Ifahamu dawa ya isoniazid katika kupambana na ugonjwa wa  TB

Ifahamu dawa ya isoniazid katika kupambana na ugonjwa wa TB

Post hii inahusu zaidi dawa ya isoniazid katika mapambano na kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu ni hatari katika jamii kwa hiyo dawa ya isoniazid ni mkombozi katika mapambano na kifua kikuu.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Dawa ya isoniazid katika kupambana na kutibu kifua kikuu.

1.  Dawa ya isoniazid ni mojawapo ya dawa inayosaidia katika matibabu ya kutibu kifua kikuu kwa sababu utibu kifua kikuu ikiwa imechanganyikana na dawa nyingine kama vile Rifampin, pyrazinamide na ethambutol, pia dawa hii utumika kwenye daraja la kwanza la matibabu ya kutibu kifua kikuu ikiwa na Rifampin, pyrazinamide na ethambutol zikiwa na muundo wa RHZE ambapo H inawakilisha isoniazid na katika daraja la pili inakuwa ni Rifampin na isoniazid ambapo muundo wake ni RH ambapo R ni Rifampin na H ni isoniazid.

 

2. Tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu usababishwa na bakteria ambaye kwa kitaamu huiitwa  mycobacterium tuberculosis, kwa hiyo kazi ya isoniazid ni kuzuia ukuaji wa bakteria Huyu na hatimaye bakteria usinyaa na ugonjwa hauwezi kuendelea kuwepo ikiwa dawa inatumika vizuri pia dawa hii inazuia kuzalishwa kwa Ganda la juu la mdudu huyu ambaye usababisha kifua kikuu na kwa hiyo mdudu kama Hana gamba la juu hawezi kuendelea kuwepo pia dawa hii Ina uwezo wa kuharibu protein ya mdudu Huyu protein hiyo kwa kitaamu huiitwa DNA.

 

3. Kwa kawaida aina hii ya protein ambayo inaitwa DNA ndiyo Ina mafuta ( lipis) wanga (carbohydrates) na virutubisho vyote vya mdudu Huyu anayesababisha kifua kikuu kwa hiyo kazi ya isoniazid ni kuharibu hiyo protein na hiyo protein kwa sababu Ina virutubisho vyote na ikishaharibiwa hakuna maisha ya bakteria huyo na ugonjwa upungua na hatimaye kutoweka kabisa kwa sababu ya kazi ya isoniazid. Kwa hiyo hui ndio uwezo mkubwa uliopo kwenye dawa hii ya isoniazid kwa watumiaji kuweni Ms Imani kwa sababu dawa hii ufanya mambo makubwa katika kupambana na bakteria.

 

4. Kwa kawaida na mara nyingi dawa hii huwa katika mfumo wa vidonge kwenye muunganiko na dawa nyingine na kwa hiyo umezwa na maji na pia kwa wakati mwingine inaweza kutolewa kupitishia kwenye damu na pia kwenye nyama ikiwezekana na kwa uhitaji maalumu kadri ya maoni ya wataalamu wa afya, katika dawa za kutibu kifua kikuu dawa hii ya isoniazid uuua asilimia tisini na tisa ya bakteria ndani ya siku chache kwa hiyo utumika kwenye daraja la kwanza na la pili kwa sababu ya kuua kiwango kikubwa cha bakteria kwa siku chache.

 

5. Pia dawa hii inatumika kwa wagonjwa wenye maambukizi mbalimbali ya virus vya ukimwi, hasa kwa wale ambao ndio wanaanza matibabu ingawa hawana ugonjwa wa Kifua kikuu, utumika dawa hizi Ili kuwakinga na hatari ya kuwa na maambukizi kwa sababu wagonjwa wa maambukizi ya ukimwi Wana kiwango kidogo cha kinga mwilini pia na kifua kikuu Kina tabia ya kuwapata watu wenye kinga ndogo ya mwili. Pia kwa wale wagonjwa wenye ukoma nao pia Wana tabia ya kuwa na kinga ndongo ya mwili kwa hiyo nao pia upatiwa dawa ya isoniazid Ili kuweza kuwakinga na kupata maambukizi ya kifua kikuu kwa sababu ya kuwepo kwa kinga ndongo ya mwili.

