picha

Imani potofu kuhusu kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi imani potofu waliyonayo Watu kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu, hizi ni imani ambazo uwepo kwenye jamii na pengine uweza kuaminika lakini si za ukweli.

Imani potofu kuhusu kifua kikuu.

1.mwenye kifua kikuu ana Maambukizi ya virus vya ukimwi, hii ni mojawapo ya imani ambayo imo miongoni mwao Watu wengi wakiamini kuwa mwenye kifua kikuu ana Maambukizi ya virus vya ukimwi, hii siyo kweli kwa sababu kifua kikuu kinapona ila Ukimwi hauna dawa na kifua kikuu usababishwa na bakteria bali Ukimwi usababisha na virus.

 

2.Watu wanaweza kusema hivyo kwa sababu dalili za awali zinaweza kufanana ila sio kweli kuwa mwenye kifua kikuu ana ukimwi kwa hiyo vipimo ni vya la, lazima ili kuweza kutambua kuwa ni kifua kikuu au ni Maambukizi ya virus vya ukimwi.

 

3.Imani potofu nyingine ni kuwa mwenye kifua kikuu anapaswa kutengwa kwenye jamii.hii ni imani ambayo Watu wanayo kwamba mtu akiwa na kifua kikuu hapaswi kuishi na wengine anapaswa kutengwa na vyombo vyake visichanganywe na vya wengine ili kuepuka kuambukiza wengine.

 

4.Ni kweli kama mtu hajaanza kutumia dawa anaweza kuambukiza wengine kwa hiyo hatupaswi kuwatenga wagonjwa wa kifua kikuu bali tuwapeleke hospitalini wapime na wakianza kutumia dawa baada ya wiki mbili hawaambukiza Watu wengine kwa hiyo hatupaswi kuwatenga bali tuwahudumie kama wagonjwa wengine.

 

5. Kwa hiyo ambacho tunapaswa kujua ni kuwa kifua kikuu kinasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine ila mtu akipata dawa hawezi kuambukiza wengine na pia ugonjwa huu unatibika vizuri sana na jamii isiwatenge wagonjwa hawa kwa sababu nao wanahitaji huduma kama wagonjwa wengine 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 2059

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 ai web app     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni

Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.

Soma Zaidi...
Upungufu wa vyakula na madhara yake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula

Soma Zaidi...
Madhara ya ulevi

Poshi hii inahusu madhara ya ulevi.Utegemezi wa pombe kwa kawaida humaanisha kuwa mtu anatumia kiasi kikubwa cha pombe na kuna masuala kuhusu kupoteza udhibiti.

Soma Zaidi...
Jifunze jinsi ya kumsaidia mwenye kifafa

Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaid

Soma Zaidi...
Aina za vidonda.

Posti hii inahusu zaidi aina kuu za vidonda,kuna aina kuu tatu za vidonda ambapo kila aina utumiwa kwa njia yake kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...