picha

Umuhimu wa kunyonyesha mtoto

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kunyonyesha mtoto, kunyonyesha ni kitendo cha Mama kutumia titi lake Ili kuweza kumpatia mtoto lishe kwa kipindi chote ambacho Mama upaswa kutumia kwa kunyonyesha mtoto wake kwa hiyo Kuna faida ambazo mama uzipata kutoka

Umuhimu wa kunyonyesha mtoto.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kuelewa kuwa Mama pindi anapojifungua anapaswa kunyonyesha mtoto wake ndani ya saa Moja kwa hiyo Kuna faida kubwa kwa Mama na kwa mtoto pia, vile vile ni vizuri kabisa Mama kunyonyesha mtoto wake kwa kipindi cha miezi sita bila kumpatia chakula chochote kile hali hii usababisha kumkinga mtoto dhidi ya magonjwa kwa sababu kwenye kinywa cha mtoto Kuna ngozi ya juu ambayo uzuia magonjwa mbalimbali. Kwa hiyo Mama akimpatia mtoto chakula wakati wa miezi ya kwanza usababisha ngozi hiyo kutoka na mtoto ni rahisi kupata maambukizi ya kinywa.

 

2.Hasa hasa kwa akina Mama wenye maambukizi wanapaswa kujitahidi sana wakati wa kunyonyesha mtoto akiwa chini ya miezi sita kutomchanganyizia mtoto chakula chochote kwa kuepuka maambukizi pale ambapo ngozi ya juu imetoka, kwa hiyo hata Kama Mama ni mfanyakazi anapaswa kutenga mda Ili kunyonyesha mtoto maziwa tu mpaka atakapofikisha umri zaidi ya miezi sita na hapo hiyo ngozi kwenye ulimi inakuwa tayari imekomaa na mtoto anaweza kupewa chakula kiraini.

 

3. Kwa upande wa wafanyakazi ambao hawawezi kushindwa na watoto wao wakati wa mchana isipokuwa asubuhi, jioni na usiku ni vizuri kukamua maziwa kabla ya kwenda kazini na kiwaachia wanaomtunza mtoto Ili wampatie kwa siku nzima na kitendo cha kukamua maziwa kina hitaji utaamu Ili kuweza kuwa kwenye hali ya usafi na kuepukana na magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kwenye ukamuaji wa maziwa, Kuna wengine wanaotumia mashine maalumu kwa ajili ya kazi hiyo.

 

4. Kwa akina Mama ambao Hawanyonyeshi kabisa ni kwa sababu pengine ya matatizo ya ki afya au kutokuwepo kwa maziwa kwa baadhi ya akina Mama Kuna maziwa ambayo yanaitwa lactose Yanafanana na maziwa ya Mama Yako madukani na yanaweza kutumiwa na mtoto ambaye Mama yake Hana maziwa au hanyonyeshi kwa sababu za ki afya.

 

5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kiwanyonyesha watoto wao kwa kufanya hivyo wanasaidia kuwepo kwa uhusiano kati ya Mama na mtoto na kuwakinga dhidi ya magonjwa na kuwapatia virutubisho muhimu ambavyo usaidia kwenye kukua kutoka hatua Moja kwenda nyingine

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2072

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 ai web app     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Dalili za Mimba ya Wiki 2 Unazopaswa Kujua

Katika ulimwengu wa kitabibu, ujauzito huanza kuhesabiwa kuanzia siku ya kwanza ya hedhi yako ya mwisho. Hivyo, katika "wiki ya pili," mwili wako kimsingi unajiandaa kwa ajili ya utungisho (ovulation). Ingawa kitaalamu bado hujaacha hedhi au kupata mimba kamili, huu ndio wakati muhimu ambapo mayai yanastawi na maandalizi ya homoni huanza. Makala hii inaelezea kile kinachotokea mwilini mwako katika hatua hii ya awali.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Soma Zaidi...
Siku za kupata ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata ujauzito

Soma Zaidi...
Kaka nasumbuliwa saan na tatizo la kuwasha kwenye kichwa Cha uume Sijui nifanyaje

Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni?

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza joto la mtoto mara tu baada ya kuzaliwa.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha i

Soma Zaidi...