picha

Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu

Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.

Ifahamu dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.

1.​​​​​1.Rifampsini ni mojawapo ya dawa ambayo imo kwenye daraja la kwanza katika matibabu ya kutibu kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba ni bakteria anayesababisha kuwepo kwa kifua kikuu, kwa hiyo dawa aina ya Rifampin inapotumika kitu cha kwanza ni kuharibu protein ambayo inaitwa DNA ni protein ya bakteria kwa hiyo bakteria huyo anakuwa Hana uwezo wa kuishi tena na ugonjwa uweza kuishia hapo kwa sababu DNA iimeshaharibiwa.

 

2. Katika matibabu ya kifua kikuu dawa hii kwa kawaida haitibu yenyewe kama yenyewe Bali huwa na mchanganyiko na madawa mengine ambayo ni isoniazid, pyrazinamide na ethambutol na dozi yake huwa na muundo wa RHZE ambapo, R ni Rifampin, H ni isoniazid, Z ni pyrazinamide na E ni ethambutol kwa hiyo dawa hizo utumika zote kwa pamoja katika matibabu ya kwanza ya kifua kikuu na katika matibabu ya pili Rifampin huwa na isoniazid na muundo wao huwa ni RH ambapo R ni Rifampin na H ni isoniazid .

 

3. Kwa kawaida dawa ya Rifampin utolewa kwa muundo wa vidonge yaana umezwa kwa maji. na ni mara chache mno Kuna Rifampin ambazo utolewa kwenye mishipa ya damu, katika dawa zote za kifua kikuu dawa hii ya Rifampin ndio iliyo na nguvu zaidi na usaidia katika kupambana na bakteria ambaye kwa kitaamu huiitwa TB bacill na pia dawa hii utumika katika daraja la kwanza na la pili katika matibabu ya kutibu kifua kikuu pia ni dawa yenye nguvu kwa sababu uua bakteria wote walio sugu na wote wanaaoanza mashambulizi .

 

4. Dawa hii pia huwa na maudhi madogo madogo katika kutumia, maudhi hayo ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, kuharisha, maumivu ya kichwa,na pia kuwepo kwa homa pia Kuna baadhi ya watu ambao huwa na viupele wanapokuwa wanatumia dawa hii ya Rifampin pia dawa hii inaweza kabisa kusababisha kupunguza kwa kwa kiasi cha aina ya protein ambayo Kwa kitaamu huiitwa platelate ,na pia kwa wakati mwingine kwa watumiaji wa dawa hii usababisha kupungua kwa kiwango cha damu kuganda .

 

5. Kiwango cha kupunguza kwa damu kuganda kwa kitaamu huiitwa clotting factors hali inayosababisha kupunguza kwa damu mwilini na kusababisha  hali Fulani ambayo Kwa kitaamu huiitwa Anaemia,na maudhi haya hayatokei kila mara ni mara chache na kwa watu wachache kwa hiyo watu wasiogope kutumia dawa hii kwa sababu ni sehemu ya matibabu .

 

6. Pia dawa hii inaweza kutumiwa na watu wote ila kwa wale ambao wanatumia uzazi wa mpango wenye vichocheo vya progesterone na oestrogen hawapaswi kutumia dawa hii kwa sababu dawa hii inaingiliana na hizi homoni na kusababisha kushika kwa mimba kwa sababu dawa hii ya Rifampin Ina nguvu kuliko hivi vichocheo kwa hiyo kwa wale wanaotumia dawa za kifua kikuu na pia wanatumia njia yoyote ya uzazi wa mpango wanapaswa kuomba ushauri kwa wataalamu wa afya kwa sababu wanaweza kupata mimba bila kutegemea au wanashauliwa kutumia njia nyingine za uzazi wa mpango kwa sababu ni nyingi.

 

7. Pia na akina Mama wenye maambukizi ya kifua kikuu na wamegundulika siku za mwisho karibia na kujifungua na kwa bahati mbaya na watoto au mtoto aliyezaliwa na yeye ana maambukizi ya kifua kikuu, kwa hiyo mama ataendelea na dawa na mtoto ataanzishiwa  Rifampin kwa hiyo mama hapaswi kumnyonyesha mtoto kwa sababu atamzidishia dozi au nguvu ya dawa itakuwa kubwa yaani dawa inayopitia kwenye maziwa  ya mama na dawa anayokunywa mototo. Kwa hiyo mtoto huyo  hapaswi kunyonya.

 

8. Pia katika matumizi ya dawa hii ni vizuri kabisa kupata ushauri wa daktari dawa hii haipaswi kutumika kiholela na ikitokea mtumiaji wa dawa amepata maudhi yakawa yasiyo ya kawaida ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kwa ushauri zaidi na pia kubadilishiwaa dawa kwa sababu katika matibabu ya kutibu kifua kikuu Kuna dawa za daraja la kwanza na la pili.

 

9. Pia kwa akina Mama wajawazito ni vizuri kabisa kupima kifua kikuu mapema Ili kuanza dawa mapema kuepuka na tatizo la kuambukiza mtoto na kusababisha mtoto kushindwa kunyonya kwa sababu maziwa ya mama ni ya muhimu na lazima kabisa kwa sababu mtoto asiponyonya ndicho chanzo cha utapiamlo na kidumaa kwa mtoto.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/12/16/Friday - 10:03:07 pm Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1443

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 web hosting    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu dawa ya kaoline

Post hii inahusu dawa ya kaoline katika kutibu au kuzuia kuharisha ni dawa ambayo imependekezwa kutumiwa hasa kwa wale walioshindwa kutumia dawa ya loperamide.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya mucolytic dawa ya kutibu kikohozi

Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto.

Soma Zaidi...
Fahamu antibiotics ya asili.

Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida.

Soma Zaidi...
Ushauri kabla ya kubeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi ushauri kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, kabisa ya kubeba mimba akina Mama na wachumba wanapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Dawa za mitishamba za kutibu meno

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za mitishamba za kutibu meno

Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi kwenye mdomo na ulimi

Utajifunza dalili za fangasi mdomoni na ulimini, sababu za fangasi wa mdomoni na ulimini, matibabu yeke na njia za kukabiliana nao

Soma Zaidi...
Faida za vidonge vya zamiconal

Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya faida ambazo upatikana kutokana na vidonge vya zamiconal,ni vidonge ambavyo utibu au kusaidia kwenye matatizo ya viungo vya uzazi.

Soma Zaidi...
Fahamu Dawa inayotumika kupunguza maumivu (ibuprofen)

Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin,

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kutumia dawa za ARV

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya aminophylline kutibi maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji

Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.

Soma Zaidi...