Umuhimu wa kunyonyesha mtoto
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kunyonyesha mtoto, kunyonyesha ni kitendo cha Mama kutumia titi lake Ili kuweza kumpatia mtoto lishe kwa kipindi chote ambacho Mama upaswa kutumia kwa kunyonyesha mtoto wake kwa hiyo Kuna faida ambazo mama uzipata kutoka
Umuhimu wa kunyonyesha mtoto.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kuelewa kuwa Mama pindi anapojifungua anapaswa kunyonyesha mtoto wake ndani ya saa Moja kwa hiyo Kuna faida kubwa kwa Mama na kwa mtoto pia, vile vile ni vizuri kabisa Mama kunyonyesha mtoto wake kwa kipindi cha miezi sita bila kumpatia chakula chochote kile hali hii usababisha kumkinga mtoto dhidi ya magonjwa kwa sababu kwenye kinywa cha mtoto Kuna ngozi ya juu ambayo uzuia magonjwa mbalimbali. Kwa hiyo Mama akimpatia mtoto chakula wakati wa miezi ya kwanza usababisha ngozi hiyo kutoka na mtoto ni rahisi kupata maambukizi ya kinywa.
2.Hasa hasa kwa akina Mama wenye maambukizi wanapaswa kujitahidi sana wakati wa kunyonyesha mtoto akiwa chini ya miezi sita kutomchanganyizia mtoto chakula chochote kwa kuepuka maambukizi pale ambapo ngozi ya juu imetoka, kwa hiyo hata Kama Mama ni mfanyakazi anapaswa kutenga mda Ili kunyonyesha mtoto maziwa tu mpaka atakapofikisha umri zaidi ya miezi sita na hapo hiyo ngozi kwenye ulimi inakuwa tayari imekomaa na mtoto anaweza kupewa chakula kiraini.
3. Kwa upande wa wafanyakazi ambao hawawezi kushindwa na watoto wao wakati wa mchana isipokuwa asubuhi, jioni na usiku ni vizuri kukamua maziwa kabla ya kwenda kazini na kiwaachia wanaomtunza mtoto Ili wampatie kwa siku nzima na kitendo cha kukamua maziwa kina hitaji utaamu Ili kuweza kuwa kwenye hali ya usafi na kuepukana na magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kwenye ukamuaji wa maziwa, Kuna wengine wanaotumia mashine maalumu kwa ajili ya kazi hiyo.
4. Kwa akina Mama ambao Hawanyonyeshi kabisa ni kwa sababu pengine ya matatizo ya ki afya au kutokuwepo kwa maziwa kwa baadhi ya akina Mama Kuna maziwa ambayo yanaitwa lactose Yanafanana na maziwa ya Mama Yako madukani na yanaweza kutumiwa na mtoto ambaye Mama yake Hana maziwa au hanyonyeshi kwa sababu za ki afya.
5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kiwanyonyesha watoto wao kwa kufanya hivyo wanasaidia kuwepo kwa uhusiano kati ya Mama na mtoto na kuwakinga dhidi ya magonjwa na kuwapatia virutubisho muhimu ambavyo usaidia kwenye kukua kutoka hatua Moja kwenda nyingine
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Dalili za tezi dume.
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Soma Zaidi...Mambo muhimu kuhusu mbegu za kiume
Post hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo tunapaswa kujua au kufahamu kuhusu mbegu za kiume, kwa kuwa mbegu za kiume usaidia katika utungaji wa mimba kwa hiyo ni vizuri kabisa kuzitunza Ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa s
Soma Zaidi...Mabadiliko ya ngozi wakati wa ujauzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye ngozi wakati wa ujauzito, ni mabadiliko yanayotokea kwenye ngozi ya Mama wakati wa ujauzito.
Soma Zaidi...Mimba huonekana katka mkojo baada ya muda gan tangu itungwe
Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.
Soma Zaidi...Dalili za ujauzito: Nini kinatokea kwanza
Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.
Soma Zaidi...