Malengo ya kutibu ukoma
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii
Malengo ya kutibu ugonjwa wa ukoma.
1.Tunajua kabisa ukoma ni Ugonjwa ambao ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye miguu na mikono na mara nyingi uondoa vidole vya kwenye miguu na mikono na mgonjwa huyo anakuwa hasikii maumivu ila uona kidole kinaondoka kwa sababu wadudu wanaharibu mfumo wa Neva system na kumfanya mgonjwa hasisikie maumivu wakati vidole vinapokuwa vinadondoka, kwa hiyo malengo ni kama ifuatavyo.
2.Kuzuia kuaribika kwa nevu na tisu nyingine kwenye mwili wa binadamu, kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria kwenye mwili usababisha nevu kuaribika na kuaribika kwa tishu kwa hiyo dawa mbalimbali zimeweza kupatikana na kuweza kupunguza ugonjwa huu kwa sasa ni Watu wachache ambao wanapatwa na ugonjwa kama huu kwa sababu ya kuwepo kwa dawa.
3. Kuzuia ugonjwa huu kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Tunajua kubwa ugonjwa huu una tabia ya kusambaa kwa hiyo ikiwa kwenye familia amepata mtu mmoja na kama haujatibiwa anaweza kumwambikiza mtu mwingine na kusababisha kuwepo kwenye familia na kwa jamii ambazo zina imani potovu wanaweza kusema kuwa ni Ugonjwa wa familia kumbe ni kwa sababu ya kutotibu ugonjwa huu kwa hiyo jamii inapaswa kujua na kutibu ugonjwa huu mapema kabla haujaanza kusambaa.
4.Kutokomeza kabisa ugonjwa huu.
Lengo kuu la afya ni kuhakikisha kwamba ugonjwa huu inatokomezwa kwanza kwa kutambua mazingira ambapo Ugonjwa huu upo kwa kiasi kikubwa, kutoa elimu hasa vijijini ili kutowatenga na kuwafukuza majumbani mwao wagonjwa wa ukoma, kuihakikishia jamii kuwa ugonjwa huu unatibika na pia kutibu ugonjwa huu kwa dawa zilizopendekezwa, kwa kufanya hivyo ugonjwa huu utapungua.
5.Kws hiyo mpaka sasa kwenye jamii ugonjwa huu umepungua kwa kiwango kikubwa mno kwa hiyo elimu inapaswa kuendelea kutolewa ili kuweza kutokomeza kabisa ugonjwa huu na inawezekana ukatokomezwa kwa hiyo tujue kuwa ugonjwa huu upo na unatibika na dawa zipo na wengi wamepona
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Kitabu cha Afya ๐2 kitabu cha Simulizi ๐3 Madrasa kiganjani ๐4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐5 Kitau cha Fiqh ๐6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Mbinu za kuponyesha majeraha
Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo hutumika kuponyesha majeraha kwa haraka zaidi,tunajua majereha utokana na kupona kwa vile vidonda au kupona kwa sehemu ambayo imekuwa na majeraha kwa hiyo ili kuponyesha majeraha hayo tunapaswa kufanya yafuatayo.
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGโATWA NA NYUKI
Kungโatwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATWA NA KWIKWI
Kwikwi sio hatari sana kwa afya, lakini inaweza kuwa hatari zaidi kwa mu aliyefanyiwa upasuaji kwenye tumbo.
Soma Zaidi...Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda
Soma Zaidi...Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...