Hii posti inahusu zaidi sifa za mkojo usio wa kawaida,ukiona mkojo wa namna hii unapaswa kwenda hospitalini kwa matibabu au vipimo vya zaidi.
Kiasi Cha mkojo kisicho Cha kawaida
1.kiasi Cha mkojo ,
Kuna wakati mwingine kiasi Cha mkojo ubadilika na kuwa mwingi au kidogo, ikiwa kiasi Cha mkojo kinaongezeka kuliko kawaida inawezekana ikawa ni shida ya sukari mwilini hii hali ya mkojo kuwa mwingi huitwa polyuria na pengine kiasi Cha mkojo kuongezeka inawezekana mtu ametumia dawa kama vile frusemide,au lasix, potassium citrate na digitalis hizi ni dawa ambazo uongeza kiwango Cha mkojo.
2.Na Kuna wakati mwingine kiasi Cha mkojo kinapungua hii kwa kitaalamu huitwa Oliguria kiasi Cha mkojo kinapungua ndani ya maasaa ishilini na manne hili tatizo utokea zaidi kwa watu wenye matatizo kwenye nephroni, matatizo ya moyo, na watu wale wenye ugonjwa wa kuishiwa maji iwapo mtu anaona dalili hizi za kuona kiasi kidogo Cha mkojo anapaswa kwenda hospitalini kupima.
3. Kuna wakati mwingine mkojo ukosa kabisa na figo linakuwa halitoi kabisa mkojo,hii ni hatari kwa sababu kunakuwepo na matatizo kwenye nephroni au kwenye figo au pengine damu inashindwa kusafili mpaka kwenye figo na usababisha kutokuwepo kwa mkojo kwa mtu, hii hali ikitokea ndani ya maasaa ishilini na manne mgonjwa Inabidi apelekwe hospitali kwa uchunguzi zaidi.
4 Tunapaswa kujua kuwa kitendo Cha mkojo kukosa ndani ya maasaa ishilini na manne ni tofauti na Ile hali ya mtu kusikia mkojo lakini akawa anashindwa namna ya kupitisha kwa Sababu maalumu kwa hiyo tunapaswa kumhudumia mgonjwa ambaye anakosa mkojo na kunywa anakunywa kila kitu kama kawaida.
5. Kwa hiyo tukiona kitendo Cha mtu kukojoa mara kwa mara, au kukojoa kidogo,au kushindwa kukojoa kabisa tujue kuwa sio dalili nzuri kwa sababu mkojo unachujwa kutoka sehemu mbalimbali za mwili Ili kuondoa sumu mwilini, kwa hiyo sumu isipoondolewa shida nyingine zinaweza kutokea kwenye mwili wa binadamu na kusababisha madhara mengine makubwa,kwa hiyo tunapaswa kudhibiti hali hii mapema.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi matumizi ya vidonge vya ARV, ni vidonge vinavyotumiwa na wagonjwa waliopata ugonjwa wa Ukimwi
Soma Zaidi...Post inaenda kuzungumzia kuhusiana na upungufu wa damu mwilini ambapo tutaona SABABU na dalili zake lakin upungufu wa damu mwilini hujulikana Kama ANEMIA.
Soma Zaidi...Katika post hii utajifunza sababu zinazowezabkuorlekea kibofu kuuma upande mmoja
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mkojo wa kawaida kwa kila mwanadamu na unavyopaswakuwa, mkojo wa kawaida kwa binadamu huwa na sifa zifuatazo.
Soma Zaidi...Kwikwi sio hatari sana kwa afya, lakini inaweza kuwa hatari zaidi kwa mu aliyefanyiwa upasuaji kwenye tumbo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula,
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kushuka
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi umuhimu wa makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika, Ni magroup manne ya damu ambayo husaidia kuongeza damu kwa mtu ambaye amepungukiwa damu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu homa ya uti wa mgongo, kwa kuwa ugonjwa huu mara nyingi uathiri sehemu za kwenye ubongo kuna madhara ambayo yanaweza kutokea endapo Ugonjwa huu haujatibiwa mapema.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe, ni kipindi ambacho ni kutoka utotoni kwendea ujana.
Soma Zaidi...