Ifahamu dawa ya isoniazid katika kupambana na ugonjwa wa TB

Post hii inahusu zaidi dawa ya isoniazid katika mapambano na kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu ni hatari katika jamii kwa hiyo dawa ya isoniazid ni mkombozi katika mapambano na kifua kikuu.

Dawa ya isoniazid katika kupambana na kutibu kifua kikuu.

1.  Dawa ya isoniazid ni mojawapo ya dawa inayosaidia katika matibabu ya kutibu kifua kikuu kwa sababu utibu kifua kikuu ikiwa imechanganyikana na dawa nyingine kama vile Rifampin, pyrazinamide na ethambutol, pia dawa hii utumika kwenye daraja la kwanza la matibabu ya kutibu kifua kikuu ikiwa na Rifampin, pyrazinamide na ethambutol zikiwa na muundo wa RHZE ambapo H inawakilisha isoniazid na katika daraja la pili inakuwa ni Rifampin na isoniazid ambapo muundo wake ni RH ambapo R ni Rifampin na H ni isoniazid.

 

2. Tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu usababishwa na bakteria ambaye kwa kitaamu huiitwa  mycobacterium tuberculosis, kwa hiyo kazi ya isoniazid ni kuzuia ukuaji wa bakteria Huyu na hatimaye bakteria usinyaa na ugonjwa hauwezi kuendelea kuwepo ikiwa dawa inatumika vizuri pia dawa hii inazuia kuzalishwa kwa Ganda la juu la mdudu huyu ambaye usababisha kifua kikuu na kwa hiyo mdudu kama Hana gamba la juu hawezi kuendelea kuwepo pia dawa hii Ina uwezo wa kuharibu protein ya mdudu Huyu protein hiyo kwa kitaamu huiitwa DNA.

 

3. Kwa kawaida aina hii ya protein ambayo inaitwa DNA ndiyo Ina mafuta ( lipis) wanga (carbohydrates) na virutubisho vyote vya mdudu Huyu anayesababisha kifua kikuu kwa hiyo kazi ya isoniazid ni kuharibu hiyo protein na hiyo protein kwa sababu Ina virutubisho vyote na ikishaharibiwa hakuna maisha ya bakteria huyo na ugonjwa upungua na hatimaye kutoweka kabisa kwa sababu ya kazi ya isoniazid. Kwa hiyo hui ndio uwezo mkubwa uliopo kwenye dawa hii ya isoniazid kwa watumiaji kuweni Ms Imani kwa sababu dawa hii ufanya mambo makubwa katika kupambana na bakteria.

 

4. Kwa kawaida na mara nyingi dawa hii huwa katika mfumo wa vidonge kwenye muunganiko na dawa nyingine na kwa hiyo umezwa na maji na pia kwa wakati mwingine inaweza kutolewa kupitishia kwenye damu na pia kwenye nyama ikiwezekana na kwa uhitaji maalumu kadri ya maoni ya wataalamu wa afya, katika dawa za kutibu kifua kikuu dawa hii ya isoniazid uuua asilimia tisini na tisa ya bakteria ndani ya siku chache kwa hiyo utumika kwenye daraja la kwanza na la pili kwa sababu ya kuua kiwango kikubwa cha bakteria kwa siku chache.

 

5. Pia dawa hii inatumika kwa wagonjwa wenye maambukizi mbalimbali ya virus vya ukimwi, hasa kwa wale ambao ndio wanaanza matibabu ingawa hawana ugonjwa wa Kifua kikuu, utumika dawa hizi Ili kuwakinga na hatari ya kuwa na maambukizi kwa sababu wagonjwa wa maambukizi ya ukimwi Wana kiwango kidogo cha kinga mwilini pia na kifua kikuu Kina tabia ya kuwapata watu wenye kinga ndogo ya mwili. Pia kwa wale wagonjwa wenye ukoma nao pia Wana tabia ya kuwa na kinga ndongo ya mwili kwa hiyo nao pia upatiwa dawa ya isoniazid Ili kuweza kuwakinga na kupata maambukizi ya kifua kikuu kwa sababu ya kuwepo kwa kinga ndongo ya mwili.

