Kiasi Cha mkojo kisichokuwa cha kawaida.
Hii posti inahusu zaidi sifa za mkojo usio wa kawaida,ukiona mkojo wa namna hii unapaswa kwenda hospitalini kwa matibabu au vipimo vya zaidi.
Kiasi Cha mkojo kisicho Cha kawaida
1.kiasi Cha mkojo ,
Kuna wakati mwingine kiasi Cha mkojo ubadilika na kuwa mwingi au kidogo, ikiwa kiasi Cha mkojo kinaongezeka kuliko kawaida inawezekana ikawa ni shida ya sukari mwilini hii hali ya mkojo kuwa mwingi huitwa polyuria na pengine kiasi Cha mkojo kuongezeka inawezekana mtu ametumia dawa kama vile frusemide,au lasix, potassium citrate na digitalis hizi ni dawa ambazo uongeza kiwango Cha mkojo.
2.Na Kuna wakati mwingine kiasi Cha mkojo kinapungua hii kwa kitaalamu huitwa Oliguria kiasi Cha mkojo kinapungua ndani ya maasaa ishilini na manne hili tatizo utokea zaidi kwa watu wenye matatizo kwenye nephroni, matatizo ya moyo, na watu wale wenye ugonjwa wa kuishiwa maji iwapo mtu anaona dalili hizi za kuona kiasi kidogo Cha mkojo anapaswa kwenda hospitalini kupima.
3. Kuna wakati mwingine mkojo ukosa kabisa na figo linakuwa halitoi kabisa mkojo,hii ni hatari kwa sababu kunakuwepo na matatizo kwenye nephroni au kwenye figo au pengine damu inashindwa kusafili mpaka kwenye figo na usababisha kutokuwepo kwa mkojo kwa mtu, hii hali ikitokea ndani ya maasaa ishilini na manne mgonjwa Inabidi apelekwe hospitali kwa uchunguzi zaidi.
4 Tunapaswa kujua kuwa kitendo Cha mkojo kukosa ndani ya maasaa ishilini na manne ni tofauti na Ile hali ya mtu kusikia mkojo lakini akawa anashindwa namna ya kupitisha kwa Sababu maalumu kwa hiyo tunapaswa kumhudumia mgonjwa ambaye anakosa mkojo na kunywa anakunywa kila kitu kama kawaida.
5. Kwa hiyo tukiona kitendo Cha mtu kukojoa mara kwa mara, au kukojoa kidogo,au kushindwa kukojoa kabisa tujue kuwa sio dalili nzuri kwa sababu mkojo unachujwa kutoka sehemu mbalimbali za mwili Ili kuondoa sumu mwilini, kwa hiyo sumu isipoondolewa shida nyingine zinaweza kutokea kwenye mwili wa binadamu na kusababisha madhara mengine makubwa,kwa hiyo tunapaswa kudhibiti hali hii mapema.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 web hosting 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia
Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia, hii ni chanjo inayozuia hasa hasa Magonjwa ya mfumo wa hewa kwa hiyo nayo upewa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Namna ya kuchoma chanjo
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuchoma chanjo, ni njia ambazo utumika kutoa chanjo kwa watoto na watu wazima kwa utaratibu uliowekwa.
Soma Zaidi...Zijue sababu za kupoteza fahamu.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Faida za chanjo
Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure
Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili
Soma Zaidi...Kazi za vitamin B na makundi yake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kazi za vitamin B na makundi take
Soma Zaidi...