Menu



Mawakala wa maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mawakala wa maradhi

MAWAKALA WA MARADHI (PAHOGEN)

Hawa tumesema ndio mawakala wakubwa wa kuambukiza maradhi. Hawa husababisha maradhi haya ya kuambukiza. Wapo aina nyingi lakini tunaweza kuwagawanya katika bakteria, virus, fungi, protozoa na parasites.

 

1.Bakteria

Hawa ni vijidudu vidogo sana ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho maavu bila ya kutumia hadubini (microscope). Vidudu hivi vina seli moja tu. Wapo bakteria ambao hawasababishi maradhi na wapo a,mbao husababisha maradhi. Bakteria karibia dunia nzima wamejaa na hata sehemu ambazo zana mabarafu bakteria pia wapo. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa kuna aina zisizopungua 300 za bakteria ambao wanaishi kwenye mdomo wa binadamu. Ila karibia bakteria hawa wote hawana madhara kwetu kwa upande mwengine wengi wao ni msaada na ni faida kwetu.

 

Mfano mzuri ni kuwa kwenye utumbo mdogo kuna bakteria ambao wanatengeneza vitamini ambavyo ni msaada kwa afya zetu. Pia ijulikane bakteria wengine wana madhara makubwa wakiwa ndani ya miili yetu kwa mfano baktria aina ya tuberculosis hawa husababisha kifua kikuu. Tetanus hawa huleta tetenasi. 2.VIRUSI

Virusi ni vidogo zaidi kuliko hata bakteria. Virusi ni vijidudu vidogo sana ambavyo vyenyewe vina genetic material na protein coat. Genetic material ni chembechembe zinazowafanya waweze kuzaliana. Virusi vinaweza kushi tu kama vipo ndani ya kiumbe hai. Vyenyewe vinaweza kuzaliana kwa kutumia seli za kiumbe hai ambapowamo. Maradhi ya Ukimwi, mafua ni baadhi tu ya maradhi ya virusi.

 

3.FUNGI

Hawa huwa tumezoea kuwaita fangasi hawa wanakula kwenye seli za kiumbe hai. Mfano mzuri ni uyoga huu ni katika jamii ya viumbe hawa wanaokula kutokana na seli au kiumbe kilichokufa. Kama bakteria hata wadudu hawa wapo wanasababisha maradhi na wengine hawasababishi. Fangasi wa miguuni ni mfano mzuri wa maradhi ya wasudu hawa. Mfano mwengine ni wale wa sehemu za siri wanaopelekea kuchubua kwa koreodani kwa wanaume na madahra menginey wa wanawake.

 

4.PROTOZOA

Hawa pia ni vijidudu vidogo visivyoonekana kwa macho makavu. Hawa pia wana seli moja tu katika miili yao. Ila hawa ni wakubwa kuliko bakteia. Hawa wanasababishwa magonjwa ambayo yanaongoza kuuwa watu wengi sana dunianii. Kwa mfano malaria husababishwa na vijidudu hivi. Kwaribia watu milioni moja kila mwaka wanakufa kwa malaria katika nchi zilizopo kwenye uoto wa tropic.

 

5.PARASIT

5.Hawa ni wadudu wanaokula kiumbe hai. Mfano mzuri ni chawa, kupe, mbu na wengineo wenye mfano huu. Wadudu hawa wanajipatia chakula kwa kunyonyo viinilishe kwenye mwili wa kiumbe hai. Hawa wanaweza kuwa nche ya mwili kama chawa au ndani ya mwili kama minyoo.

 

NJIA AMBAZO MARADHI HUAMBUKIZWA

1.kutoka mtu kwenda mtu mwingine. Hii ni njia nzuri ya kuambukiza maradhi kutoka mgonjwa kwenda mzima, ama kutoka mtu kwenda mtu. Inaweza kuwa kwa njia ya hewa kama mafua pindi mgonjwa anapopiga chafya, au kifua kikuu pindi mgonjwa napokohoa. Pindi mgonjwa akikohoa au chafya anatowa mamilioni ya wadudu ambao wanabakia hewani kwa muda. Na ikitokea mtu ameivuta hewa ile anaweza kuambukizwa.

 

Kupitia kugusa maradhi yanaweza kutoka mtu hadi mtu, kwa mfano kitambaa alichotumia mtu mwenye mafua au kifuua kikuu na wewe ukashika unaweza kuwabeba wadudu wale na wakaingia kwako. Pia maradhi kama kipindupindu, homa ya mafua a ndege na ebila huweza kuambukizwa kwa kugusana.

 

Wakati mwingine kupitia kumkisi mgonjwa unaweza kupata maradhi kwa mfano homa ya ini inaweza kuambukizwa kwa kukisi kupitia mate. Pia kupitia vyombo kama kijiko au kikombe cha kunywea maji kama mgonjwa ametumia na wewe ukatumia palelpale kuweka mdomo wako.

 

2.kupitia vyakula tumeshaona mifano yake kwenye kurasa zilizopita.

3.Mazigura pia tumeona kurasa za juu

4.Wanyama kwa mfano mbwa kusababisha tetenasi na panya kusababisha ugonjwa wa taun. Hawa wanyama wanakuwa wanabeba pathogen wa maradhi hawa.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 1029

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA

Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte.

Soma Zaidi...
Aina za kuungua

Post hii inahusu Aina za kuungua, kuungua ni Hali ya kubabuka kwa ngozi ya mwili na kusababisha madhara mbalimbali

Soma Zaidi...
Njia za kuingiza chanjo mwilini

Posti hii inahusu njia mbalimbali ambazo utumika kupitisha chanjo, njia hizo utegemea na kazi ya chanjo kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPANDWA NA PRESHA

Presha ya kupanda hutokea pale kipimo kinaposoma zaidi ya 120/80mm Hg.

Soma Zaidi...
huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni

Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara

Soma Zaidi...
Je unaweza ukapona macho kama huoni vizuri kwa sababu ya vitamini A,

Jiamini A ni katika vitamini inayojulikana sana kuboresha na kuimarisha afya vya macho na uoni. Tafiti zinaonyesha kuwa kuna kundi kubwa la watoto wanaopata tayizobla kutokuona kutokana na ukosefu wa vitamini A vya kutosha.

Soma Zaidi...
Zijue kazi za uke (vagina)

Uke ni sehemu ambayo imo ndani ya mwili wa mwanamke, sehemu hii ufanya kazi mbalimbali hasa wakati wa kujamiiana, kubarehe na kujifungua kwa mama.

Soma Zaidi...
Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure

Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu.

Posti hii inahusu zaidi mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu, tunajua kubwa kifua kikuu ni Ugonjwa ambao utumia mda mrefu kidogo katika matibabu kwa hiyo mgawanyiko wake uko kwenye sehemu mbili muhimu kama tutajavyoona

Soma Zaidi...
Ijue rangi za mkojo na maana zake katika mwili kuhsu afya yako

Posti hii inahusu zaidi rangi za mkojo na maana zake, hizi ni rangi ambazo uweza kutokea kwenye mkojo wa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa, chakula,na mtindo wa maisha inawezekana unywaji wa maji au kutokunywa maji.

Soma Zaidi...