Fahamu kuhusu dawa ya marcolides dawa ya kuuwa bakteria, kwenye mfumo wa hewa
Post hii inahusu zaidi dawa ya macrolide ni mojawapo ya dawa ya kutibu au kupambana na bakteria na upambana na bakteria wafuatao streptococcus pyogenes, staphylococcus aureus na haihusiki na haemophilia influenza ambao usababisha maambukizi kwenye mfumo w
Fahamu kuhusu dawa ya macrolide
1. Dawa hii ya macrolide ni dawa ambayo Ina dawa nyingine ndani yake kama vile azithromycin, erythromycin na clarithromysin ambazo kwa pamoja upambana na bakteria ambao tumeweza kuwaona hapo juu.
2. Dawa hii kwa sababu ya mkusanyiko wa dawa zaidi ya Moja kwa hiyo usaidia kwenye matibabu ya maambukizi ya bakteria ndani ya sikio, kwenye miwasho na viupele vya mwilini, pia utibu kikohozi, usaidia kwenye minyoo ya tumboni ambayo Kwa kitaamu huiitwa intestinal ameobiasis, kwenye maambukizi ya kwenye mlango wa kizazi kwa kitaamu huiitwa pelvic inflammatory diseases, pia usaidia kwenye matibabu ya kaswende na kisonono.
3. Pia dawa hizi mara nyingi huwa kwenye mfumo wa vidonge kwa hiyo zinapotumiwa uenda Moja kwa moja kwenye mmengenyo wa chakula na pia kuingia kwenye mzunguko wa damu na hatimaye kuingia kwenye sehemu mbalimbali ambapo Kuna bakteria na kuanza mashambulizi na pia dawa hizi zinaweza kuingia kwenye maji maji ambayo yapo kwenye ubongo na kweye mfumo wa fahamu kwa kitaamu huiitwa central nerve system na pia dawa zinaweza kuingia kwenye plasenta au kondo la nyuma na kuweza kuuua bakteria walioma ndani.
4. Dawa hii ya macrolide haipaswi kutumiwa na watu wenye aleji na dawa hiyo na pia dawa hizi hazipaswi kutumiwa kabisa na watu wenye magonjwa ya ini na pia zitumiwe kwa uangalifu kwa wenye matatizo ya Figo, mimba changa na wale watumiaji wa pombe Kali wanapotumia dawa hizi wanapaswa kuacha kutumia kabisa pombe. Kwa wale wenye mimba changa dawa hizi zinaweza kutoa mimba,na kwa wale wagonjwa wa ini dawa hizi uwezo wa kuongeza sumu upo mkubwa mno na pia kwa wale wenye tatizo la Figo ni vizuri kunywa maji mengi endapo watatumia dawa hizi.
5. Vile vile dawa hizi zina matokeo mbalimbali kama vile kichefuchefu na kutapika maumivu ya tumbo na kichwa na pengine maupeke na miwasho.
Pia dawa hizi zinapaswa kutumika kwa uwepo wa uangalizi wa wa wataalamu wa afya sio kutumia dawa hii kiholela to.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 ai web app 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Fahamu kuhusu dawa ya ALU au kwa lugha nyingine ni dawa ya mseto
Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya propranolol ambayo hutibu magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya propranolol katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii ipo kwenye kundi la beta blockers na ufanya Kazi mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya kutibu maumivu ya mgongo (back none pain) na kiuno
Fahamu dawa ya back bone pain kwa matibabu ya mgongo, ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza maumivu ya mgongo.
Soma Zaidi...Dawa ya fangasi ukeni
Usisumbuliwe tene na fangasi ukeni, zijuwe hapa dalili za fangasi ukeni, tiba yake na njia za kukabiliana na fangasi ukeni
Soma Zaidi...Fahamu dawa za 5-fluorouracil,Tegafur na uracili
Post hii inahusu zaidi dawa za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa.
Soma Zaidi...