Mambo yanayosababisha kupona kwa vidonda.

Posti hii inahusu mambo yanayochangia katika kupona kwa kidonda, ni mambo ambayo yapo kwa mgonjwa mwenyewe kama ifuayavyo.

Mambo yanayosababisha kupona kwa vidonda.

1. Kiasi au kiwango Cha kidonda.

Kwa kawaida kidonda kikiwa kikubwa uponaji wake uchelewa ukiulinganisha kama kidonda ni kidogo na uponyaji wake uwahi hii ni kwa sababu kidonda kikiwa kikubwa labda na wadudu waliopo ni wengi kuliko kidonda kidogo uwa na wadudu wachache na utunzaji wa kidonda kikubwa ni shida kuliko utunzaji wa kidonda kidogo huwa ni afadhari kwa hiyo kiasi Cha kidonda usaidia kupona haraka kwa kidonda hicho.

 

2. Mlo wa mgonjwa wa kidonda usaidia kidonda kupona kwa sababu. 

Mgonjwa wa kidonda kama anatumia mlo kamili kama vile  kiasi kikubwa Cha vyakula vya protein,  kiasi Cha kutosha kwa vitamini C kiwango Cha kupona kwa vidonda ni kwa urahisi ukiulinganisha na mtu ambaye mlo wake ni wa kubabaisha kwa hiyo tunajua kabisa kuwa chakula Bora ni dawa kwa hiyo tunapaswa kula vyakula mbalimbali ambavyo vinaongeza kinga mwilini Ili pale tunaposhambuliwa na vidonda tuweze kupona haraka na kurudia kwenye hali zetu za kawaida.

 

3.umri wa mgonjwa.

Umri wa mgonjwa nao pia uchangiwa katika uponyaji wa vidonda, kama ni mtoto atachukua mda mfupi tu kupona kwa sababu seli zake zinazalishwa kila mara na viungo vyake bado vinafanya kazi vizuri kuliko Mzee, lakini kama ni mzee kupona kwake kitakuwa ni shida kwa sababu kiasi Cha seli zinazokufa ni nyingi kuliko zile zinazozalishwa au pengine seli zinazozalishwa na kufa ni sawa kuliko kwa mtoto ambaye seli zinazaliana ni nyingi zile zinazoharibika.

 

4. Kuwepo kwa Magonjwa.

Kuwepo kwa magonjwa mengine kwa mtu Mwenye kidonda usababisha kidonda kupona kwa mda mrefu kuliko mtu yule ambaye Hana magonjwa, kwa mfano  mgonjwa wa kisukari utumia mda mrefu kupona kwa sababu ya kuwepo kiwango Cha sukari nyingi kwenye damu.kuliko mtu ambaye Hana ugonjwa wa kisukari upona mapema zaidi kwa sababu ya kuwepo kwa sukari ya kawaida kwenye mwili.

 

5. Sehemu ambapo kidonda kipo.

Kidonda kama kipo sehemu za miguuni, kwenye kucha, na sehemu ambazo ni rahisi kuwepo kwa uchafu kupona kwa kidonda uchelewa kuliko kama kidonda kipo kwenye sehemu za usoni ambapo ni rahisi kusafisha.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 2262

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPANDWA NA PRESHA

Presha ya kupanda hutokea pale kipimo kinaposoma zaidi ya 120/80mm Hg.

Soma Zaidi...
Aina kuu tatu za mvunjiko wa viuno vya mwilini na mifupa

Posti hii inahusu zaidi Aina kuu tatu za mvunjiko ni Aina za kuvunjika ambazo uwakumba watu mbalimbali na watu ushindwa kutambua hizi Aina tatu za mvunjiko, zifuatazo ni Aina za mvunjiko.

Soma Zaidi...
Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.

Soma Zaidi...
Kuboresha afya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mambo yanayosaidia kuboresha afya

Soma Zaidi...
Njia za kujikinga na kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATWA NA KWIKWI

Kwikwi sio hatari sana kwa afya, lakini inaweza kuwa hatari zaidi kwa mu aliyefanyiwa upasuaji kwenye tumbo.

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanza kwa mgonjwa aliyepata ajali ya kichwa

Ajali ya kichwa na ajali inayotolewa kwenye sehemu mbalimbali za kichwa, ambavyo husababishwa madhara kwa aliyepata ajali hiyo

Soma Zaidi...
Mkojo usio wa kawaida huwa na vitu vifuatavyo.

Posti hii inahusu zaidi Aina ya mkojo usiokuwaa wa kawaida uwa na vitu vifuatavyo, ukiona dalili kama hizo wahi mapema hospitalini Ili upatiwe huduma.

Soma Zaidi...
Habari,mfano umekunywa dawa za chupa hizi halafu baadae unagundua chupa ilikuwa na UFA nn kofanyike

Kunywa soda ama dawa kwenyechupa zakioo ambayo ina ufa ama mipasuko ni hatari. Ni kwa sababu huwezijuwa huwenda kipande kikaingia mdomoni na umangimeza. Sasa nini ufanye endapo umeshakula?

Soma Zaidi...