JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript
JINSI YA KUWEKA VARIABLE KWENYE JAVASCRIPT.
Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye javascript na kuweza kuzitumia. Pia tutaona kanuni zinazoambatana na variable kwenye javascript.
Je variable ni nini?
Variable ni kama chombo kinachohifadhia taarifa. Chukulia mfano una ndoo ambayo ndani yake ina maji, mikate, na mchele. Hapa ndoo ni variable ambayo inahifadhi. Ama mfano kusema x inawakilisha 8. hapa x ni variable ambayo inahifadhi 8.
Variable hutambulika kwa jina lake ambalo halitakiwi lijirudie tena kuwakilisha variable nyingine. Jina hili ni unique ambalo hutambulika kama identifier. Variable inatakiwa iwe na zifa zifuatazo:-
- Jina hili linaweza kuwa na herufi, namba, underscore (_) na alama ya dola ($)
- jina lazima lianze na herufi au alama ya dola ($) au underscore (_)
- jina linatakiwa lizingatiwe matumizi ya herufi kubwa na ndogo. kwani katika javascript juma na JUMA ni majina mawili tofauti.
- majina yote ambayo ni javascript keyword hayaruhusiwi kwenye variable. Tumezungumzia kuhusu keyword kwenye somo lililotangulia.
Namna ya kuipa thamani javascript
Tunatumia alama ya = ili kuipa thamani variable. Kwenye javascript alama hii huitwa assignment operator na sio alama ya sawasawa kama ilivyo kwenye hesabu.
Kuna njia kuu tatu ambazo hutumika kwenye javascript ili kuipa variable thamani yake. Njia hizo ni kwa kutumia keyword kama:-
- var
- let
- const
1. Kwa kutumia var:
Hii hutumika pale unapotaka kuweka variable ambayo itaweza kutumiaka kwenye ukurasa mzima wenye block code nyingi yaani globally. Block code tulisha izungumzia katika masomo yaliyopita.
Mfano 1:
<script>
var bc = "www.bongoclass.com";
document.write(bc)
</script>
Hii itakupa matokeao haya:
Mfano 2
<script>
var x = 2;
var X = 3;
document.write(x + X)
</script>
Hii itakupa matokeo haya
2. Kwa kutumia let
Let hutumika kuipa thamani variable ambayo itatumika ...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 12: Function zinazotumika kwenye namba
Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method
Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 10: Jinsi ya kuandika object na matumizi yake kwenye javascript
Ksomo hili litakwenda kukufundisha kuhusu object kwenye javascript, kazi zake na sheria zake katika kuiandika.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
Soma Zaidi...