Madhara ya Tiba mionzi
Post hii inahusu zaidi madhara ya Tiba mionzi kwa wagonjwa wa saratani, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wanaotumia mionzi katika matibabu ya saratani.
1. Kupoteza hamu ya chakula.
Hii ni mojawapo ya madhara ambayo utokea kwa watumiaji wa mionzi kwa sababu ya kuwepo kwa dawa kwenye damu usababisha kuingilia mfumo wa hamu ya kula kwa hiyo mgonjwa ushindwa kula, kwa hiyo mgonjwa anapaswa kula kidogo kidogo na kwa kila mara na pia anapaswa kula vyakula kama vile supu na vyakula vingine vilaini Ili aweze kuruhusu dawa kufanya kazi maana dawa bila chakula mambo hayaendi vizuri.
2. Mgonjwa usikia uchovu mara kwa mara.
Kwa sababu mionzi uharibifu seli zinazosababisha saratani na vile vile zile ambazo ni nzima nazo uharibiwa na mionzi kwa hiyo tunajua kabisa maisha yetu msingi wake ni seli kwa hiyo seli zikifa bila kufikia mda wake na mambo mengine mwilini yanakwama ndo maana mtu uhisi uchovu kwa hiyo wanaotumia mionzi wanapaswa kupumzika kwa mda wa kutosha, kutembea walau dakika Kumi na Tano kwa siku na kunywa maji mengi, kula chakula Cha kutosha Ili kuupatia mwili nguvu.
3.Mabadiliko ya ngozi.
Kwa wagonjwa wanaotumia mionzi huwa na mabadiliko kwenye ngozi zao , pengine ngozi ubadilika na kuwa pinki, nyeusi, kuhisi moto kwenye ngozi, ngozi kuwa kavu, kuwasha na ngozi kuwa na upele au malengelenge kwa mgonjwa anayetumia mionzi akiona dalili kama hizi hasiogope Bali achukue dawa za kawaida zinazotumika kutibu magonjwa ya ngozi na pia apate ushauri wa daktari Ili kuweza kujua Cha kufanya maana madhara mengine kwenye ngozi huwa yanatisha na kumnyima mgonjwa amani.
4. Mgonjwa huisi kichefuchefu.
Kwa sababu dawa hizi za mionzi zinaharibu seli na pia uingilia mfumo wa chakula na kumfanya mgonjwa kutaka kutapika kila kitu, kwa hiyo mgonjwa anapaswa kukaa woman Ili asitapike, pia anapaswa kula chakula kidogo kidogo kwa wakati b tofauti na pia anapaswa kujiadhari na vyakula vile ambavyo huwa havipendelei Ili kuepuka kutapika kwa kufanya hivyo mgonjwa ataweza kula chakula na dawa zitaweza kufanya kazi.
5. Tukumbuke kuwa mionzi huua seli zinazosababisha saratani na pamoja na zile ambazo ziko kawaida na pia mwili wa binadamu unapaswa kuwa na seli zinatosha Ila kwa sababu ya magonjwa seli zinaharibika kwa mionzi kwa hiyo wagonjwa hawa wanahitaji uangalizi wa karibu na kupewa chakula chenye virutubisho vyote Ili waendelee kuishi na pia jamii inapaswa kuwasaidia na kuwapa ushirikiano wa karibu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 ai web app 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Dawa ya kutibu fangasi wa kwenye mdomo na kinywa
Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi.
Soma Zaidi...Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa
Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa
Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili.
Soma Zaidi...Dawa ya kutibu mapunye
DAWA YA MAPUNYEMatibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo.
Soma Zaidi...Matibabu ya Fangasi ukeni na dawa za fangasi wanaoshambulia uke.
Fangasi wanaweza kushambulia uke, kwa juu kwenye mashhav ya uke ama kwa ndani. Hali hii inaweza kusababisha miwasho na maumivu pia. Inaweza kusababisha michubuko na kutofurahia tendo la ndoa. Makala hii inakwenda kukujuza dawa na matibabu ya fangasi ukeni
Soma Zaidi...