Dawa ya Carvedilol na kazi yake.
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Carvedilol na kazi yake, ni dawa inayotibu au kuzuia mapigo ya moyo ambayo yako juu na kusababisha kulegeza kwa mishipa ya moyo.
Kazi ya Carvedilol.
1. Dawa ya Carvedilol ni mojawapo ya Dawa ambazo usaidia kushusha presha kama iko juu , ufanya kazi hii kwa kuhakikisha kwamba mishipa ya moyo imelegezwa kwa sababu mishipa ya moyo kama imebana usababisha presha kuwa juu kwa hiyo dawa hii ikitumika usababisha mishipa kuregea na mapigo ya moyo kuwa kawaida.
2.pia dawa hii inatabia ya kushusha sukari, kwa hiyo mgonjwa wa matatizo ya moyo kabla ya kutumia Dawa hii anapaswa kupima kiwango cha sukari mwilini, kama iko chini hapaswi kutumia kwa sababu anaweza kushusha zaidi, kwa hiyo watu wenye matatizo ya sukari kushuka wanapaswa kuwa makini.
3.Dawa hii pia usaidia kuzuia kupatwa kwa ghafla ugonjwa wa moyo ambao kwa kitaalamu huitwa heart attack, ambapo mgonjwa uwea kuzimia ghafla na pengine kupoteza fahamu, pamoja na kuwepo kwa dawa hii ya Carvedilol kuna dawa Ambazo ufanya kazi kama ya Carvedilol ambazo ni Atenolo, propanol and labetalo, kwa hiyo dawa hizi zisitumike kiholela zinapaswa kutumika kwa ushauri wa daktari na wataalamu wengine wa afya.
4. Katika kutumia dawa hizi kuna maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kama vile kizungu Zungu, mwili mzima kuchoka, kushuka sana kwa mapigo ya moyo, kuharisha kuongezeka kwa uzito, na kushusha sukari, kwa hiyo Mgonjwa akihisi dalili kama hizi anapaswa kujua kuwa ni kwa sababu ya dawa anazozitumia kwa hiyo maudhi mengine ni ya hatari yanapaswa kufanyiwa kazi mapema kama vile presha kushuka kuzidi kiasi kwa sababu hii ni hali ya hatari kwa mgonjwa.
5. Dawa hii haipaswi kutumiwa na watu mbalimbali kama vile wenye Asthma kali kwa sababu inaweza kupasua sehemu mbalimbali ambazo zinahusika kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo mwenye presha anapaswa kujua hili kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo kwenye upumuaji, hata mgonjwa anapaswa kuwa wazi pindi hawapo hospitali na inabidi ajieleze wazi ili kuepuka matatizo mengine na jamii inapaswa kujua matumizi mazuri ya Dawa hii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 web hosting 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 ai web app 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Fahamu kuhusu dawa za Doxorubicin na Daunorubicin
Post hii inahusu zaidi dawa za Doxorubicin and Daunorubicin katika kupambana na kansa.
Soma Zaidi...Dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Soma Zaidi...Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu
Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.
Soma Zaidi...Dawa ya Vidonda vya tumbo
Nitakujuza dawa ya kutibu vidonda vya tumbo, na kutibu vidonda vya tumbo sugu
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya Albendazole
Post hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia kutibu minyoo, na pia imefanikiwa sana kadri ya watumiaji wa dawa hiyo.
Soma Zaidi...Dawa ya vidonda vya tumbo
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...