Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme


image


Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza ili waje watoe siri siku ya kuapishwa kwa mfalme.


Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya tatu).

1. Kama tulivyomalizia kwenye sehemu ya pili pale mama wa kijana wa kiume wa mfalme alitaka kumuua binti na bibi ili kupoteza ushahidi ila kijana huyo wa mfalme aliwahi akawaokoa na kumwona kipenzi cha moyo wake na kumchukua nyumbani kama mke wake ila mama hakukubaliana naye ila mfalme kwa kuwa alikuwa anampenda kijana wake akisikiliza kila kitu alichotaka na akaamua kufanya sherehe kubwa na ya kifahari.

 

2 . Na yule bibi kwa kuwa alipenda sana umaarufu na maisha mazuri alijisalimisha kwa wake wenza na akatoa siri zote za yule mke mdogo wa mfalme, wale wake wenza walifurahi sana kusikia habari hiyo na wakapata sehemu ya kumwaibisha adui yao kwa sababu yule mke mdogo wa mfalme alikuwa ni kama kizuizi kwao na mfalme, basi wakapanga njama na kutunza siri ili siku ya kumwapisha mfalme siri itobolewe na kujana wa kiume wa mfalme hasiweze kupata ufalme.

 

3. Katika wakati ule palikuwepo na sheria moja kwamba ili mtu aje kuwa mfalme ni lazima awe ameoa kwenye ukoo ambao hawana undugu hata kidogo ili kuepuka hali ya ufalme kugawanyika kwa hiyo walitaka ufalme ubaki ndani, au kama  kwenye familia ya kifalme hakuna mtoto wa kiume wa kurithi ufalme au yupo ila hana sifa za kuwa mfalme mtoto wa kike anaweza kuwa malkia ila mme wake atoke sehemu tofauti na ile sehemu na hasiweze na undugu wowote na familia ya kifalme iwe kati ya ndugu wa wake wenza yaani pasiwepo na undugu hata chembe.

 

4. Katika maandalizi yote hayo mama wa kijana wa kiume wa mfalme aliona kwamba mwanae hawezi kupata ufalme kwa sababu aliona bibi yupo pale akiwa na ushahidi wote na yuko kati ya maadui zake akapata shida sana akawaza mpaka akakonda , kwa kuwa bibi alikuwa mnafiki na mpenda sifa aliamua kumwita yule mke wa mfalme kwa siri akamwambia kuwa kwamba kwa sasa mwanao hawezi kupata ufalme sasa cha kufanya ni kuhakikisha kuwa tunafanya mbinu ili kijana aweze kuachana na yule binti .

 

5. Kwa kuwa yule Mke wa mfalme alikuwa kwenye hali ngumu akamuuliza bibi tufanye je? Bibi akasema nitakwambia cha kufanya baada ya siku chache, kisha bibi akaenda kwa yule mke wa kwanza wa mfalme akasema andaa binti yako ili yule kijana wa kiume wa mfalme hasipopata ufalme huyu atakuwa malkia. Baadae siku mbili zinafika bibi akaenda kuonana na mke mdogo wa mfalme kwa ajili ya maongezi.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Hadithi iliyosimuliwa na kijakazi wa sultani
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Hati.a ya kijana mchonganishi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image NIMLAUMU NANI (sehemu ya sita)
Post inahusu zaidi hadithi ya NIMLAUMU NANI ambayo ni sehemu ya sita, katika kipengele hiki tunaenda kumwona msichana Amina anapambana na hatimaye anafunga ndoa ya kiserikali na Frank Soma Zaidi...

image USALITI (sehemu ya tatu)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi. Soma Zaidi...

image Hadithi ya chongo watatu wa mfalme na wanawake wa Baghdad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu. Soma Zaidi...

image Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi. Soma Zaidi...

image Hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali Soma Zaidi...

image Hadithi ya Kaka wa pili wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...