 

6. Kwa hiyo sio kwamba wagonjwa wanaopewa dawa ya kifua kikuu ya isoniazid ni wagonjwa wa Kifua kikuu Bali wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa Kifua kikuu wanapewa kama kinga, kwa hiyo dawa hii inaweza kutumiwa na wagonjwa waliotayari na maambukizi ya kifua kikuu pia na wale walio katika hatari ya kupata kifua kikuu, kwa hiyo wale wenye aleji na dawa hii hawapaswi kuitumia au kwa wale wanaoanza matibabu wakiona maudhi madogo madogo yamezidi na kuwa si ya kawaida ni vizuri kuomba msaada kwa wataalamu wa afya.

 

7. Dawa hii ya isoniazid Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea wakati wa kutumia maudhi hayo ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, kuharibu, maumivu ya kichwa, kuwepo kwa homa, kuwepo kwa vidonda vidogo vidogo kwenye mwili na matumizi ya mda mrefu ya dawa hii usababisha matatizo kwenye nefron,na pengine kwenye ini na kusababisha homa ya ini na nikwa kiwango kidogo na kwa watu wachache,kwa hiyo hayo ni maudhi madogo madogo ila yakiongezeka na kuwa yasiyo ya Kawaida ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya.

 

8. Pia dawa hii haiitumiki kiholela ni kwa maoni ya wataalamu wa afya na pia kabla ya kutumia dawa hii ni vizuri kabisa kupima kwanza ugonjwa na ndipo uanze kutumia dawa hii na pia kwa wale wanaotumia dawa hii kama tiba wasijisikiea vibaya hii ni dawa ya knga hasa kwa wale walio kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa Kifua na ukoma wakumbuke kwamba wanatumia kwa mda na watapumzika kwa sababu ugonjwa huu unapona na ni wengi wametibiwa na kupona na pia waliokwisha patw ugonjwa huu ni vizuri kabisa wakazingatia matibabu kwa Sababu ugonjwa huu unatibika.

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1135

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu dawa ya pyrantel pamoate
Fahamu kuhusu dawa ya pyrantel pamoate

Post hii inahusu zaidi dawa ya pyrantel pamoate ni dawa ambayo usaidia kutibu minyoo ambayo kwa kawaida ukaa kwenye utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
   Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo paracetamol.
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo paracetamol.

Paracetamol kwa jina kingine hujulikana kama(acetaminophen) ni dawa ya kawaida ya kutuliza maumivu ambayo hutumiwa kupunguza aina mbalimbali za maumivu. Paracetamol ndilo jina linalojulikana zaidi katika kutuliza maumivu ya kawaida. Paracetamol inajulik

Soma Zaidi...
Dawa za Anesthesia katika kutuliza maumivu.
Dawa za Anesthesia katika kutuliza maumivu.

Unapotaka kufanyiwa baadhi ya matibabu unatakiwa kupewa ganzi ama nusu kaput ili kulifanyia usihisi maumivu. Dawa hizi zinajulikana na Anesthesia.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa
Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa

Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.

Soma Zaidi...
 Fahamau madhara ya flagyl (Metronidazole)
Fahamau madhara ya flagyl (Metronidazole)

Flagyl ni nini? Flagyl (metronidazole) ni antibiotic. Inapigana na bakteria katika mwili wako. Flagyl hutumiwa kutibu maambukizo ya bakteria ya uke, tumbo, ngozi, viungo na njia ya upumuaji.

Soma Zaidi...
Tiba ya minyoo
Tiba ya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tiba ya minyoo

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones/quinolones
Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones/quinolones

Post hii inahusu dawa ya kupambana na bakteria, hili kundi la fluoroquinolones lina dawa kuu mbili ambazo ni ciprofloxin na ofloxacin.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu mapunye
Dawa ya kutibu mapunye

DAWA YA MAPUNYEMatibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo.

Soma Zaidi...
  Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.

Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya ketoconazole.
Fahamu kuhusu dawa ya ketoconazole.

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya ketoconazole ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye koo.

Soma Zaidi...