Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mawakala wa maradhi
MAWAKALA WA MARADHI (PAHOGEN)
Hawa tumesema ndio mawakala wakubwa wa kuambukiza maradhi. Hawa husababisha maradhi haya ya kuambukiza. Wapo aina nyingi lakini tunaweza kuwagawanya katika bakteria, virus, fungi, protozoa na parasites.
1.Bakteria
Hawa ni vijidudu vidogo sana ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho maavu bila ya kutumia hadubini (microscope). Vidudu hivi vina seli moja tu. Wapo bakteria ambao hawasababishi maradhi na wapo a,mbao husababisha maradhi. Bakteria karibia dunia nzima wamejaa na hata sehemu ambazo zana mabarafu bakteria pia wapo. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa kuna aina zisizopungua 300 za bakteria ambao wanaishi kwenye mdomo wa binadamu. Ila karibia bakteria hawa wote hawana madhara kwetu kwa upande mwengine wengi wao ni msaada na ni faida kwetu.
Mfano mzuri ni kuwa kwenye utumbo mdogo kuna bakteria ambao wanatengeneza vitamini ambavyo ni msaada kwa afya zetu. Pia ijulikane bakteria wengine wana madhara makubwa wakiwa ndani ya miili yetu kwa mfano baktria aina ya tuberculosis hawa husababisha kifua kikuu. Tetanus hawa huleta tetenasi. 2.VIRUSI
Virusi ni vidogo zaidi kuliko hata bakteria. Virusi ni vijidudu vidogo sana ambavyo vyenyewe vina genetic material na protein coat. Genetic material ni chembechembe zinazowafanya waweze kuzaliana. Virusi vinaweza kushi tu kama vipo ndani ya kiumbe hai. Vyenyewe vinaweza kuzaliana kwa kutumia seli za kiumbe hai ambapowamo. Maradhi ya Ukimwi, mafua ni baadhi tu ya maradhi ya virusi.
3.FUNGI
Hawa huwa tumezoea kuwaita fangasi hawa wanakula kwenye seli za kiumbe hai. Mfano mzuri ni uyoga huu ni katika jamii ya viumbe hawa wanaokula kutokana na seli au kiumbe kilichokufa. Kama bakteria hata wadudu hawa wapo wanasababisha maradhi na wengine hawasababishi. Fangasi wa miguuni ni mfano mzuri wa maradhi ya wasudu hawa. Mfano mwengine ni wale wa sehemu za siri wanaopelekea kuchubua kwa koreodani kwa wanaume na madahra menginey wa wanawake.
4.PROTOZOA
Hawa pia ni vijidudu vidogo visivyoonekana kwa macho makavu. Hawa pia wana seli moja tu katika miili yao. Ila hawa ni wakubwa kuliko bakteia. Hawa wanasababishwa magonjwa ambayo yanaongoza kuuwa watu wengi sana dunianii. Kwa mfano malaria husababishwa na vijidudu hivi. Kwaribia watu milioni moja kila mwaka wanakufa kwa malaria katika nchi zilizopo kwenye uoto wa tropic.
5.PARASIT
5.Hawa ni wadudu wanaokula kiumbe hai. Mfano mzuri ni chawa, kupe, mbu na wengineo wenye mfano huu. Wadudu hawa wanajipatia chakula kwa kunyonyo viinilishe kwenye mwili wa kiumbe hai. Hawa wanaweza kuwa nche ya mwili kama chawa au ndani ya mwili kama minyoo.
NJIA AMBAZO MARADHI HUAMBUKIZWA
1.kutoka mtu kwenda mtu mwingine. Hii ni njia nzuri ya kuambukiza maradhi kutoka mgonjwa kwenda mzima, ama kutoka mtu kwenda mtu. Inaweza kuwa kwa njia ya hewa kama mafua pindi mgonjwa anapopiga chafya, au kifua kikuu pindi mgonjwa napokohoa. Pindi mgonjwa akikohoa au chafya anatowa mamilioni ya wadudu ambao wanabakia hewani kwa muda. Na ikitokea mtu ameivuta hewa ile anaweza kuambukizwa.
Kupitia kugusa maradhi yanaweza kutoka mtu hadi mtu, kwa mfano kitambaa alichotumia mtu mwenye mafua au kifuua kikuu na wewe ukashika unaweza kuwabeba wadudu wale na wakaingia kwako. Pia maradhi kama kipindupindu, homa ya mafua a ndege na ebila huweza kuambukizwa kwa kugusana.
Wakati mwingine kupitia kumkisi mgonjwa unaweza kupata maradhi kwa mfano homa ya ini inaweza kuambukizwa kwa kukisi kupitia mate. Pia kupitia vyombo kama kijiko au kikombe cha kunywea maji kama mgonjwa ametumia na wewe ukatumia palelpale kuweka mdomo wako.
2.kupitia vyakula tumeshaona mifano yake kwenye kurasa zilizopita.
3.Mazigura pia tumeona kurasa za juu
4.Wanyama kwa mfano mbwa kusababisha tetenasi na panya kusababisha ugonjwa wa taun. Hawa wanyama wanakuwa wanabeba pathogen wa maradhi hawa.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wazee
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Aina ya choo kisichokuwa cha kawaida, ni dalili za choo ambacho siyo Cha kawaida, Ina maana ukiona dalili za choo Cha Aina hii ni vizuri kwenda hospitalini Ili kupata matibabu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria kwa kitaalamu huitwa vibrio cholera.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Endapo U.T.I inajirudiarudia baada yavkutibiwa inawezabkuwa ikakupa mawazo mengi. Katika post hii nitakufafanulia nini ufanye.
Soma Zaidi...Natak kufaham kuwa binadam akiwa mweupe mikononi atakuwa na upungufu wa vitamin gani?
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mabadiliko katika umri wa kubarehe kwa wsichana, ni kipindi ambacho watoto huelekea ujana, utokea Kati ya miaka kuanzia Kumi na kuendelea.
Soma Zaidi...Kushambuliwa kwa moyo na kupumua ni kitendo Cha moyo kusimama ghafla, Hali hii unapaswa kutolewa huduma ya kwanza Ili moyo ufanye kazi tena,
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa kawaida ili mtu aweze kuwa na uzito wa kawaida ni vizuri na kiafya kupima urefu ukilinganisha na uzito wa mtu.
Soma Zaidi...Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.
Soma Zaidi...