picha

Umuhimu wa kunyonyesha mtoto

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kunyonyesha mtoto, kunyonyesha ni kitendo cha Mama kutumia titi lake Ili kuweza kumpatia mtoto lishe kwa kipindi chote ambacho Mama upaswa kutumia kwa kunyonyesha mtoto wake kwa hiyo Kuna faida ambazo mama uzipata kutoka

Umuhimu wa kunyonyesha mtoto.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kuelewa kuwa Mama pindi anapojifungua anapaswa kunyonyesha mtoto wake ndani ya saa Moja kwa hiyo Kuna faida kubwa kwa Mama na kwa mtoto pia, vile vile ni vizuri kabisa Mama kunyonyesha mtoto wake kwa kipindi cha miezi sita bila kumpatia chakula chochote kile hali hii usababisha kumkinga mtoto dhidi ya magonjwa kwa sababu kwenye kinywa cha mtoto Kuna ngozi ya juu ambayo uzuia magonjwa mbalimbali. Kwa hiyo Mama akimpatia mtoto chakula wakati wa miezi ya kwanza usababisha ngozi hiyo kutoka na mtoto ni rahisi kupata maambukizi ya kinywa.

 

2.Hasa hasa kwa akina Mama wenye maambukizi wanapaswa kujitahidi sana wakati wa kunyonyesha mtoto akiwa chini ya miezi sita kutomchanganyizia mtoto chakula chochote kwa kuepuka maambukizi pale ambapo ngozi ya juu imetoka, kwa hiyo hata Kama Mama ni mfanyakazi anapaswa kutenga mda Ili kunyonyesha mtoto maziwa tu mpaka atakapofikisha umri zaidi ya miezi sita na hapo hiyo ngozi kwenye ulimi inakuwa tayari imekomaa na mtoto anaweza kupewa chakula kiraini.

 

3. Kwa upande wa wafanyakazi ambao hawawezi kushindwa na watoto wao wakati wa mchana isipokuwa asubuhi, jioni na usiku ni vizuri kukamua maziwa kabla ya kwenda kazini na kiwaachia wanaomtunza mtoto Ili wampatie kwa siku nzima na kitendo cha kukamua maziwa kina hitaji utaamu Ili kuweza kuwa kwenye hali ya usafi na kuepukana na magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kwenye ukamuaji wa maziwa, Kuna wengine wanaotumia mashine maalumu kwa ajili ya kazi hiyo.

 

4. Kwa akina Mama ambao Hawanyonyeshi kabisa ni kwa sababu pengine ya matatizo ya ki afya au kutokuwepo kwa maziwa kwa baadhi ya akina Mama Kuna maziwa ambayo yanaitwa lactose Yanafanana na maziwa ya Mama Yako madukani na yanaweza kutumiwa na mtoto ambaye Mama yake Hana maziwa au hanyonyeshi kwa sababu za ki afya.

 

5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kiwanyonyesha watoto wao kwa kufanya hivyo wanasaidia kuwepo kwa uhusiano kati ya Mama na mtoto na kuwakinga dhidi ya magonjwa na kuwapatia virutubisho muhimu ambavyo usaidia kwenye kukua kutoka hatua Moja kwenda nyingine

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2090

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 ai web app     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Maandalizi ya mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia.

Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.

Soma Zaidi...
Habar doctor mm nahc kuwa ni mjamzito tumbo la chin ya kitovu linaniuma muda mwingine linaacha chuchu zinawasha na cku niliyokutana na mume wangu ni cku 11

Kuna uwezekano una ujauzito ila hujajijuwa, huwenda hujapata dalili zozote. Unataka kujuwa kama una ujauzito baada ya tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa wanawake.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kufunga kizazi kwa wanawake.

Soma Zaidi...
Ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango.

Posti hii inahusu zaidi ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango, sio kwa imani potofu ambazo Watu utumia kuelezea uzazi wa mpango.

Soma Zaidi...
Vitu vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid (majimaji yanayomzungruka mtoto aliyekuwepo tumboni wakati wa ujauzito)

Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.

Soma Zaidi...
Sababu za kutangulia kwa kitovu wakati Mtoto anazaliwa

Posti hii inahusu zaidi sababu za kutangulia kwa kitovu wakati wa mtoto anapozaliwa.

Soma Zaidi...