Kiasi Cha mkojo kisichokuwa cha kawaida.
Hii posti inahusu zaidi sifa za mkojo usio wa kawaida,ukiona mkojo wa namna hii unapaswa kwenda hospitalini kwa matibabu au vipimo vya zaidi.
Kiasi Cha mkojo kisicho Cha kawaida
1.kiasi Cha mkojo ,
Kuna wakati mwingine kiasi Cha mkojo ubadilika na kuwa mwingi au kidogo, ikiwa kiasi Cha mkojo kinaongezeka kuliko kawaida inawezekana ikawa ni shida ya sukari mwilini hii hali ya mkojo kuwa mwingi huitwa polyuria na pengine kiasi Cha mkojo kuongezeka inawezekana mtu ametumia dawa kama vile frusemide,au lasix, potassium citrate na digitalis hizi ni dawa ambazo uongeza kiwango Cha mkojo.
2.Na Kuna wakati mwingine kiasi Cha mkojo kinapungua hii kwa kitaalamu huitwa Oliguria kiasi Cha mkojo kinapungua ndani ya maasaa ishilini na manne hili tatizo utokea zaidi kwa watu wenye matatizo kwenye nephroni, matatizo ya moyo, na watu wale wenye ugonjwa wa kuishiwa maji iwapo mtu anaona dalili hizi za kuona kiasi kidogo Cha mkojo anapaswa kwenda hospitalini kupima.
3. Kuna wakati mwingine mkojo ukosa kabisa na figo linakuwa halitoi kabisa mkojo,hii ni hatari kwa sababu kunakuwepo na matatizo kwenye nephroni au kwenye figo au pengine damu inashindwa kusafili mpaka kwenye figo na usababisha kutokuwepo kwa mkojo kwa mtu, hii hali ikitokea ndani ya maasaa ishilini na manne mgonjwa Inabidi apelekwe hospitali kwa uchunguzi zaidi.
4 Tunapaswa kujua kuwa kitendo Cha mkojo kukosa ndani ya maasaa ishilini na manne ni tofauti na Ile hali ya mtu kusikia mkojo lakini akawa anashindwa namna ya kupitisha kwa Sababu maalumu kwa hiyo tunapaswa kumhudumia mgonjwa ambaye anakosa mkojo na kunywa anakunywa kila kitu kama kawaida.
5. Kwa hiyo tukiona kitendo Cha mtu kukojoa mara kwa mara, au kukojoa kidogo,au kushindwa kukojoa kabisa tujue kuwa sio dalili nzuri kwa sababu mkojo unachujwa kutoka sehemu mbalimbali za mwili Ili kuondoa sumu mwilini, kwa hiyo sumu isipoondolewa shida nyingine zinaweza kutokea kwenye mwili wa binadamu na kusababisha madhara mengine makubwa,kwa hiyo tunapaswa kudhibiti hali hii mapema.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 ai web app 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Njia za kujikinga na vidonda vya tumbo
Kama unahitaji kujuwa namna ya kuweza kujikinga na vidonda vya tumbo, basi makala hii ni kwa ajili yako. Hapa utaweza kuzijuwa hatuwa zote za kujikinga na kupata vidonda vya tumbo.
Soma Zaidi...Huduma ya kanza kwa mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza ya mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo, ni Tiba ambayo utolewa kulingana na dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Njia za kuongeza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya njia za kuongeza nguvu za kiume
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa aliyeungua
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa aliyeungua
Soma Zaidi...Faida za kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi faida za kusafisha vidonda, ni faida ambazo Mgonjwa mwenye vidonge uzipata kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...