Mawakala wa maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mawakala wa maradhi

MAWAKALA WA MARADHI (PAHOGEN)

Hawa tumesema ndio mawakala wakubwa wa kuambukiza maradhi. Hawa husababisha maradhi haya ya kuambukiza. Wapo aina nyingi lakini tunaweza kuwagawanya katika bakteria, virus, fungi, protozoa na parasites.

 

1.Bakteria

Hawa ni vijidudu vidogo sana ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho maavu bila ya kutumia hadubini (microscope). Vidudu hivi vina seli moja tu. Wapo bakteria ambao hawasababishi maradhi na wapo a,mbao husababisha maradhi. Bakteria karibia dunia nzima wamejaa na hata sehemu ambazo zana mabarafu bakteria pia wapo. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa kuna aina zisizopungua 300 za bakteria ambao wanaishi kwenye mdomo wa binadamu. Ila karibia bakteria hawa wote hawana madhara kwetu kwa upande mwengine wengi wao ni msaada na ni faida kwetu.

 

Mfano mzuri ni kuwa kwenye utumbo mdogo kuna bakteria ambao wanatengeneza vitamini ambavyo ni msaada kwa afya zetu. Pia ijulikane bakteria wengine wana madhara makubwa wakiwa ndani ya miili yetu kwa mfano baktria aina ya tuberculosis hawa husababisha kifua kikuu. Tetanus hawa huleta tetenasi. 2.VIRUSI

Virusi ni vidogo zaidi kuliko hata bakteria. Virusi ni vijidudu vidogo sana ambavyo vyenyewe vina genetic material na protein coat. Genetic material ni chembechembe zinazowafanya waweze kuzaliana. Virusi vinaweza kushi tu kama vipo ndani ya kiumbe hai. Vyenyewe vinaweza kuzaliana kwa kutumia seli za kiumbe hai ambapowamo. Maradhi ya Ukimwi, mafua ni baadhi tu ya maradhi ya virusi.

 

3.FUNGI

Hawa huwa tumezoea kuwaita fangasi hawa wanakula kwenye seli za kiumbe hai. Mfano mzuri ni uyoga huu ni katika jamii ya viumbe hawa wanaokula kutokana na seli au kiumbe kilichokufa. Kama bakteria hata wadudu hawa wapo wanasababisha maradhi na wengine hawasababishi. Fangasi wa miguuni ni mfano mzuri wa maradhi ya wasudu hawa. Mfano mwengine ni wale wa sehemu za siri wanaopelekea kuchubua kwa koreodani kwa wanaume na madahra menginey wa wanawake.

 

4.PROTOZOA

Hawa pia ni vijidudu vidogo visivyoonekana kwa macho makavu. Hawa pia wana seli moja tu katika miili yao. Ila hawa ni wakubwa kuliko bakteia. Hawa wanasababishwa magonjwa ambayo yanaongoza kuuwa watu wengi sana dunianii. Kwa mfano malaria husababishwa na vijidudu hivi. Kwaribia watu milioni moja kila mwaka wanakufa kwa malaria katika nchi zilizopo kwenye uoto wa tropic.

 

5.PARASIT

5.Hawa ni wadudu wanaokula kiumbe hai. Mfano mzuri ni chawa, kupe, mbu na wengineo wenye mfano huu. Wadudu hawa wanajipatia chakula kwa kunyonyo viinilishe kwenye mwili wa kiumbe hai. Hawa wanaweza kuwa nche ya mwili kama chawa au ndani ya mwili kama minyoo.

 

NJIA AMBAZO MARADHI HUAMBUKIZWA

1.kutoka mtu kwenda mtu mwingine. Hii ni njia nzuri ya kuambukiza maradhi kutoka mgonjwa kwenda mzima, ama kutoka mtu kwenda mtu. Inaweza kuwa kwa njia ya hewa kama mafua pindi mgonjwa anapopiga chafya, au kifua kikuu pindi mgonjwa napokohoa. Pindi mgonjwa akikohoa au chafya anatowa mamilioni ya wadudu ambao wanabakia hewani kwa muda. Na ikitokea mtu ameivuta hewa ile anaweza kuambukizwa.

 

Kupitia kugusa maradhi yanaweza kutoka mtu hadi mtu, kwa mfano kitambaa alichotumia mtu mwenye mafua au kifuua kikuu na wewe ukashika unaweza kuwabeba wadudu wale na wakaingia kwako. Pia maradhi kama kipindupindu, homa ya mafua a ndege na ebila huweza kuambukizwa kwa kugusana.

 

Wakati mwingine kupitia kumkisi mgonjwa unaweza kupata maradhi kwa mfano homa ya ini inaweza kuambukizwa kwa kukisi kupitia mate. Pia kupitia vyombo kama kijiko au kikombe cha kunywea maji kama mgonjwa ametumia na wewe ukatumia palelpale kuweka mdomo wako.

 

2.kupitia vyakula tumeshaona mifano yake kwenye kurasa zilizopita.

3.Mazigura pia tumeona kurasa za juu

4.Wanyama kwa mfano mbwa kusababisha tetenasi na panya kusababisha ugonjwa wa taun. Hawa wanyama wanakuwa wanabeba pathogen wa maradhi hawa.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-10-30     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 771

Post zifazofanana:-

Faida za mbegu za maboga
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za mbegu za maboga Soma Zaidi...

Tatizo la kutanuka kwa tezi dume.
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutanuka kwa tezi dume, ni tatizo ambalo linawakumba wanaume wengi kwa wakati huu kwa sababu ya kuwepo kwa maaambukizi kwenye tezi ambayo Usababishwa na vitu mbalimbali kama tulivyoona. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa ukoma ni Ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayejulika kama mycobacterium leprae. Soma Zaidi...

Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Binti huyu Ni Nani?
Posti hii inakwenda kukuendelezea hadithi kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.
Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa ngiri
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo mgonjwa wa ngiri anaweza kuzipata, kwa hiyo baada ya kusoma na kuelewa dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospitali mapema kwa ajili ya kupata matibabu. Soma Zaidi...

Mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili pamoja na mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua kwa Wanaume Soma Zaidi...

Yajue matatizo yanayosababisha Ugonjwa wa akili.
Madhara ya ugonjwa wa akili yanaweza kuwa ya muda au ya kudumu. Unaweza pia kuwa na zaidi ya ugonjwa mmoja wa afya ya akili kwa wakati mmoja. Kwa mfano, unaweza kuwa na ulegevu na ugonjwa wa matumizi ya madawa ya kulevya. Soma Zaidi...

Vipi kuhusu kibofu kukaza sana na unapokula unahisi kama tumbo kujaa zaidi je hii nidall yamimba?
Dalili za mimba zinaweza kuwa tata sana kuzijua mpaka upate vipimo. Kwa mfano unaweza kupatwa na maumivu yakibofu. Je unadhani nayo ni dalili ya mimba? Soma Zaidi...

Kwanini mwanadamu hawezi kuunda dini sahihi
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Dalili za macho kuwa makavu
posti hii inaelezea kuhusiana na dalilili na Mambo ya hatari ya Macho makavu  hutokea wakati machozi yako hayawezi kutoa unyevu wa kutosha kwa macho yako. Machozi yanaweza kuwa duni kwa sababu nyingi. Kwa mfano, Macho makavu  yanaweza ku Soma Zaidi...