picha

Choo kisichokuwa cha kawaida

Posti hii inahusu zaidi Aina ya choo kisichokuwa cha kawaida, ni dalili za choo ambacho siyo Cha kawaida, Ina maana ukiona dalili za choo Cha Aina hii ni vizuri kwenda hospitalini Ili kupata matibabu.

Choo kisichokuwa cha kawaida.

1. Choo kuwa kigumu.

Choo kisichokuwa huwa ni kigumu na Kuna shida wakati wa kutoa choo hicho kwa kitaalamu huitwa constipation, hali hii uwatokea hasa watu wale ambao huwa hawanywi maji ambapo maji ufyonzwa kwenye choo na kwenda kufanya kazi mbalimbali kwenye sehemu za mwili , choo hiki kwa kawaida huwa na kikavu kabisa, wakati mwingine mtu ufikishwa hospitalini na kupata matibabu zaidi kwa sababu ya choo kuwa kigumu, kwa hiyo watu wanashauliwa kunywa maji kwa wingi Ili kufanya choo kuwa laini.

 

2. Kinyesi kuwa kilaini au kuharisha.

Ni kitendo Cha kupitisha kinyesi kama maji , kinyesi hiki huwa ni maji  hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye tumbo ambapo pengine mtu anakuwa amekula chakula kichafu au pengine ni kwa sababu ya magonjwa ambayo yapo mwilini, kwa hali ya kawaida kinyesi hakipaswa kuwa hivi kinapaswa kuwa Cha kawaida bila kuwa kwenye mfumo wa maji, kwa hiyo kuharisha ni kitendo mibaya ambacho upelekea kuishiwa na maji mwilini na kusababisha madhara mengine makubwa zaidi ambayo huwezi kutengeneza, kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kinyesi kinakuwa Cha kawaida.

 

3. Kinyesi kuwa na damu.

Hali ya kinyesi hiki siyo ya kawaida kwa sababu kinyesi hakipaswa kuwa na damu, hali ya kinyesi kuwa na damu ni kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye sehemu mbalimbali kama vile kwenye coloni na sehemu nyingine ambapo kinyesi upitia na kutoka nje  kwa hiyo ikiwa mtu anaona damu kwenye kinyesi anapaswa kwenda hospitalini kupima.

 

4. Kinyesi kuwa na rangi ya kijani.

Hii ni Aina ya kinyesi ambapo kinyesi kinakuwa na rangi ya kijani kwa sababu mbalimbali kama vile kuwepo kwa matatizo kwenye mmengenyo wa chakula na mara nyingine kula sana mboga za majani ufanya kinyesi kuwa na rangi ya kijani. Kwa hiyo kinyesi kikiwa na rangi ya kijani tunapaswa kwenda hospitalini Ili kuangalia shida ni nini?. Itambulik kuwa kama ulikula mboga za majani huwenda ikasababisha kinyesi kuwa cha kijani, hivyo hakuna haja ya kuogopa.

 

5. Kuwepo kwa Ute mwingi kwenye kinyesi na pia kuwepo kwa usaha kwenye kinyesi.

Hali hii ya kuwepo kwa usaha na Ute kwenye kinyesi sio hali ya amani labda Kuna maambukizi yoyote kwenye sehemu ambapo kinyesi upitia na Aina ya chakula ambacho mtu utumia Mara kwa mara na ufanya kuwepo kwa Ute mwingi kwenye kinyesi, kwa hiyo hali hii sio nzuri inabidi kuchukua vipimo maana Pana uwezekano wa kuwepo kwa maambukizi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 4312

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 web hosting     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Namna ya kusaidia mwili kupambana na maradhi

Somo hili linakwenda kukuletea namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Soma Zaidi...
Mbinu za kuponyesha majeraha

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo hutumika kuponyesha majeraha kwa haraka zaidi,tunajua majereha utokana na kupona kwa vile vidonda au kupona kwa sehemu ambayo imekuwa na majeraha kwa hiyo ili kuponyesha majeraha hayo tunapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Utajuwaje kama kidonda kupona

Posti hii inahusu zaidi juu ya kuhakiki kama kidonda kimepona kwa mgonjwa mwenye vidonda, kwanza kabisa tunajua kuwa vidonda uwanyima Watu raha na pengine kuwafanya wakate tamaa kama wapo hospitalini kwa hiyo tunapaswa kutumia njia zifuatazo ili kuweza ku

Soma Zaidi...
Vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda.

Posti hii inahusu zaidi vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda, ni vifaa muhimu ambavyo mara nyingi kutwa hospitalini.

Soma Zaidi...
Njia za kufuata unapohudumia watu waliopata ajali

Post hii inahusu zaidi namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa watu waliopata ajali. Ajali ni tukio lisilotarajiwa ambalo kinaweza kumkuta mtu yeyote, tunapotoa huduma ya kwanza tnazingatia rangi ambazo huwakilisha jinsi watu walivyoumia.

Soma Zaidi...
Aina mbalimbali za maumivu ya mwili.

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali ya maumivu ya mwili, Maumivu ya mwili utokea kwa aina mbalimbali kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...