Fahamu kuhusu madhara ya uzito mkubwa

Fahamu kuhusu madhara ya uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa kawaida ili mtu aweze kuwa na uzito wa kawaida ni vizuri na kiafya kupima urefu ukilinganisha na uzito wa mtu.

Madhara ya uzito kuwa mkubwa.

1 kwanza kabisa tunafahamu kwamba uzito mkubwa ni chanzo cha matatizo mbalimbali kwenye mwili wa binadamu, kuna watu wengine ni kawaida kuwaa wanene kwa sababu familia yao yote wanafanana hivyo wanakuwa na miili mikubwa pia na uzito mkubwa,ila kama kwa asilimia mwili ulikuwa mdogo na kwa sababu ya mtindo wa maisha mwili umeongezeka ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa umepunguza uzito kwa namna moja au nyingine kwa sababu kuna madhara mbalimbali yanaweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa kama tutakavyoona.

 

2. Kuwepo kwa maumivu makali kwenye mgongo.

Maumivu hayo uanzia kiunoni na kushuka kueneza kwenye mgongo hali hiyo utokea kwa sababu pingili za kwenye mgongo Uweza kuelemewa na kusababisha pingili kuchoka na kusababisha maumivu kwenye mgongo hali ambayo kwa wakati mwingine usababisha pingili za kwenye utu wa mgongo kusagika.

 

3. Kuna wakati mwingine kama unene umekuwa mkubwa sana usababisha matatizo mbalimbali ambayo ni pamoja na kushindwa kubeba ujauzito kwa wanawake kwa hiyo ni vizuri kabisa kupunguza uzito ili kuweza kupunguza na matatizo mengine ya maisha yakiwemo kushindwa kubeba mimba.

 

4. Kuwepo kwa shinikizo la damu.

Kwa kawaida unene na uzito ukiwa mwingi pia usababisha na kuwepo kwa Tatizo la shinikizo la damu kwa sababu mishipa huwa midogo na kusababisha moyo kutumia nguvu ili kuweza kusukuma damu kwa nguvu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

 

5. Kuwepo kwa kufa ganzi kwenye sehemu mbalimbali.

Kuna kipindi kunakuwepo na ganzi kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa sababu ya hewa ya oxygen gas inakuwa haifiki sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha kuwepo kwa ganzi kwenye mikono, miguu na sehemu nyingine.

 

6. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuhakikisha kwamba tunapunguza uzito na kuwa kwenye hali ya kawaida kwa sababu kuwepo kwa uzito mkubwa ni chanzo cha kuwepo pia kwa magonjwa mbalimbali.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views: 4178

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda

Soma Zaidi...
Upungufu wa vyakula na madhara yake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula

Soma Zaidi...
Kazi ya chanjo ya kifua kikuu

Posti hii inahusu kazi ya chanjo ya kifua kikuu kwa kitaalamu huitwa BCG. Ni chanjo ambayo uzuia kifua kikuu na ukoma.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa maisha kwa aliye athirika

Somo hili linakwenda kukuletea utaratibu wa maisha kwa aliye athirika

Soma Zaidi...
Faida za tumbo katika mwili wa binadamu

Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula,

Soma Zaidi...
Kumsaidia mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote machoni

Posti hii inahusu hasa jinsi uchafu, wadudu na vitu vingine vinavyoweza kuingia machoni.macho ni mojawapo ya milango mitano ya fahamu ambapo kazi yake ni kuona.

Soma Zaidi...