image

Mawakala wa maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mawakala wa maradhi

MAWAKALA WA MARADHI (PAHOGEN)

Hawa tumesema ndio mawakala wakubwa wa kuambukiza maradhi. Hawa husababisha maradhi haya ya kuambukiza. Wapo aina nyingi lakini tunaweza kuwagawanya katika bakteria, virus, fungi, protozoa na parasites.

 

1.Bakteria

Hawa ni vijidudu vidogo sana ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho maavu bila ya kutumia hadubini (microscope). Vidudu hivi vina seli moja tu. Wapo bakteria ambao hawasababishi maradhi na wapo a,mbao husababisha maradhi. Bakteria karibia dunia nzima wamejaa na hata sehemu ambazo zana mabarafu bakteria pia wapo. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa kuna aina zisizopungua 300 za bakteria ambao wanaishi kwenye mdomo wa binadamu. Ila karibia bakteria hawa wote hawana madhara kwetu kwa upande mwengine wengi wao ni msaada na ni faida kwetu.

 

Mfano mzuri ni kuwa kwenye utumbo mdogo kuna bakteria ambao wanatengeneza vitamini ambavyo ni msaada kwa afya zetu. Pia ijulikane bakteria wengine wana madhara makubwa wakiwa ndani ya miili yetu kwa mfano baktria aina ya tuberculosis hawa husababisha kifua kikuu. Tetanus hawa huleta tetenasi. 2.VIRUSI

Virusi ni vidogo zaidi kuliko hata bakteria. Virusi ni vijidudu vidogo sana ambavyo vyenyewe vina genetic material na protein coat. Genetic material ni chembechembe zinazowafanya waweze kuzaliana. Virusi vinaweza kushi tu kama vipo ndani ya kiumbe hai. Vyenyewe vinaweza kuzaliana kwa kutumia seli za kiumbe hai ambapowamo. Maradhi ya Ukimwi, mafua ni baadhi tu ya maradhi ya virusi.

 

3.FUNGI

Hawa huwa tumezoea kuwaita fangasi hawa wanakula kwenye seli za kiumbe hai. Mfano mzuri ni uyoga huu ni katika jamii ya viumbe hawa wanaokula kutokana na seli au kiumbe kilichokufa. Kama bakteria hata wadudu hawa wapo wanasababisha maradhi na wengine hawasababishi. Fangasi wa miguuni ni mfano mzuri wa maradhi ya wasudu hawa. Mfano mwengine ni wale wa sehemu za siri wanaopelekea kuchubua kwa koreodani kwa wanaume na madahra menginey wa wanawake.

 

4.PROTOZOA

Hawa pia ni vijidudu vidogo visivyoonekana kwa macho makavu. Hawa pia wana seli moja tu katika miili yao. Ila hawa ni wakubwa kuliko bakteia. Hawa wanasababishwa magonjwa ambayo yanaongoza kuuwa watu wengi sana dunianii. Kwa mfano malaria husababishwa na vijidudu hivi. Kwaribia watu milioni moja kila mwaka wanakufa kwa malaria katika nchi zilizopo kwenye uoto wa tropic.

 

5.PARASIT

5.Hawa ni wadudu wanaokula kiumbe hai. Mfano mzuri ni chawa, kupe, mbu na wengineo wenye mfano huu. Wadudu hawa wanajipatia chakula kwa kunyonyo viinilishe kwenye mwili wa kiumbe hai. Hawa wanaweza kuwa nche ya mwili kama chawa au ndani ya mwili kama minyoo.

 

NJIA AMBAZO MARADHI HUAMBUKIZWA

1.kutoka mtu kwenda mtu mwingine. Hii ni njia nzuri ya kuambukiza maradhi kutoka mgonjwa kwenda mzima, ama kutoka mtu kwenda mtu. Inaweza kuwa kwa njia ya hewa kama mafua pindi mgonjwa anapopiga chafya, au kifua kikuu pindi mgonjwa napokohoa. Pindi mgonjwa akikohoa au chafya anatowa mamilioni ya wadudu ambao wanabakia hewani kwa muda. Na ikitokea mtu ameivuta hewa ile anaweza kuambukizwa.

 

Kupitia kugusa maradhi yanaweza kutoka mtu hadi mtu, kwa mfano kitambaa alichotumia mtu mwenye mafua au kifuua kikuu na wewe ukashika unaweza kuwabeba wadudu wale na wakaingia kwako. Pia maradhi kama kipindupindu, homa ya mafua a ndege na ebila huweza kuambukizwa kwa kugusana.

 

Wakati mwingine kupitia kumkisi mgonjwa unaweza kupata maradhi kwa mfano homa ya ini inaweza kuambukizwa kwa kukisi kupitia mate. Pia kupitia vyombo kama kijiko au kikombe cha kunywea maji kama mgonjwa ametumia na wewe ukatumia palelpale kuweka mdomo wako.

 

2.kupitia vyakula tumeshaona mifano yake kwenye kurasa zilizopita.

3.Mazigura pia tumeona kurasa za juu

4.Wanyama kwa mfano mbwa kusababisha tetenasi na panya kusababisha ugonjwa wa taun. Hawa wanyama wanakuwa wanabeba pathogen wa maradhi hawa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 888


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Namna ya kumwosha Mgonjwa vidonda
Posti hii inahusu zaidi njia za kutumia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda, ni njia muhimu ambazo ni lazima kuzipitia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda. Soma Zaidi...

Kwanini mdomo unakuwa mchungu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za mdomo kuwa mchungu Soma Zaidi...

Utaratibu wa maisha kwa aliye athirika
Somo hili linakwenda kukuletea utaratibu wa maisha kwa aliye athirika Soma Zaidi...

Upungufu wa vyakula na madhara yake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula Soma Zaidi...

huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni
Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara Soma Zaidi...

Namna ya kumfanyia usafi Mgonjwa kwa mwili mzima.
Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani. Soma Zaidi...

Njia za kutumia Ili kuepuka tatizo la kupungua kwa damu
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa tatizo na kuishiwa damu, kuishiwa damu ni tatizo linolowakumba watu wengi na kusababisha matatizo mengi Soma Zaidi...

viapo
20. Soma Zaidi...

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia Soma Zaidi...

Zijue sababu za kupungukiwa damu mwilini
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kupungukiwa damu mwilini, ni ugonjwa unaotokana sana hasa kwa watoto wadogo chini ya miaka mitano ingawa na kwa watu wazima. Soma Zaidi...

Madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo, ni hatari inayotokea kwa mtu ambaye haujatibiwa vidonda vya tumbo. Soma Zaidi...

Malengo ya kutibu ukoma
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii Soma Zaidi...