 

6. Kwa hiyo sio kwamba wagonjwa wanaopewa dawa ya kifua kikuu ya isoniazid ni wagonjwa wa Kifua kikuu Bali wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa Kifua kikuu wanapewa kama kinga, kwa hiyo dawa hii inaweza kutumiwa na wagonjwa waliotayari na maambukizi ya kifua kikuu pia na wale walio katika hatari ya kupata kifua kikuu, kwa hiyo wale wenye aleji na dawa hii hawapaswi kuitumia au kwa wale wanaoanza matibabu wakiona maudhi madogo madogo yamezidi na kuwa si ya kawaida ni vizuri kuomba msaada kwa wataalamu wa afya.

 

7. Dawa hii ya isoniazid Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea wakati wa kutumia maudhi hayo ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, kuharibu, maumivu ya kichwa, kuwepo kwa homa, kuwepo kwa vidonda vidogo vidogo kwenye mwili na matumizi ya mda mrefu ya dawa hii usababisha matatizo kwenye nefron,na pengine kwenye ini na kusababisha homa ya ini na nikwa kiwango kidogo na kwa watu wachache,kwa hiyo hayo ni maudhi madogo madogo ila yakiongezeka na kuwa yasiyo ya Kawaida ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya.

 

8. Pia dawa hii haiitumiki kiholela ni kwa maoni ya wataalamu wa afya na pia kabla ya kutumia dawa hii ni vizuri kabisa kupima kwanza ugonjwa na ndipo uanze kutumia dawa hii na pia kwa wale wanaotumia dawa hii kama tiba wasijisikiea vibaya hii ni dawa ya knga hasa kwa wale walio kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa Kifua na ukoma wakumbuke kwamba wanatumia kwa mda na watapumzika kwa sababu ugonjwa huu unapona na ni wengi wametibiwa na kupona na pia waliokwisha patw ugonjwa huu ni vizuri kabisa wakazingatia matibabu kwa Sababu ugonjwa huu unatibika.

 

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/12/16/Friday - 10:46:11 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 577

Post zifazofanana:-

Parachichi (avocado)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za parachichi Soma Zaidi...

Alif lela ulela
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Faida za mbegu za maparachichi.
Posti hii inahusu zaidi faida za mbegu za maparachichi, kwa kawaida tunajua wazi faida za maparachichi pamoja na faida za maparachichi kuna faida kubwa katika mbegu zake kama tutakavyoona Soma Zaidi...

Kazi za wahudumu wa afya wakati wa kutoa dawa kwa wagojwa
Hii post inahusu zaidi kazi za wahudumu wa afya wakati wa kutoa dawa, ni kanuni zinazopaswa kufuata wakati wa kutoa dawa kwa wagojwa. Soma Zaidi...

Huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum.
Posti hii inahusu huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum, ni wanawake ambao wana shida ya akili, walionyanyaswa kijinsia, wakimbizi na wote wenye matatizo mbalimbali. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za spinachi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula spinach Soma Zaidi...

Umoja wa mataifa unazungumziaje afya
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo ya kiafya yanayozungumzwa na umoja wa mataifa Soma Zaidi...

Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)
Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa. Soma Zaidi...

Matibabu ya vidonda vya tumbo
Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu. Soma Zaidi...

Nina shida hiyo maumivu chini ya tumbo upande wa kushoto na mkojo wa kahawia sana na unatoa arufu
Kama unapatwa na maumivu ya tumbo na ilhali mkojo ni mchafu, ama una harufu sana, basi post hii ni kwa ajili yako. Soma Zaidi...

Kutokwa maji yan seminal swhemu za siri kwa mwanamke nidalili ya ugojwa gan?
Kutokwa Majimaji sehemu za siri kwa mwanamke sio jambo la kushangaza na kuhisivunaumwa. Majimajivhaya ndio huboresha afya ya uzazi kwa kusafisha na kulinda via vya uzazi. Lakini majimajivhaya yakiwa mengi, ama yanawasha ama yanaharufu haa ndipo kwenye tat Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kunywa maziwa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kunywa maziwa Soma Zaidi...