picha

JAVASCRIPT - somo la 10: Jinsi ya kuandika object na matumizi yake kwenye javascript

Ksomo hili litakwenda kukufundisha kuhusu object kwenye javascript, kazi zake na sheria zake katika kuiandika.

Katika post hii tutajifunza kuhusu javascript object. Utajifunza jinsi ya kutengeneza javascript object. Pia tutajifunza kuhusu kutimia method kwenye javascript. 

 

Object ni nini?

Object ni data ambayo ina sifa na tabia (property). Mfano unaposema gari linakuwa na sifa kama rangi,  mwendo kasi, aina ya injini. Hivyo kwa mfano huu gari ni object ambayo inaweza kuandikwa kama hivi: 

 

<script>

  var gari={

  jina: "Toyota",

  injini: "Disel",

  speed: "180kh/h",

  manufacture:"Japan"

  }

  

  document.write(gari.jina +"<br>"+

  gari.speed +"<br>"+

  gari.injini +"<br>"+

  gari.manufacture

  );

</script>

Ukiangalia code hizo utagundua kuwa:-

  1. OBJECT ni variable kama unavyoona hapo bar gari, ambapo OBJECT yetu ni gari ambayo ni variable

 

  1. OBJECT ina jina la OBJECT na thamani ama sifa zake kwa mfano hapo jina ni gari na sifa zake ni mwendo, injini, manufacture, jina la gari. 

 

  1. Jina la OBJECT linaitwa object name, na hizo sifa huitwa object property au behaviour na hizo thamani kwa mfano Toyota, dizel, 180kh/h hizo zote huitwa property values. 

 

  1. Kutoka property moja kwenda nyingine hutenganishwa na alama ya koma (,).

 

  1. Property na value yake kutenganishwa na alama ya nukta pacha (:)

 

 

Jinsi ya kuandika OBJECT katika javascript.

  1. Utaweka jina la object. Jina hili halitakiwibkuanza na namba ama special character wala javascript keywords

 

  1. Kisha utaweka jina la object likifuatiwa na mabano {}

 

  1. Ndani ya mabano ndio utaweka hizo property zake. 

 

  1. Kuandika property ataandika. Jina la hiyo property ikifuatiwa na alama ya nukta pacha kisha itafuatiwa na value. Kama ni string utaweka ndani ya alama za "".

 

Mfano: 

<script>

  var tovuti={

  jina: "Bongoclass",

  umri: 4,

  nchi: "Tanzania",

  hai:true,

  mafunzo: ["html", "php", "javascript", "sql"]

  }

 

  document.write(tovuti["jina"] +"<br>"+tovuti.mafunzo[0] +" "+tovuti.mafunzo[1])

</script>

Katika mfano huo hapo utagundua kuwa object inaweza kuwa na array ndani yake kwa mfano hapo juu property mafunzo value zake zipo kwenye array. 

 

Si hivyo tu bali object pia inaweza kuwa na function kama tutakavyoona katika mifano inayokuja. 

 

 

Jinsi ya ku access object

Ku access object ni sawa na kuitumia hiyo objectvkwenye code zako. Kwa nfano katika mifano miwili iliyotangulia baada ya kuandika object tuliweza kuzitumia na ku out put code ndipo tukapata matokeo ya hizo code. 

 

Kuna njia kuu tatu ambazo hutumika ku access object. Yaani njia tatu ambazo hutumika ili uweze kuitumia object kwenye code zako. Njia hizo ni: -

  1. Kwa kutumia doti. Kama tulivyoona katika mfano wa kwanza gari.jina

 

  1. Njia ya pili ni kwa kutumia mabango kama ilivyo katika mfano wa pili tovuti[jina]

 

  1. Njia ya tatu ni kwa kutumia this keyword kama tutakavyojifunza. 

 

  1. KWA KUTUMIA DOTI

ili uweze ku access object kwa kutumia doti kwanza utaandika jina la hiyo Object kisha itafuatiwa na kidoti kisha ndipo itafanya jina la property. 

 

Mfano: 

<script>

  var mafunzo={

  somo: "Javascript",

  muda: "wiki mbili",

  lugha: "kiswahili",

  host:"Bongoclass"

  }

  

  alert("Je upo tayari kujiunga na mafunzo ya"+mafunzo.somo+ "yatakayotolewa"+mafunzo.host+"kwa muda wa"+mafunzo.muda+"kwa lugha ya"+mafunzo.lugha)

</script>

 

2.KWA KUTUMIA MABANO []

Kutumia njia hii kwanza utaweka jina ka object kisha litafuatiea na mabano,  ndani ya mabano utaweka jina la hiyo property. Zingatia kama ni string kuiweka ndani ya alama za ""

 

Mfano: 

 

<p id="demo"></p>

<script>

  var mafunzo={

  somo: "Javascript",

  muda: "wiki mbili",

  lugha: "kiswahili",

  host:"Bongoclass"

  }

document.getElementById("demo").innerHTML="karibu" + mafunzo["host"] + "upate mafunzo ya" + mafunzo["somo"]+ "yatakayifanyika kwa muda wa" + mafunzo["muda"] + "kwa lugha ya" + mafunzo["lugha"];

</script>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-20 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 1153

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 web hosting    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css

Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard

Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 12: Function zinazotumika kwenye namba

Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 18: Jinsi ya kutumia switch case kwenye javascript

Kwa kutumia mfano huu na iliyotangulia unaweza kuweka masharti kadiri uwezavyo. Tukutane somo linalofuata tutajifunza kuhusu switch statement.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop

Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript

Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 15: Jinsi ya kukusanya user input

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript.

Soma Zaidi...