picha

JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript

 

JINSI YA KUWEKA VARIABLE KWENYE JAVASCRIPT.

Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye javascript na kuweza kuzitumia. Pia tutaona kanuni zinazoambatana na variable kwenye javascript.

 

Je variable ni nini?

Variable ni kama chombo kinachohifadhia taarifa. Chukulia mfano una ndoo ambayo ndani yake ina maji, mikate, na mchele. Hapa ndoo ni variable ambayo inahifadhi. Ama mfano kusema x inawakilisha 8. hapa x ni variable ambayo inahifadhi 8.

 

Variable hutambulika kwa jina lake ambalo halitakiwi lijirudie tena kuwakilisha variable nyingine. Jina hili ni unique ambalo hutambulika kama identifier.  Variable inatakiwa iwe na zifa zifuatazo:-

  1. Jina hili linaweza kuwa na herufi, namba, underscore (_) na alama ya dola ($)
  2. jina lazima lianze na herufi au alama ya dola ($) au underscore (_)
  3. jina linatakiwa lizingatiwe matumizi ya herufi kubwa na ndogo. kwani katika javascript juma na JUMA ni majina mawili tofauti.
  4. majina yote ambayo ni javascript keyword hayaruhusiwi kwenye variable. Tumezungumzia kuhusu keyword kwenye somo lililotangulia.

 

Namna ya kuipa thamani javascript

Tunatumia alama ya = ili kuipa thamani variable. Kwenye javascript alama hii huitwa assignment operator na sio alama ya sawasawa kama ilivyo kwenye hesabu.

 

Kuna njia kuu tatu ambazo hutumika kwenye javascript ili kuipa variable thamani yake. Njia hizo ni kwa kutumia keyword kama:-

  1. var
  2. let
  3. const

 

1. Kwa kutumia var:

Hii hutumika pale unapotaka kuweka variable ambayo itaweza kutumiaka kwenye ukurasa mzima wenye block code nyingi yaani globally. Block code tulisha izungumzia katika masomo yaliyopita.

 

Mfano 1:

<script>

   var bc = "www.bongoclass.com";

   document.write(bc)

</script>

 

Hii itakupa matokeao haya:

Mfano 2

<script>

   var x = 2;

   var X = 3;

   document.write(x + X)

</script>

Hii itakupa matokeo haya

2. Kwa kutumia let

Let hutumika kuipa thamani variable ambayo itatumika ...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: JavaScript Main: Masomo File: Download PDF Views 868

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 ai web app     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.

Soma Zaidi...
Game 3: Mchezo wa kufikiria namba kwa kutumia javascript

Hii ni game ambayo utafikiria namba, ambayo inatakiwa iwe sawa na namba ambayo game imeiweka.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 12: Function zinazotumika kwenye namba

Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 17: condition statement za if else, else if kwenye javascript

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.

Soma Zaidi...