Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.
1.​​​​​1.Rifampsini ni mojawapo ya dawa ambayo imo kwenye daraja la kwanza katika matibabu ya kutibu kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba ni bakteria anayesababisha kuwepo kwa kifua kikuu, kwa hiyo dawa aina ya Rifampin inapotumika kitu cha kwanza ni kuharibu protein ambayo inaitwa DNA ni protein ya bakteria kwa hiyo bakteria huyo anakuwa Hana uwezo wa kuishi tena na ugonjwa uweza kuishia hapo kwa sababu DNA iimeshaharibiwa.
2. Katika matibabu ya kifua kikuu dawa hii kwa kawaida haitibu yenyewe kama yenyewe Bali huwa na mchanganyiko na madawa mengine ambayo ni isoniazid, pyrazinamide na ethambutol na dozi yake huwa na muundo wa RHZE ambapo, R ni Rifampin, H ni isoniazid, Z ni pyrazinamide na E ni ethambutol kwa hiyo dawa hizo utumika zote kwa pamoja katika matibabu ya kwanza ya kifua kikuu na katika matibabu ya pili Rifampin huwa na isoniazid na muundo wao huwa ni RH ambapo R ni Rifampin na H ni isoniazid .
3. Kwa kawaida dawa ya Rifampin utolewa kwa muundo wa vidonge yaana umezwa kwa maji. na ni mara chache mno Kuna Rifampin ambazo utolewa kwenye mishipa ya damu, katika dawa zote za kifua kikuu dawa hii ya Rifampin ndio iliyo na nguvu zaidi na usaidia katika kupambana na bakteria ambaye kwa kitaamu huiitwa TB bacill na pia dawa hii utumika katika daraja la kwanza na la pili katika matibabu ya kutibu kifua kikuu pia ni dawa yenye nguvu kwa sababu uua bakteria wote walio sugu na wote wanaaoanza mashambulizi .
4. Dawa hii pia huwa na maudhi madogo madogo katika kutumia, maudhi hayo ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, kuharisha, maumivu ya kichwa,na pia kuwepo kwa homa pia Kuna baadhi ya watu ambao huwa na viupele wanapokuwa wanatumia dawa hii ya Rifampin pia dawa hii inaweza kabisa kusababisha kupunguza kwa kwa kiasi cha aina ya protein ambayo Kwa kitaamu huiitwa platelate ,na pia kwa wakati mwingine kwa watumiaji wa dawa hii usababisha kupungua kwa kiwango cha damu kuganda .
5. Kiwango cha kupunguza kwa damu kuganda kwa kitaamu huiitwa clotting factors hali inayosababisha kupunguza kwa damu mwilini na kusababisha hali Fulani ambayo Kwa kitaamu huiitwa Anaemia,na maudhi haya hayatokei kila mara ni mara chache na kwa watu wachache kwa hiyo watu wasiogope kutumia dawa hii kwa sababu ni sehemu ya matibabu .
6. Pia dawa hii inaweza kutumiwa na watu wote ila kwa wale ambao wanatumia uzazi wa mpango wenye vichocheo vya progesterone na oestrogen hawapaswi kutumia dawa hii kwa sababu dawa hii inaingiliana na hizi homoni na kusababisha kushika kwa mimba kwa sababu dawa hii ya Rifampin Ina nguvu kuliko hivi vichocheo kwa hiyo kwa wale wanaotumia dawa za kifua kikuu na pia wanatumia njia yoyote ya uzazi wa mpango wanapaswa kuomba ushauri kwa wataalamu wa afya kwa sababu wanaweza kupata mimba bila kutegemea au wanashauliwa kutumia njia nyingine za uzazi wa mpango kwa sababu ni nyingi.
7. Pia na akina Mama wenye maambukizi ya kifua kikuu na wamegundulika siku za mwisho karibia na kujifungua na kwa bahati mbaya na watoto au mtoto aliyezaliwa na yeye ana maambukizi ya kifua kikuu, kwa hiyo mama ataendelea na dawa na mtoto ataanzishiwa Rifampin kwa hiyo mama hapaswi kumnyonyesha mtoto kwa sababu atamzidishia dozi au nguvu ya dawa itakuwa kubwa yaani dawa inayopitia kwenye maziwa ya mama na dawa anayokunywa mototo. Kwa hiyo mtoto huyo hapaswi kunyonya.
8. Pia katika matumizi ya dawa hii ni vizuri kabisa kupata ushauri wa daktari dawa hii haipaswi kutumika kiholela na ikitokea mtumiaji wa dawa amepata maudhi yakawa yasiyo ya kawaida ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kwa ushauri zaidi na pia kubadilishiwaa dawa kwa sababu katika matibabu ya kutibu kifua kikuu Kuna dawa za daraja la kwanza na la pili.
9. Pia kwa akina Mama wajawazito ni vizuri kabisa kupima kifua kikuu mapema Ili kuanza dawa mapema kuepuka na tatizo la kuambukiza mtoto na kusababisha mtoto kushindwa kunyonya kwa sababu maziwa ya mama ni ya muhimu na lazima kabisa kwa sababu mtoto asiponyonya ndicho chanzo cha utapiamlo na kidumaa kwa mtoto.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ,ni dawa ambayo utumiwa na watu wengi kwa matibabu ya ugonjwa wa Malaria.
Soma Zaidi...Fangasi wanaweza kushambulia uke, kwa juu kwenye mashhav ya uke ama kwa ndani. Hali hii inaweza kusababisha miwasho na maumivu pia. Inaweza kusababisha michubuko na kutofurahia tendo la ndoa. Makala hii inakwenda kukujuza dawa na matibabu ya fangasi ukeni
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali ambazo uchangia katika kupunguza nguvu za kiume , hii ni kwa sababu ya wataalamu mbalimbali wanavyosema
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
Soma Zaidi...MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za fangasi na matumizi yake kwa kutumia dawa ya fluconazole kama dawa mojawapo ya fangasi.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukuletea dawa za kutibu ugonjwa wa macho
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.
Soma Zaidi...