogo.
4. Baada ya bibi kutoka kwa yule mke mdogo akaenda kwa yule mke mkubwa ambaye alimwambia aandae binti mkubwa kwa ajili ya kupata umalkia, basi bibi akaenda kwa ndugu wa mfalme akamshawishi kijana wa ndugu wa mfalme akamwambia , mfalme ana mpango wa kugawa mali kwa watoto wake ila mali kubwa zitaenda kwa binti wa kwanza na kwa mme wake akamwambia kijana kwa nini usimtongoze yule binti na ukampa mapenzi ya kweli ili upate zawadi nyingi na kuishi na binti wa mfalme.
5. Kijana akafanya hivyo na akafanikiwa kumpa binti yule mimba na binti akaogopa kuishi kwa mfalme akiwa na mimba kwa sababu siku zile wasichana waliobobea mimba kwa waliuawa na yule kijana akamwoa mtoto wa mfalme . Kwa hiyo sifa za kuwa malkia zikaishia hapo . Bibi baada ya kufanikiwa mbinu hiyo akaenda kwa mke mdogo na kutoa taarifa mke mdogo alifurahi sana ila akaendelea kumwacha bibi akae kwa wake wenza ili kuleta habari zaidi, basi bibi akapanga kukutana na mke mdogo kwa maongezi zaidi,
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowPosti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali
Soma Zaidi...Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hadithi ya Binti mfalme ni hadithi ya kusisimua, kuhusu hadithi hii ni kwamba mfalme alihitaji mtoto wa kiume ila wanawake wote hawakumpata ila alitokea mke mdogo mmoja wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha mmoja wa kiume na
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kijana Frank anayelazimishwa kuolewa na Amisa yeye hayuko tayari ila kwa sababu ya maisha kuwa magumu anaamua kulala na Amina na kumbebesha Mimba ya watoto mapacha.
Soma Zaidi...Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma.
Soma Zaidi...