Hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi hadithi ya Binti mfalme ni hadithi ya kusisimua, kuhusu hadithi hii ni kwamba mfalme alihitaji mtoto wa kiume ila wanawake wote hawakumpata ila alitokea mke mdogo mmoja wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha mmoja wa kiume na

Hadithi ya Binti mfalme.

1. Hapo zamani za kale palikuwepo na mfalme mmoja aliitwa Gwanta , mfalme alioa wanawake watano ila kati ya wanawake wote hakuna aliyefanikiwa kupata mtoto wa kiume, hali hii ilimuumiza sana mfalme na kufikilia mambo mengi hasa mtoto wa kuridhi Mali yake, katika kuongea na washauri wake jinsi anavyoumia kwa sababu ya kutopata mtoto wa kiume waliamua kumpatia mfalme Binti mzuri Sana wa miaka kumi na mbili Ili aweze kumfariji, kwa hiyo mfalme aliishi na Binti huyo kwa miaka mitano na hatimaye akabeba mimba.

 

2. Kitendo cha mfalme kuishi na yule mke mdogo kilifanya mfalme awasahau wanawake wengine na pia alikuwa anampenda sana yule mke mdogo na yule mke alikuwa anamtii mfalme na kufanya kila kitu alichokipenda na pia yule mke mdogo alikuwa na uso mzuri na WA kuvutia sana kwa macho. Kwa hiyo wale wanawake watano wa mfalme wakimchukia sana yule mke mdogo isipokuwa mke wa tatu aliyeitwa Janka alimpenda kisiri Siri na kumwambia yule mke mdogo kila kitu wanachopanga juu yake.

 

3. Siku Moja baada ya mimba kukua na kuonekana kwa kila mmoja wale wake wenza wakaenda kwa mganga na kwa mizimu yao Ili kujua kuhusu mimba iliyobebwa ni mtoto gani , kwanza mganga akawaambia kuwa ni mtoto wa kiume na WA kike pia na mizimu ikatoa jibu hilo hilo,kwa hiyo walipofahamu hayo wakatafuta mbinu za kumwangamiza, yule Janka mke wa tatu akamwambia kimbia Ili usiuawe na kweli yule Binti akakimbilia mbali kabisa mbugani na huku akakutana na bibi aliyekuwa na kilimo cha njugu mawe, yule mke akamwekeza kila kitu na yule bibi akaamua kumficha.

 

4. Baada ya mfalme kutomwona mke wake alilia sana na kuita mkutano kwamba atakayemwona yule mke mdogo atapewa nusu ya ufalme wake, watu wakaanza safari kwenda sehemu mbalimbali kwa ajili ya kumtafuta, basi Kuna waliofikia kwa yule bibi wakaeleza kila kitu na ahadi za mfalme,bibi akawajibu sijamwona lengo la bibi ni kusubiri yule mke mdogo wa mfalme ajifungue Ili aweze kupeleka mtoto na mke mdogo wa mfalme na alijua wazi kuwa atapata zawadi kubwa na maisha mazuri.

 

5. Basi siku za kujifungua zikafika yule bibi alikuwa mtaalamu na mkunga akamzalisha yule mke mdogo wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha wa kwanza wa kiume na WA pili wa kike , mke mdogo wa mfalme alifurahi sana ila kwa sababu bibi yule alipenda sana sifa alimwambia mke mdogo wa mfalme kwamba wapeleke mtoto wa kiume tu wa kike akae na bibi na wakafanikiwa kufanya hivyo, basi bibi akakimbia kwa mfalme akatoa habari kwamba mke mdogo wa mfalme amepatikana na amejifungua mtoto wa kiume. 

 

6. Mfalme baada ya kusikia habari hizo alifurahi sana mpaka akazimia baadae alizinduka akatuma viongozi wake wamfuate yule mke mdogo,walimleta na kuimba njia nzima wale wake wenza waliumia sana isipokuwa yule rafiki yake , basi bibi akapewa zawadi nyingi na pia akaamuliwa Aishi na mfalme alikataa kwa sababu ya kuwepo kwa yule mtoto wa kike aliyebaki kwake, kwa hiyo bibi akapewa zawadi nyingi sana na akajengewa kwake na wakaishi vizuri na yule mtoto wa kike aliyebaki kwake.

