Namna ya kuzuia ugonjwa wa kipindupindu,
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria kwa kitaalamu huitwa vibrio cholera.
Namna ya kuzuia ugonjwa wa kipindupindu.
Ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria ambaye uingia kwenye utumbo na kusababisha madhara kama vile kuharisha na kitapika zifuatazo ni njia za kuzuia kipindupindu..
1. Kuchemsha maji na kuyachuja, tunajua kuwa wadudu wengi ukaa kwenye maji na ukinywa maji hayo vidudu uingia kwenye mmengenyo wa chakula na kusababisha madhara kwa hiyo mtu huanza kuharisha,kwa hiyo tunapaswa kuchemsha maji Ili tuweze kuua hao wadudu.
2. Kunawa mikono kwa sabuni na maji baada ya kutoka choo, maana tukiwa chooni huwa tunagusa sehemu mbalimbali ambazo ni chafu na tubabeba wadudu tukishika chakula bila kunawa mikono tunakula hao wadudu na kusababisha madhara ya tumbo.
3. Nawa mikono kabla ya kuandaa chakula.
Wakati wa kuandaa chakula tunapaswa kunawa mikono kwa sababu Ili tuepuke kuweka wadudu kwenye chakula na kusababisha madhara kwa wengine ambao tunawaandalia chakula, kwa hiyo kabla ya kuandaa chakula tunapaswa kunawa mikono.
4.Epuka kula vyakula ambavyo havijaiva vizuri.
Kuna watu wengine ambao upenda kula vyakula ambavyo havijapikwa vizuri, vyakula hivyo pengine uwa na wadudu,kama hajaungua wanaoingia mwilini na kusababisha madhara makubwa ya kuharibika na kutapika,kwa hiyo tunapaswa kupika vyakula mpaka viive ndipo tuvitumie.
5. Osha matunda kwa maji Safi kabla ya kuyatumi.
Kabla ya kuandaa matunda inabidi yaoshwe vizuri, maana wadudu wengi upitia kwenye matunda na kuacha mazari ambayo usababisha madhara mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo matunda yakitumika bila kuishiwa vizuri.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 web hosting 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
HUDUMA YA KWANZA KWA MWENYE KIZUNGUZUNGU
Unapokuwa na kizunguzungu unashindwa kuudhibiti mwili wako, unaweza kuanguka kabisa.
Soma Zaidi...Nini husababisha kibofu cha mkojo kuuma na baadae kutoka damu
Katika post hii utajifunza sababu zinazowezabkuorlekea kibofu kuuma upande mmoja
Soma Zaidi...Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Dalili za fizi kuvuja damu
Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa fizi ambapo fizi huweza kuwa na maumivu, kuambukizwa, kuvuja damu kwenye fizi na Vidonda.
Soma Zaidi...Ratiba ya chanjo ya polio
Posti hii inahusu zaidi namna chanjo ya polio inavyotolewa na ratiba zake yaani kuanzia siku ya kwanza mpaka pale mtoto anapomaliza chanjo hii kwa hiyo tuone ratiba ya chanjo ya polio.
Soma Zaidi...Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume
Soma Zaidi...