Imani potofu kuhusu kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi imani potofu waliyonayo Watu kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu, hizi ni imani ambazo uwepo kwenye jamii na pengine uweza kuaminika lakini si za ukweli.
Imani potofu kuhusu kifua kikuu.
1.mwenye kifua kikuu ana Maambukizi ya virus vya ukimwi, hii ni mojawapo ya imani ambayo imo miongoni mwao Watu wengi wakiamini kuwa mwenye kifua kikuu ana Maambukizi ya virus vya ukimwi, hii siyo kweli kwa sababu kifua kikuu kinapona ila Ukimwi hauna dawa na kifua kikuu usababishwa na bakteria bali Ukimwi usababisha na virus.
2.Watu wanaweza kusema hivyo kwa sababu dalili za awali zinaweza kufanana ila sio kweli kuwa mwenye kifua kikuu ana ukimwi kwa hiyo vipimo ni vya la, lazima ili kuweza kutambua kuwa ni kifua kikuu au ni Maambukizi ya virus vya ukimwi.
3.Imani potofu nyingine ni kuwa mwenye kifua kikuu anapaswa kutengwa kwenye jamii.hii ni imani ambayo Watu wanayo kwamba mtu akiwa na kifua kikuu hapaswi kuishi na wengine anapaswa kutengwa na vyombo vyake visichanganywe na vya wengine ili kuepuka kuambukiza wengine.
4.Ni kweli kama mtu hajaanza kutumia dawa anaweza kuambukiza wengine kwa hiyo hatupaswi kuwatenga wagonjwa wa kifua kikuu bali tuwapeleke hospitalini wapime na wakianza kutumia dawa baada ya wiki mbili hawaambukiza Watu wengine kwa hiyo hatupaswi kuwatenga bali tuwahudumie kama wagonjwa wengine.
5. Kwa hiyo ambacho tunapaswa kujua ni kuwa kifua kikuu kinasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine ila mtu akipata dawa hawezi kuambukiza wengine na pia ugonjwa huu unatibika vizuri sana na jamii isiwatenge wagonjwa hawa kwa sababu nao wanahitaji huduma kama wagonjwa wengine
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 ai web app 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Kazi ya chanjo ya Surua
Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya Surua kwa watoto, ni Aina ya chanjo ambayo utolewa kwa watoto na kufanya kazi mbalimbali mwilini ambazo ni kumkinga mtoto asipatwe na magonjwa.
Soma Zaidi...Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa Damu kwenye moyo.
 Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo, kitaalamu huitwa Angina ni dalili ya Ugonjwa wa ateri ya Coronary. Ugonjwa huu kawaida hufafanuliwa kama kufinya, shinikizo, uzito, kubana au maumivu kwenye
Soma Zaidi...Upungufu wa vyakula vya madini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu kazi za ini.
Posti hii inahusu zaidi kazi za ini, kwa kawaida tunafahamu kwamba ini ni sehemu muhimu kwenye mwili wa binadamu kwa sababu ni.likikosa kufanya kazi yake maisha ya binadamu yanakuwa hatarini kwa sababu mbalimbali.
Soma Zaidi...Mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu, kama mtu amepoteza fahamu Kuna mambo muhimu yanapaswa kuangaliwa kwa makini kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...