Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.

Mtoto wa Tajiri na maskini .

1.watoto hawa walikuwa majirani, na walikuwa wanasoma shule moja , kila siku mtoto wa tajiri alikuwa anaamshwa anaoshwa, anasaidiwa kupiga mswaki anavalishwa anaangaliwa cha na baadae anawekwa kwenye gari mpaka shuleni na kufungiwa juice na maanda kwenye begi kwa ajili ya kula baadae , na mda wa saa nne alikuwa anafuatwa shule anaenda kunywa maziwa nyumbani na kurudishwa kuendelea na masomo na baada ya kumaliza masomo mtoto alifuatwa kwa gari mpaka nyumbani baada ya kufika nyumbani alibadilisha nguo akala chakula alichokuwa ameagizwa kupokwe mara nyingi zilikuwa ni Chipsi.

 

 

 

 

 

2. Baada ya kumaliza kula aliwekewa tv akaanza kuangalia katuni na michezo mingine na alipokuwa anachoka anaenda kuogelea kwenye swimming pool na baadaye alikula kila alichopenda kula na baadae alikwenda kulala hata bila kukumbushwa kufanya home work hiyo ndiyo iliyokuwa ratiba ya mtoto wa tajiri.

 

 

 

 

3. Kama nilivyotangulia kusema kwamba palikuwepo pia mtoto wa maskini, yeye ratiba yake ilikuwa tofauti kabisa na mtoto wa tajiri yeye kila siku alijiamsha mwenyewe akanawa uso akajipaka sabini kwa sababu mafuta yalikuwa shida ,akasafisha nyumba kwa kufagia huku akisubiria chai aliyoweka kwenye mafiga akimaliza kufagia  anakunywa chai bila sukari pamoja na kiporo kidogo cha ugali kilichobaki na akikumbuka kumbakizia mdogo wake ambaye bado amelala na akimaliza anaosha vyombo anavaa uniform na kuacha amekunja shuka lake maana alikuwa na Moja la kulalia Kisha anawaaga wazazi anakimbia shuleni kugonga kengere kwa sababu alikuwa time keeper .

 

 

 

 

 

4. Akifika shuleni anawasimamia darasa la kwanza na la pili kwa sababu yeye na mtoto wa tajiri waliokuwa darasa la tano, na baadae anaingia darasani na kuanza kusoma na alikuwa anabaki shuleni mpaka saaa na zikifika saa nane anaenda nyumbani akifika nyumbani ana Kuta wazazi wake bado wako shamba anabadilisha nguo anachukua ndoo anaenda kisomani kuchota maji anayaleta anachemsha maji na kusonga ugali na kupika mboga kwa ajili ya kulisha ugali, akimaliza anakula anawabakizia wazazi wake ila yeye anakula na ndugu yake akimaliza kabla ya jua kuisha anafanya homework mapema na kujisomea kidogo kabla ya giza kuingia kwa sababu hawakuwa na umeme.

 

 

 

 

5, giza likiingia tu anawaosha ndugu zake na yeye anaoga na akimaliza asaidiana kuandaa chakula cha jion na Mama yake na baadae wanawasha tochi wanaenda kula na kulaa na hayo ndiyo maisha na ratiba ya mtoto wa maskini.

 

 

Itaendelea.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/12/16/Friday - 12:36:39 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1040


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hadithi ya binti mwenye kufichwa mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hatma ya kinyozi maishani mwangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Matibabu ya vidonda sugu
Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya vidonda vya tumbo sugu Soma Zaidi...

Ndoa ya Sinbad na binti mfalme
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Malipo ya wema ni wema
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya kinyozi yeye mwenyew
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

SAFARI YA MUUJIZA
Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama. Soma Zaidi...

Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Hadithi ya mvuvi na jini
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme. Soma Zaidi...

Ujio wa wageni wa baraka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Mshenga wa aladini mbele ya mfalme
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...