picha

Dawa ya Carvedilol na kazi yake.

Posti hii inahusu zaidi dawa ya Carvedilol na kazi yake, ni dawa inayotibu au kuzuia mapigo ya moyo ambayo yako juu na kusababisha kulegeza kwa mishipa ya moyo.

Kazi ya Carvedilol.

1. Dawa ya Carvedilol ni mojawapo ya Dawa ambazo usaidia kushusha presha kama iko juu , ufanya kazi hii kwa kuhakikisha kwamba mishipa ya moyo imelegezwa kwa sababu mishipa ya moyo kama imebana usababisha presha kuwa juu kwa hiyo dawa hii ikitumika usababisha mishipa kuregea na mapigo ya moyo kuwa kawaida.

 

2.pia dawa hii inatabia ya kushusha sukari, kwa hiyo mgonjwa wa matatizo ya moyo kabla ya kutumia Dawa hii anapaswa kupima kiwango cha sukari mwilini, kama iko chini hapaswi kutumia kwa sababu anaweza kushusha zaidi, kwa hiyo watu wenye matatizo ya sukari kushuka wanapaswa kuwa makini.

 

3.Dawa hii pia usaidia kuzuia kupatwa kwa ghafla ugonjwa wa moyo ambao kwa kitaalamu huitwa heart attack, ambapo mgonjwa uwea kuzimia ghafla na pengine kupoteza fahamu, pamoja na kuwepo kwa dawa hii ya Carvedilol kuna dawa Ambazo ufanya kazi kama ya Carvedilol ambazo ni Atenolo, propanol and labetalo, kwa hiyo dawa hizi zisitumike kiholela zinapaswa kutumika kwa ushauri wa daktari na wataalamu wengine wa afya.

 

4. Katika kutumia dawa hizi kuna maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kama vile  kizungu Zungu, mwili mzima kuchoka, kushuka sana kwa mapigo ya moyo, kuharisha kuongezeka kwa uzito, na kushusha sukari, kwa hiyo Mgonjwa akihisi dalili kama hizi anapaswa kujua kuwa ni kwa sababu ya dawa anazozitumia kwa hiyo maudhi mengine ni ya hatari yanapaswa kufanyiwa kazi mapema kama vile presha kushuka kuzidi kiasi kwa sababu hii ni hali ya hatari kwa mgonjwa.

 

5. Dawa hii haipaswi kutumiwa na watu mbalimbali kama vile wenye Asthma kali kwa sababu inaweza kupasua sehemu mbalimbali ambazo zinahusika kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo mwenye presha anapaswa kujua hili kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo kwenye upumuaji, hata mgonjwa anapaswa kuwa wazi pindi hawapo hospitali na inabidi ajieleze wazi ili kuepuka matatizo mengine na jamii inapaswa kujua matumizi mazuri ya Dawa hii.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 3472

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 web hosting     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Ifahamu dawa ya kupunguza maumivu

Post hii inahusu dawa ya aspirin katika kupunguza maumivu,ni dawa ambayo upunguz maumivu ya Kawaida, kushusha homa na pia usaidia kwenye magonjwa ya moyo hasa kuzuia stroke kama imetokea mda ndani ya masaa ishilini na manne

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya pyrantel pamoate

Post hii inahusu zaidi dawa ya pyrantel pamoate ni dawa ambayo usaidia kutibu minyoo ambayo kwa kawaida ukaa kwenye utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Fahamu Dawa inayotibu minyoo iitwayo albenza (albendazole)

Albenza (albendazole) hutumika kutibu magonjwa ya minyoo ya ndani ikiwa ni pamoja na maambukizi ya minyoo ya tegu. Albenza inafanya kazi kukomesha kuenea kwa maambukizo ya minyoo kwenye chanzo, na kukata chanzo chao cha nishati, na hivyo kuzuia kuenea k

Soma Zaidi...
Vyakula vya wanga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya wanga

Soma Zaidi...
Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria

Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali.

Soma Zaidi...
Dawa ya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za minyoo

Soma Zaidi...