 

 

 

7. Baada ya miaka na miaka bibi aliendelea kutunza yule Binti akakuwa akawa dada mzima mzuri Sana kwa umbo na sura ila alimwuliza bibi kuhusu history yake ila bibi hakumwambia basi na yule kijana wa kiume wa mfalme akakua akafikia wakati wa kuoa ila alimwambia mfalme baba nioze msichana wa kwa bibi kwa sababu nampenda sana,basi mfalme akatuma ujumbe kwa bibi , yule bibi kusikia hivyo alizimia na kuwa mgonjwa sana kwa hiyo yule dada akamuuguuza bibi yake ila bibi alipoona hali ni mbaya akapaswa kumwambia mjukuu wake story yote,Binti akaumia sana kusikia hivyo.

 

8. Kadri siku zinavyoonda ndivyo yule kijana akaendelea kumpenda Binti Ila Binti anakataa kuolewa naye na Mama wa watoto alikuwa anapinga sana , ndipo yule mvulana akashauliwa kuoa Binti mwingine ila alikataa kabisa alisema anampenda sana Binti wa kwa bibi. Basi siku Moja mvulana alitunga wimbo i akaanza kumwimbia yule Binti alisema.

 

9. Dada nakupenda sana kushindwa kukupata Bora nife, kujiua ni kazi rahisi kusema ukweli usipokubali nitajiua, 

 

10, na msichana akajibu, mimi nakupenda sana na ningependa kuolewa na kijana wa mfalme ila mimi na wewe ni ndugu mama alituzaa wawili mimi na wewe kwa kuwa mfalme alihitaji sana mtoto wa kiume mimi nilibakizwa kwa bibi wewe ukapelekwa kwa mfalme.

 

11. Baada ya yule kijana wa kiume wa mfalme kusikia hivyo aliumia sana na kwenda kumwambia mama yake mama naye akapanic sana akafikilia kuwa inshu hii ikifika kwa mfalme na watu wote atapata aibu kwa hivyo yule mama akapanga mbinu za kumtorosha mbali mtoto wa kike na yule Bibi  mbali Ili yule kijana asiweze kuwaona tena na apoteze Ile kumbukumbu ya yule dada ila kijana alimpenda sana na pia kijana hakutoa Siri hiyo kwa mfalme au kwa mtu yeyote ila kijana alisema hata kama ni ndugu mpaka nimuone,basi yule mke wa mfalme akawatorosha akawapeleka mbali kweli ila kijana akaamua kuwatafuta kila sehemu. 

 

Itaendelea

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 4254

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 web hosting    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili baada ya kuhamia shule mpya.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI part 1

Post hii inahusu hadithi Moja ya kijana maaalufu aliyeitwa Frank, ni kijana aliyekuwa mwaminifu ila amekumbana na wasichana wengi wanamasaliti ukizingatia Frank alikuwa kijana mstaalabu na mwaminifu sana ila anafikia kufanya maamuzi magumu kufuatana na ku

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)

Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa.

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 3)

Posti hii inahusu zaidi hasara za kuwa na wivu na kutokuwa wazi, sehemu hii inahusu zaidi maendeleo ya Lisa shuleni yanakuwa mabaya zaidi na lina anaendelea kumtunzia siri lengo lake lina ni kuendelea kuwa wa kwanza darasani.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA

Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI (sehemu ya sita)

Post inahusu zaidi hadithi ya NIMLAUMU NANI ambayo ni sehemu ya sita, katika kipengele hiki tunaenda kumwona msichana Amina anapambana na hatimaye anafunga ndoa ya kiserikali na Frank

Soma Zaidi...
Mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)

Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na maskini (sehemu ya pili)

Post hii inahusu zaidi watoto wa wawili ambapo mmoja ni mtoto wa tajiri na mwingine ni mtoto wa maskini.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali.

Soma Zaidi...