Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.
1.1.Rifampsini ni mojawapo ya dawa ambayo imo kwenye daraja la kwanza katika matibabu ya kutibu kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba ni bakteria anayesababisha kuwepo kwa kifua kikuu, kwa hiyo dawa aina ya Rifampin inapotumika kitu cha kwanza ni kuharibu protein ambayo inaitwa DNA ni protein ya bakteria kwa hiyo bakteria huyo anakuwa Hana uwezo wa kuishi tena na ugonjwa uweza kuishia hapo kwa sababu DNA iimeshaharibiwa.
2. Katika matibabu ya kifua kikuu dawa hii kwa kawaida haitibu yenyewe kama yenyewe Bali huwa na mchanganyiko na madawa mengine ambayo ni isoniazid, pyrazinamide na ethambutol na dozi yake huwa na muundo wa RHZE ambapo, R ni Rifampin, H ni isoniazid, Z ni pyrazinamide na E ni ethambutol kwa hiyo dawa hizo utumika zote kwa pamoja katika matibabu ya kwanza ya kifua kikuu na katika matibabu ya pili Rifampin huwa na isoniazid na muundo wao huwa ni RH ambapo R ni Rifampin na H ni isoniazid .
3. Kwa kawaida dawa ya Rifampin utolewa kwa muundo wa vidonge yaana umezwa kwa maji. na ni mara chache mno Kuna Rifampin ambazo utolewa kwenye mishipa ya damu, katika dawa zote za kifua kikuu dawa hii ya Rifampin ndio iliyo na nguvu zaidi na usaidia katika kupambana na bakteria ambaye kwa kitaamu huiitwa TB bacill na pia dawa hii utumika katika daraja la kwanza na la pili katika matibabu ya kutibu kifua kikuu pia ni dawa yenye nguvu kwa sababu uua bakteria wote walio sugu na wote wanaaoanza mashambulizi .
4. Dawa hii pia huwa na maudhi madogo madogo katika kutumia, maudhi hayo ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, kuharisha, maumivu ya kichwa,na pia kuwepo kwa homa pia Kuna baadhi ya watu ambao huwa na viupele wanapokuwa wanatumia dawa hii ya Rifampin pia dawa hii inaweza kabisa kusababisha kupunguza kwa kwa kiasi cha aina ya protein ambayo Kwa kitaamu huiitwa platelate ,na pia kwa wakati mwingine kwa watumiaji wa dawa hii usababisha kupungua kwa kiwango cha damu kuganda .
5. Kiwango cha kupunguza kwa damu kuganda kwa kitaamu huiitwa clotting factors hali inayosababisha kupunguza kwa damu mwilini na kusababisha hali Fulani ambayo Kwa kitaamu huiitwa Anaemia,na maudhi haya hayatokei kila mara ni mara chache na kwa watu wachache kwa hiyo watu wasiogope kutumia dawa hii kwa sababu ni sehemu ya matibabu .
6. Pia dawa hii inaweza kutumiwa na watu wote ila kwa wale ambao wanatumia uzazi wa mpango wenye vichocheo vya progesterone na oestrogen hawapaswi kutumia dawa hii kwa sababu dawa hii inaingiliana na hizi homoni na kusababisha kushika kwa mimba kwa sababu dawa hii ya Rifampin Ina nguvu kuliko hivi vichocheo kwa hiyo kwa wale wanaotumia dawa za kifua kikuu na pia wanatumia njia yoyote ya uzazi wa mpango wanapaswa kuomba ushauri kwa wataalamu wa afya kwa sababu wanaweza kupata mimba bila kutegemea au wanashauliwa kutumia njia nyingine za uzazi wa mpango kwa sababu ni nyingi.
7. Pia na akina Mama wenye maambukizi ya kifua kikuu na wamegundulika siku za mwisho karibia na kujifungua na kwa bahati mbaya na watoto au mtoto aliyezaliwa na yeye ana maambukizi ya kifua kikuu, kwa hiyo mama ataendelea na dawa na mtoto ataanzishiwa Rifampin kwa hiyo mama hapaswi kumnyonyesha mtoto kwa sababu atamzidishia dozi au nguvu ya dawa itakuwa kubwa yaani dawa inayopitia kwenye maziwa ya mama na dawa anayokunywa mototo. Kwa hiyo mtoto huyo hapaswi kunyonya.
8. Pia katika matumizi ya dawa hii ni vizuri kabisa kupata ushauri wa daktari dawa hii haipaswi kutumika kiholela na ikitokea mtumiaji wa dawa amepata maudhi yakawa yasiyo ya kawaida ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kwa ushauri zaidi na pia kubadilishiwaa dawa kwa sababu katika matibabu ya kutibu kifua kikuu Kuna dawa za daraja la kwanza na la pili.
9. Pia kwa akina Mama wajawazito ni vizuri kabisa kupima kifua kikuu mapema Ili kuanza dawa mapema kuepuka na tatizo la kuambukiza mtoto na kusababisha mtoto kushindwa kunyonya kwa sababu maziwa ya mama ni ya muhimu na lazima kabisa kwa sababu mtoto asiponyonya ndicho chanzo cha utapiamlo na kidumaa kwa mtoto.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Soma Zaidi...Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin
Soma Zaidi...PoPosti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo unaweza kutumia iwapo umepata tatizo la kiungulia
Soma Zaidi...Hapa utajifuanza dalili za presha ya kushuka, na dawa ya presha ya kushuka na nJia za kuzuiaama kudhibiti presha ya kushuka
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya griseofulvin ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye ngozi ambazo usababisha mabaka mabaka kwenye ngozi.
Soma Zaidi...