Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.

Mtoto wa Tajiri na maskini .

1.watoto hawa walikuwa majirani, na walikuwa wanasoma shule moja , kila siku mtoto wa tajiri alikuwa anaamshwa anaoshwa, anasaidiwa kupiga mswaki anavalishwa anaangaliwa cha na baadae anawekwa kwenye gari mpaka shuleni na kufungiwa juice na maanda kwenye begi kwa ajili ya kula baadae , na mda wa saa nne alikuwa anafuatwa shule anaenda kunywa maziwa nyumbani na kurudishwa kuendelea na masomo na baada ya kumaliza masomo mtoto alifuatwa kwa gari mpaka nyumbani baada ya kufika nyumbani alibadilisha nguo akala chakula alichokuwa ameagizwa kupokwe mara nyingi zilikuwa ni Chipsi.

 

 

 

 

 

2. Baada ya kumaliza kula aliwekewa tv akaanza kuangalia katuni na michezo mingine na alipokuwa anachoka anaenda kuogelea kwenye swimming pool na baadaye alikula kila alichopenda kula na baadae alikwenda kulala hata bila kukumbushwa kufanya home work hiyo ndiyo iliyokuwa ratiba ya mtoto wa tajiri.

 

 

 

 

3. Kama nilivyotangulia kusema kwamba palikuwepo pia mtoto wa maskini, yeye ratiba yake ilikuwa tofauti kabisa na mtoto wa tajiri yeye kila siku alijiamsha mwenyewe akanawa uso akajipaka sabini kwa sababu mafuta yalikuwa shida ,akasafisha nyumba kwa kufagia huku akisubiria chai aliyoweka kwenye mafiga akimaliza kufagia  anakunywa chai bila sukari pamoja na kiporo kidogo cha ugali kilichobaki na akikumbuka kumbakizia mdogo wake ambaye bado amelala na akimaliza anaosha vyombo anavaa uniform na kuacha amekunja shuka lake maana alikuwa na Moja la kulalia Kisha anawaaga wazazi anakimbia shuleni kugonga kengere kwa sababu alikuwa time keeper .

 

 

 

 

 

4. Akifika shuleni anawasimamia darasa la kwanza na la pili kwa sababu yeye na mtoto wa tajiri waliokuwa darasa la tano, na baadae anaingia darasani na kuanza kusoma na alikuwa anabaki shuleni mpaka saaa na zikifika saa nane anaenda nyumbani akifika nyumbani ana Kuta wazazi wake bado wako shamba anabadilisha nguo anachukua ndoo anaenda kisomani kuchota maji anayaleta anachemsha maji na kusonga ugali na kupika mboga kwa ajili ya kulisha ugali, akimaliza anakula anawabakizia wazazi wake ila yeye anakula na ndugu yake akimaliza kabla ya jua kuisha anafanya homework mapema na kujisomea kidogo kabla ya giza kuingia kwa sababu hawakuwa na umeme.

 

 

 

 

5, giza likiingia tu anawaosha ndugu zake na yeye anaoga na akimaliza asaidiana kuandaa chakula cha jion na Mama yake na baadae wanawasha tochi wanaenda kula na kulaa na hayo ndiyo maisha na ratiba ya mtoto wa maskini.

 

 

Itaendelea.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 3109

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.

Soma Zaidi...
Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya nne)

Post hii inahusu zaidi watoto Hawa wawili wakiwa kwenye kituo cha mapumziko ambapo mtoto wa tajiri anabugia soda aliyopewa na yule mwalimu pia tumbo linaanza tena na anaanza kuendesha

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il

Soma Zaidi...
Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)

Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa.

Soma Zaidi...
WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 1

Post hii inahusu zaidi hadithi mpya na nzuri inayoitwa wakati wa Kufumbuka, ni hadithi inayohusu maisha ya kawaida ambapo watu ushindwa kudhamini watu wa karibu nao na kuona watu wa mbali ndio wenye maana ila shida zikifika ndipo wanaona umuhimu wao.

Soma Zaidi...
Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi

Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.

Soma Zaidi...