Dawa ya Carvedilol na kazi yake.

Dawa ya Carvedilol na kazi yake.

Posti hii inahusu zaidi dawa ya Carvedilol na kazi yake, ni dawa inayotibu au kuzuia mapigo ya moyo ambayo yako juu na kusababisha kulegeza kwa mishipa ya moyo.

Kazi ya Carvedilol.

1. Dawa ya Carvedilol ni mojawapo ya Dawa ambazo usaidia kushusha presha kama iko juu , ufanya kazi hii kwa kuhakikisha kwamba mishipa ya moyo imelegezwa kwa sababu mishipa ya moyo kama imebana usababisha presha kuwa juu kwa hiyo dawa hii ikitumika usababisha mishipa kuregea na mapigo ya moyo kuwa kawaida.

 

2.pia dawa hii inatabia ya kushusha sukari, kwa hiyo mgonjwa wa matatizo ya moyo kabla ya kutumia Dawa hii anapaswa kupima kiwango cha sukari mwilini, kama iko chini hapaswi kutumia kwa sababu anaweza kushusha zaidi, kwa hiyo watu wenye matatizo ya sukari kushuka wanapaswa kuwa makini.

 

3.Dawa hii pia usaidia kuzuia kupatwa kwa ghafla ugonjwa wa moyo ambao kwa kitaalamu huitwa heart attack, ambapo mgonjwa uwea kuzimia ghafla na pengine kupoteza fahamu, pamoja na kuwepo kwa dawa hii ya Carvedilol kuna dawa Ambazo ufanya kazi kama ya Carvedilol ambazo ni Atenolo, propanol and labetalo, kwa hiyo dawa hizi zisitumike kiholela zinapaswa kutumika kwa ushauri wa daktari na wataalamu wengine wa afya.

 

4. Katika kutumia dawa hizi kuna maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kama vile  kizungu Zungu, mwili mzima kuchoka, kushuka sana kwa mapigo ya moyo, kuharisha kuongezeka kwa uzito, na kushusha sukari, kwa hiyo Mgonjwa akihisi dalili kama hizi anapaswa kujua kuwa ni kwa sababu ya dawa anazozitumia kwa hiyo maudhi mengine ni ya hatari yanapaswa kufanyiwa kazi mapema kama vile presha kushuka kuzidi kiasi kwa sababu hii ni hali ya hatari kwa mgonjwa.

 

5. Dawa hii haipaswi kutumiwa na watu mbalimbali kama vile wenye Asthma kali kwa sababu inaweza kupasua sehemu mbalimbali ambazo zinahusika kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo mwenye presha anapaswa kujua hili kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo kwenye upumuaji, hata mgonjwa anapaswa kuwa wazi pindi hawapo hospitali na inabidi ajieleze wazi ili kuepuka matatizo mengine na jamii inapaswa kujua matumizi mazuri ya Dawa hii.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views: 3796

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 web hosting     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin

Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin

Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kutuliza mishutuko.

Post hii inahusu zaidi dawa ya phenytoin,ni dawa inayotuliza mishutuko mbalimbali inayoweza kutokea kwenye mwili na kutokana na mishutuko hiyo tunaweza kupata kifafa.

Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi ukeni

Usisumbuliwe tene na fangasi ukeni, zijuwe hapa dalili za fangasi ukeni, tiba yake na njia za kukabiliana na fangasi ukeni

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo

Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.

Soma Zaidi...
Mebendazole kama dawa ya kutibu Minyoo.

Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii.

Soma Zaidi...