picha

Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.

Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili.

1. Baada ya mtihani kuisha wazazi na vijana wote walikusanyika kwenye ofisi ya nidhamu pamoja na wazazi wao , ila Jackie akili yake yote ilikuwa kwa julius na katika mkutano waliwatenga wasichana kwa wavulana ila Jackie alienda kwa wavulana akiwa ameweka mkono juu ya julius ila julius alijitahidi kuutoa mkono mama alipoona hayo alihisu hasira na kumrikia Jackie na kumpiga makofi kama mawili hivi na baba yake akamshika na kusudi mama yake hasilete Fujo zaidi.

 

2. Ndipo mwalimu aliyemkuta Jackie ananuka pombe kwenye chumba cha mtihani akamsimulia kila kitu kilivyoendelea ndivyo marafiki zake wakaulizwa kisiri kinachoendelea ndipo wakamsimulia maisha ya Jackie shuleni na yalikuwa yanasikitisha kwa wazazi , na pia Julius alitajwa sana , kwa sababu julius alikuwa mwoga baada ya kuchapwa vibao na baba yake naye akamsimulia jinsi alivyotumwa na hatimaye wale vijana waliokuwa wanamlipa julius wakaitwa nao wakapewa makofi Kama mawili hivi kila mtu alikuwa anashusha story Kama ilivyokuwa.

 

3. Baadae na wazazi wa wale vijana waliomtuma julius waliitwa nao pia na adhabu ya suspension ilitolewa kwa wote wanafunzi isipokuwa Julius na Jackie walifukuzwa shule kabisa , lengo lilikuwa ni kuwatenganisha, basi wazazi wakaamua kuwatafutia shule nyingine,kwa sababu ela kwao na Jackie zilikuwepo baba yake akampleka Ukraine kusoma ila julius Akabaki nchini, kwa sababu Jackie aliona kuwa amechezea Sana mda aliamua kusoma na kuwa mwanafunzi Bora darasani na pia julius alisoma na akaamua kiuacha mchezo.

 

4. Baada ya masomo yao ya kidato cha sita Jackie aliendelea kusoma udaktari Ukraine na Juliusi alisoma uinginia ,Basi kila mtu kwa anga zake wakasoma kila mtu akapata kazi, ILa mana yake na Jackie alimchukia mno Julius kwa sababu ndiye aliyekuwa chanzo cha kuleta Fujo kwenye maisha ya mwanae, kwa hiyo Jackie akakabidhiwa kuwa daktari mkuu wa hospital na akawa anafanya kazi zake vizuri na kwa umakini na Julius akawa engineering mzuri Sana.

 

5. Na siku Moja Jackie alipewa ela za kujenga hospital yenye viwango na selikali na akapewa engineer mkuu wa selikali aliyeitwa engineer julius kusudi waje wapange kuhusu ujenzi wa hospital na wakapeana simu yaani engineer na daktari ila walikuwa hawajuani ila waliongea kwenye simu na kupanga siku ya kukutana kwa ajili ya kupanga jinsi ya kujenga hospital na siku ikafika.

itaendelea baadae

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF Views 1468

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)

Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa.

Soma Zaidi...
Chemsha bongo na bongoclass

Jipime uwezo wako wa kufikiri pamoja nasi.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)

Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mtihani unafika ila Jackie hakujiandaa alishutuliwa na marafiki zake baada ya kuona mwenendo wake haueleweki.

Soma Zaidi...
Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.

Soma Zaidi...