picha

Choo kisichokuwa cha kawaida

Posti hii inahusu zaidi Aina ya choo kisichokuwa cha kawaida, ni dalili za choo ambacho siyo Cha kawaida, Ina maana ukiona dalili za choo Cha Aina hii ni vizuri kwenda hospitalini Ili kupata matibabu.

Choo kisichokuwa cha kawaida.

1. Choo kuwa kigumu.

Choo kisichokuwa huwa ni kigumu na Kuna shida wakati wa kutoa choo hicho kwa kitaalamu huitwa constipation, hali hii uwatokea hasa watu wale ambao huwa hawanywi maji ambapo maji ufyonzwa kwenye choo na kwenda kufanya kazi mbalimbali kwenye sehemu za mwili , choo hiki kwa kawaida huwa na kikavu kabisa, wakati mwingine mtu ufikishwa hospitalini na kupata matibabu zaidi kwa sababu ya choo kuwa kigumu, kwa hiyo watu wanashauliwa kunywa maji kwa wingi Ili kufanya choo kuwa laini.

 

2. Kinyesi kuwa kilaini au kuharisha.

Ni kitendo Cha kupitisha kinyesi kama maji , kinyesi hiki huwa ni maji  hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye tumbo ambapo pengine mtu anakuwa amekula chakula kichafu au pengine ni kwa sababu ya magonjwa ambayo yapo mwilini, kwa hali ya kawaida kinyesi hakipaswa kuwa hivi kinapaswa kuwa Cha kawaida bila kuwa kwenye mfumo wa maji, kwa hiyo kuharisha ni kitendo mibaya ambacho upelekea kuishiwa na maji mwilini na kusababisha madhara mengine makubwa zaidi ambayo huwezi kutengeneza, kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kinyesi kinakuwa Cha kawaida.

 

3. Kinyesi kuwa na damu.

Hali ya kinyesi hiki siyo ya kawaida kwa sababu kinyesi hakipaswa kuwa na damu, hali ya kinyesi kuwa na damu ni kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye sehemu mbalimbali kama vile kwenye coloni na sehemu nyingine ambapo kinyesi upitia na kutoka nje  kwa hiyo ikiwa mtu anaona damu kwenye kinyesi anapaswa kwenda hospitalini kupima.

 

4. Kinyesi kuwa na rangi ya kijani.

Hii ni Aina ya kinyesi ambapo kinyesi kinakuwa na rangi ya kijani kwa sababu mbalimbali kama vile kuwepo kwa matatizo kwenye mmengenyo wa chakula na mara nyingine kula sana mboga za majani ufanya kinyesi kuwa na rangi ya kijani. Kwa hiyo kinyesi kikiwa na rangi ya kijani tunapaswa kwenda hospitalini Ili kuangalia shida ni nini?. Itambulik kuwa kama ulikula mboga za majani huwenda ikasababisha kinyesi kuwa cha kijani, hivyo hakuna haja ya kuogopa.

 

5. Kuwepo kwa Ute mwingi kwenye kinyesi na pia kuwepo kwa usaha kwenye kinyesi.

Hali hii ya kuwepo kwa usaha na Ute kwenye kinyesi sio hali ya amani labda Kuna maambukizi yoyote kwenye sehemu ambapo kinyesi upitia na Aina ya chakula ambacho mtu utumia Mara kwa mara na ufanya kuwepo kwa Ute mwingi kwenye kinyesi, kwa hiyo hali hii sio nzuri inabidi kuchukua vipimo maana Pana uwezekano wa kuwepo kwa maambukizi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 3487

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 web hosting    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Aina za vidonda

Posti hii inahusu zaidi Aina mbalimbali za vidonda kwenye mwili wa binadamu, ni vidonda ambavyo utokea kwenye mwili wa binadamu kwa Aina tofauti.

Soma Zaidi...
Namna ugonjwa wa herpes simplex unavyosambaa.

Posti hii inahusu zaidi namna ya ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza nywele za mgonjwa

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza nywele za mgonjwa hasa kwa wagonjwa mahututi na wale wasiojiweza tunafanya hivyo ili tuweze kuwatoa kwenye hali ya usafi.

Soma Zaidi...
Madhara ya chakula kutosagwa vizuri tumboni.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya chakula kushindwa kumengenywa vizuri tumboni, haya ni madhara ambayo utokea kwa sababu ya chakula kushindwa kumengenywa vizuri tumboni.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupumzika kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupumzika kiafya, kwa kawaida mwili na viungo vingine vya mwili uweza kufanya kazi zaidi pale mtu akiwa amepumzika.

Soma Zaidi...
Imani potofu juu ya ugonjwa wa Ukimwi.

Posti hii inahusu zaidi imani potofu juu ya ugonjwa wa Ukimwi,ni Imani walizonazo watu wengi kuhusiana na ugonjwa wa Ukimwi.

Soma Zaidi...
Zijue sababu za kupoteza fahamu.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Mfuno wa damu na makundi manne ya damu na asili yake nani anayepasa kutoa damu?

Posti hii inakwenda kukujuza kuhusu makundi manne ya damu, asili yake, maana ya antijeni na antibody, pia utajifunza kuhusu mfumo wa Rh. Mwisho utajifunza watu wanaopasa kutoa damu.

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Njia juu zinazosababisha kuenea kwa ugonjwa wa Ukimwi

Post hii inahusu zaidi njia za kuenea kwa ugonjwa wa Ukimwi. Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.

Soma Zaidi...