Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa kawaida ili mtu aweze kuwa na uzito wa kawaida ni vizuri na kiafya kupima urefu ukilinganisha na uzito wa mtu.
1 kwanza kabisa tunafahamu kwamba uzito mkubwa ni chanzo cha matatizo mbalimbali kwenye mwili wa binadamu, kuna watu wengine ni kawaida kuwaa wanene kwa sababu familia yao yote wanafanana hivyo wanakuwa na miili mikubwa pia na uzito mkubwa,ila kama kwa asilimia mwili ulikuwa mdogo na kwa sababu ya mtindo wa maisha mwili umeongezeka ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa umepunguza uzito kwa namna moja au nyingine kwa sababu kuna madhara mbalimbali yanaweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa kama tutakavyoona.
2. Kuwepo kwa maumivu makali kwenye mgongo.
Maumivu hayo uanzia kiunoni na kushuka kueneza kwenye mgongo hali hiyo utokea kwa sababu pingili za kwenye mgongo Uweza kuelemewa na kusababisha pingili kuchoka na kusababisha maumivu kwenye mgongo hali ambayo kwa wakati mwingine usababisha pingili za kwenye utu wa mgongo kusagika.
3. Kuna wakati mwingine kama unene umekuwa mkubwa sana usababisha matatizo mbalimbali ambayo ni pamoja na kushindwa kubeba ujauzito kwa wanawake kwa hiyo ni vizuri kabisa kupunguza uzito ili kuweza kupunguza na matatizo mengine ya maisha yakiwemo kushindwa kubeba mimba.
4. Kuwepo kwa shinikizo la damu.
Kwa kawaida unene na uzito ukiwa mwingi pia usababisha na kuwepo kwa Tatizo la shinikizo la damu kwa sababu mishipa huwa midogo na kusababisha moyo kutumia nguvu ili kuweza kusukuma damu kwa nguvu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
5. Kuwepo kwa kufa ganzi kwenye sehemu mbalimbali.
Kuna kipindi kunakuwepo na ganzi kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa sababu ya hewa ya oxygen gas inakuwa haifiki sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha kuwepo kwa ganzi kwenye mikono, miguu na sehemu nyingine.
6. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuhakikisha kwamba tunapunguza uzito na kuwa kwenye hali ya kawaida kwa sababu kuwepo kwa uzito mkubwa ni chanzo cha kuwepo pia kwa magonjwa mbalimbali.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Hata kama mtu atakuambbia usile vyakula yenye mafuta bado itahitajika kula tu. Kuna mafuta na fati je unajuwa utofauti wao. Ni zipi kazi zao mwilini? Endelea na makala hii
Soma Zaidi...Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi, mimba kutungwa ni kitendo ambapo mbegu za kiume kuungana na yai la kike na kutengeneza zygote.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa figo. Ni ugonjwa unaotokana pale figo linaposhindwa kufanya kazi, tuone mbinu za kufanya Ili kuepuka na tatizo hilo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu njia mbalimbali ambazo utumika kupitisha chanjo, njia hizo utegemea na kazi ya chanjo kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Rangi za mkojo na maana zake na mkojo mchafu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia damu isiendelee kuvuja, ni njia ambazo utumika ikiwa kuna damu inavuja kwenye sehemu yoyote ya mwili,kwa hiyo tunaweza kutumia njia hizi ili kuepuka kuendelea kuvuja kwa damu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kazi za ini, ni kiungo muhimu kwenye mwili ambacho Kina umuhimu sana, bila ini maisha ya mwanadamu yanaweza kuishia pabaya
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ya kunywa pombe kiafya, ni madhara ambayo utokea kwa watu wanaokumywa pombe kwa kupita kiasi kwa hiyo wanapaswa kupunguza kunywa pombe baada ya kujua madhara yake.
Soma Zaidi...