Tufaha ni katika matunda adimu na matamu, je unazijuwa faida zake kkiafya?
5.Tufaha (apple) au epo.
Hili ni katika matunda yaliyokuwa na historia katika maisha ya binadamu toka zamani sana. Wataalamu wa afya wanazungumzia tunda hili kuwa limesheheni virutubisho vingi sana. Tunda hili lina kiasi kikubwa cha vitamin C, vitamin K na vitamini B, pia tunda hili lina kiasi kikubwa cha madini ya potassium pamoja na kambakamba yaani fiber.
Tafiti za kisayansi zinathibitisha kuwa antioxodant iliyopo kwenye tunda hili husaidia katika kuimarisha afya ya moyo na kupunguza hatari ya kupata maradhi ya kisukari hasa kile kinachoitwa type 2 diaberes. Pia antioxidant iliyopo kwenye tunda hili huzuia kupata maradhi ya saratani (cancer) na kusaidia katika kuongeza ujazo wa kwenye mifupa.
Tafiti nyingine za kisayansi zinathibitisha kuwa tunda hili lina pectin. Hii pia huitwa prebiotic fiber nayo husaidia katika kupambana na kuuwa bakteria waliopo tumboni na kusaidia mfumo wa mmengβenyo wa chakula kuwa katika hali salama na madhubuti. Pia husaidia afya katika metabolic activities nazo na shuhuli zote za kikemikali zinazofanyika ndani ya seli.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula ambavyo vinaweza kupunguza presha ya kupanda
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula ukwaju
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula nanasi
Soma Zaidi...Zijuwe sababu za upungufu wa damu, dalili za upungufu wa damu na kazi za damu mwilini,n avyakula vya kuongeza damu
Soma Zaidi...Umetaja faida za matunda , mimi ninataka kujuwa Je miwa ina madhara yoyote?
Soma Zaidi...Hapa tutaona kuhusu virutubisho vya wanga, kazi zake na athari za upungufu wake
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...