picha

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sita

Post hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sehemu ya sita.sehemu hii inaonyesha jinsi bibi alivyo ndumila kuwili na hapendi kuonekana mbaya.

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sita.

1. Baada ya bibi kutoka kumpasha habari mke mdogo wa mfalme kwa kila kitu kinachoendelea alirudi kwa mke mkubwa  wa mfalme na kumwambia kwamba binti yako ameharibu kwa kuolewa na yule kijana ila ni lazima tufanye mbinu ila upate mfalme kwenye ukoo wako  kwa sababu nitaongea na mke mdogo wa mfalme aende kumtembelea kijana wake ilai siku akienda nenda ulale na mfalme utapata mimba ya mtoto wa kiume,kwa sababu bibi ashafanya mazindiko yake ili mama apate mtoto wa kiume.

 

2. Basi ilifika wakati yule mtoto wa  Mzee na kijana wa kiume wakapata watoto wa kiume wawili mapacha, kwa hiyo yule mke mdogo akaenda kuwasalimia wajukuu wa kiume ili aje ampashe mfalme habari, yule Mke mdogo wa mfalme alipoondoka yule mke mkubwa akaenda kwa mfalme akalala na mfalme akabeba mimba ya mtoto wa kiume, baada ya mke mdogo wa mfalme kurudi bibi akamwambia kwamba mke mkubwa wa mfalme amebeba mimba na dalili ni mtoto wa kiume.

 

3. Basi yule mke mdogo akapanic sana akamuuliza bibi mjanja tufanyeje? Bibi akamwambia tumpeleke yule mke wa kwanza wa kijana wa mfalme mbali na mme wake amsindikize na pia tumwambie mfalme kuwa anapaswa kusimika mrithi wa ufalme, kwa hiyo wakapanga na mtoto wa kiume wa mfalme wakamwahidia mali nyingi kwa sababu ya kupenda mali akakubali kurudi nyumbani kutoka machimboni ila mke yule alimwacha, akamwambia mfalme kwamba niko tayari kurithi ufalme wako, mfalme akafurahi sana ila akampa mashariti kwamba hapendi sherehe anaomba akabidhiwe kadri ya sheria na watu wachache sherehe itakuwa baadae mfalme akakubali.

 

4. Basi kesho yake yule mtoto wa kiume wa mfalme akamwambia mke wake yule pacha wake waende kutembea kwenye ufalme mwingine yule binti akafurahi sana wakaenda walipofika akamwacha huko akampitia mke mwingine yule mwenye mapacha akamleta kwa baba yake mfalme, baba yake akafurahi sana akaandaa sherehe akampatia mtoto wake ufalme na bibi akaitwa kukaa ikulu na baada ya siku chache yule mama mkubwa akajifungua mtoto wa kiume . hadithi yangu imeishia hapo.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF Views 3095

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 ai web app     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na maskini (sehemu ya pili)

Post hii inahusu zaidi watoto wa wawili ambapo mmoja ni mtoto wa tajiri na mwingine ni mtoto wa maskini.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA

Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya tatu)

Post hii inahusu zaidi mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini wakipanda gari kuelekea shule kuanza maisha mapya.

Soma Zaidi...
Ni nani kama mama

Nani kama mama? Hadithi hii itakufunza umuhimu wa kuwa muwazi kuhusu familia yako.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto.

Soma Zaidi...