picha

JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript

 

JINSI YA KUWEKA VARIABLE KWENYE JAVASCRIPT.

Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye javascript na kuweza kuzitumia. Pia tutaona kanuni zinazoambatana na variable kwenye javascript.

 

Je variable ni nini?

Variable ni kama chombo kinachohifadhia taarifa. Chukulia mfano una ndoo ambayo ndani yake ina maji, mikate, na mchele. Hapa ndoo ni variable ambayo inahifadhi. Ama mfano kusema x inawakilisha 8. hapa x ni variable ambayo inahifadhi 8.

 

Variable hutambulika kwa jina lake ambalo halitakiwi lijirudie tena kuwakilisha variable nyingine. Jina hili ni unique ambalo hutambulika kama identifier.  Variable inatakiwa iwe na zifa zifuatazo:-

  1. Jina hili linaweza kuwa na herufi, namba, underscore (_) na alama ya dola ($)
  2. jina lazima lianze na herufi au alama ya dola ($) au underscore (_)
  3. jina linatakiwa lizingatiwe matumizi ya herufi kubwa na ndogo. kwani katika javascript juma na JUMA ni majina mawili tofauti.
  4. majina yote ambayo ni javascript keyword hayaruhusiwi kwenye variable. Tumezungumzia kuhusu keyword kwenye somo lililotangulia.

 

Namna ya kuipa thamani javascript

Tunatumia alama ya = ili kuipa thamani variable. Kwenye javascript alama hii huitwa assignment operator na sio alama ya sawasawa kama ilivyo kwenye hesabu.

 

Kuna njia kuu tatu ambazo hutumika kwenye javascript ili kuipa variable thamani yake. Njia hizo ni kwa kutumia keyword kama:-

  1. var
  2. let
  3. const

 

1. Kwa kutumia var:

Hii hutumika pale unapotaka kuweka variable ambayo itaweza kutumiaka kwenye ukurasa mzima wenye block code nyingi yaani globally. Block code tulisha izungumzia katika masomo yaliyopita.

 

Mfano 1:

<script>

   var bc = "www.bongoclass.com";

   document.write(bc)

</script>

 

Hii itakupa matokeao haya:

Mfano 2

<script>

   var x = 2;

   var X = 3;

   document.write(x + X)

</script>

Hii itakupa matokeo haya

2. Kwa kutumia let

Let hutumika kuipa thamani variable ambayo itatumika ...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: JavaScript Main: Masomo File: Download PDF Views 913

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 ai web app     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard

Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 15: Jinsi ya kukusanya user input

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.

Soma Zaidi...
Game 1: Jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawili kwa kutumia html, css na javascript

Katika post hii utakwenda kujifundisha jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawii kwa utumia html, css na javascript

Soma Zaidi...