JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo
JAVASCRIPT FUNCTIONS:
Function ni kundi la code ambalo unaweza kulitumia zaidi na zaidi. Na hata hivyo function haiwezi kufanyakazi hata mpaka iwe imeitwa (invoked/called).
Function zipo katika namna mbili ambazo ni built in functions na user defined functions. Hizi built in function ni zile ambazo zimetengenezwa moja kwa moja na walioivumbuwa hii language. Na Usher defined function ni zile ambazo mtumiaji anazitengeneza yeye mwenyewe.
Jinsi ya kutengeneza function:
Iili kuweza kuandika function javascript hutumia keyword function kisha hufuatiwa na jina la function kisha hufuatiwa na mabano () ambayo ndani yake kunakaa parameta. Endapo zitakuwepo parameta zaidi ya moja utazitenganisha na alama ya kima, baada ya kuweka hayo mabano yenye parameta utaweka mabano mengine hay {} ambayo ndani yake ndio hukaa hizo cede za function yako.
Wacha tuone mifano ya functiona hapo chini: -
Mfano 1:
<!DOCTYPE html>
<html>
<head>
<title> Mfano wa 1 </title>
</head>
<body>
<script>
/* Mwanzo wa function */
function karibu(str) {
/* Code za function hukaa hapa */
document.write("Karibu Bongoclass");
}
/* Hapa ndipo utaiita function */
karibu();
</script>
</body>
</html>
Mfano 2:
Katika function pia tunaweza kutumia return keyword. Hii hutumika pale unapotaka kupata thamani ya fulani kutoka kwenye function yako.
Kwa mfano unafanya usajili wa watoto, hivyo unataka kuandika jina la mtoto, la bana ama ukoo pamoja na kabila lake. Unaweza kutumia return keyword ili kupata taarifa za mtoto huyu.
Keyword hii hasa hutumika kustop code zisiendelee ku run kisha huleta matokeo ya code hizo popote pale zilipoitwa.
<!DOCTYPE html>
...Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 10: Jinsi ya kuandika object na matumizi yake kwenye javascript
Ksomo hili litakwenda kukufundisha kuhusu object kwenye javascript, kazi zake na sheria zake katika kuiandika.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 17: condition statement za if else, else if kwenye javascript
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia.
Soma Zaidi...Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css
Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player
Soma Zaidi...