Choo kisichokuwa cha kawaida
Posti hii inahusu zaidi Aina ya choo kisichokuwa cha kawaida, ni dalili za choo ambacho siyo Cha kawaida, Ina maana ukiona dalili za choo Cha Aina hii ni vizuri kwenda hospitalini Ili kupata matibabu.
Choo kisichokuwa cha kawaida.
1. Choo kuwa kigumu.
Choo kisichokuwa huwa ni kigumu na Kuna shida wakati wa kutoa choo hicho kwa kitaalamu huitwa constipation, hali hii uwatokea hasa watu wale ambao huwa hawanywi maji ambapo maji ufyonzwa kwenye choo na kwenda kufanya kazi mbalimbali kwenye sehemu za mwili , choo hiki kwa kawaida huwa na kikavu kabisa, wakati mwingine mtu ufikishwa hospitalini na kupata matibabu zaidi kwa sababu ya choo kuwa kigumu, kwa hiyo watu wanashauliwa kunywa maji kwa wingi Ili kufanya choo kuwa laini.
2. Kinyesi kuwa kilaini au kuharisha.
Ni kitendo Cha kupitisha kinyesi kama maji , kinyesi hiki huwa ni maji hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye tumbo ambapo pengine mtu anakuwa amekula chakula kichafu au pengine ni kwa sababu ya magonjwa ambayo yapo mwilini, kwa hali ya kawaida kinyesi hakipaswa kuwa hivi kinapaswa kuwa Cha kawaida bila kuwa kwenye mfumo wa maji, kwa hiyo kuharisha ni kitendo mibaya ambacho upelekea kuishiwa na maji mwilini na kusababisha madhara mengine makubwa zaidi ambayo huwezi kutengeneza, kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kinyesi kinakuwa Cha kawaida.
3. Kinyesi kuwa na damu.
Hali ya kinyesi hiki siyo ya kawaida kwa sababu kinyesi hakipaswa kuwa na damu, hali ya kinyesi kuwa na damu ni kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye sehemu mbalimbali kama vile kwenye coloni na sehemu nyingine ambapo kinyesi upitia na kutoka nje kwa hiyo ikiwa mtu anaona damu kwenye kinyesi anapaswa kwenda hospitalini kupima.
4. Kinyesi kuwa na rangi ya kijani.
Hii ni Aina ya kinyesi ambapo kinyesi kinakuwa na rangi ya kijani kwa sababu mbalimbali kama vile kuwepo kwa matatizo kwenye mmengenyo wa chakula na mara nyingine kula sana mboga za majani ufanya kinyesi kuwa na rangi ya kijani. Kwa hiyo kinyesi kikiwa na rangi ya kijani tunapaswa kwenda hospitalini Ili kuangalia shida ni nini?. Itambulik kuwa kama ulikula mboga za majani huwenda ikasababisha kinyesi kuwa cha kijani, hivyo hakuna haja ya kuogopa.
5. Kuwepo kwa Ute mwingi kwenye kinyesi na pia kuwepo kwa usaha kwenye kinyesi.
Hali hii ya kuwepo kwa usaha na Ute kwenye kinyesi sio hali ya amani labda Kuna maambukizi yoyote kwenye sehemu ambapo kinyesi upitia na Aina ya chakula ambacho mtu utumia Mara kwa mara na ufanya kuwepo kwa Ute mwingi kwenye kinyesi, kwa hiyo hali hii sio nzuri inabidi kuchukua vipimo maana Pana uwezekano wa kuwepo kwa maambukizi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 web hosting 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure
Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili
Soma Zaidi...Madhara ya kuchelewa kutibu tatizo la kiafya
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.
Soma Zaidi...Dalili za shambulio la hofu
Shambulio la hofu ni tukio la ghafla la hofu kali ambayo husababisha athari kali za kimwili wakati hakuna hatari halisi au sababu inayoonekana. Mashambulizi ya hofu yanaweza kuwa ya kutisha sana. Mashambulizi ya hofu yanapotokea, unaweza kufikiri kwamba
Soma Zaidi...Njia ambazo maradhi huambukizwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo maradhi huambukizwa
Soma Zaidi...Mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu.
Posti hii inahusu zaidi mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu, tunajua kubwa kifua kikuu ni Ugonjwa ambao utumia mda mrefu kidogo katika matibabu kwa hiyo mgawanyiko wake uko kwenye sehemu mbili muhimu kama tutajavyoona
Soma Zaidi...Huduma ya kwanza kwa mwenye uchafu kwenye sikio.
Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kqa mgonjwa aliyeingiliwa na kitu au uchafu kwenye sikio.
Soma Zaidi...